Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aagiza DED Mkalama achunguzwe

wankuru nyankuru

JF-Expert Member
Feb 11, 2019
491
763
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Singida, Bw. Adili Elinipenda amchunguze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkalama, Bw. Godfrey Sanga kwa matumizi mabaya ya fedha za umma.

Baadhi ya tuhuma alizonazo ni kujilipa posho ya safari Machi mwaka huu bila kusafiri, kuwasainisha watumishi wa chini yake vocha na kisha kuwapa ‘asante kidogo’ kwa madai fedha hizo zinaenda mkoani, kujilipa stahiki kabla ya wakati na kuagiza gari liende gereji kwa matengenezo bila nyaraka zozote.

Ametoa agizo hilo leo jioni (Jumamosi, Oktoba 5, 2019), wakati akizungumza na madiwani na watumishi wa Halmashauri hiyo kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Halmshauri hiyo.

“Kuna watumishi wanne uliwaambia wasaini vocha ya sh. 1,320,000. Hii ni kwa safari iliyopangwa kati ya tarehe 15 na 24 Septemba, mwaka huu; ukawapa asante ya sh. 30,000 ukidai kuwa zinatakiwa mkoani. RAS ni kweli hela hiyo ililetwa mkoani?” Alihoji Waziri Mkuu na kujibiwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Dkt. Anjelina Lutambi kwamba hakutoa hayo maagizo.

Alipoulizwa Mweka Hazina wa Wilaya hiyo, Bw. Peniel Mbula kwamba fedha alilipwa nani, mweka hazina huyo alijibu kwamba alikuwa Dodoma kikazi. Mhasibu aliyekaimu nafasi yake, Bi. Lulu Hamadi aliwataja watumishi hao kuwa ni Stella Mawa, Godfrey Mnubi, Richard Laizer na Method Kafuku.

Waziri Mkuu aliwasimamisha watumishi hao na kuwauliza walilipwa hiyo posho ili waende wapi lakini walikosa majibu. Ndipo akawaeleza kwamba walimkabidhi Mkurugenzi na wakalipwa asante ya sh. 30,000.

Alipoulizwa kuhusu malipo ya sh. 1,090,000 ambayo yalilipwa Septemba 9, mwaka huu yalikuwa ya nini, Mkurugenzi huyo alijibu kuwa ni ya stahiki zake za kila mwezi ambapo kati ya hizo, sh. 600,000/- ni za malipo ya nyumba; sh. 230,000 ni za umeme na sh. 260,000 ni za simu. Lakini hakuweza kujibu ni kwa nini amejilipa kabla mwezi haujaisha.

Kuhusu gari la elimu lenye namba za usajili STK 913 lililopelekwa gereji kupakwa rangi kwa gharama ya sh. milioni saba, Waziri Mkuu alitaka aoneshe dokezo lililotumika kupitisha idhini hiyo na malipo hayo lakini akajibiwa kwamba hakuna utaratibu wa kuandika dokezo pindi magari ya Halmashauri yanapoenda kufanyiwa matengenezo bali wanapeana taarifa kwa mdomo tu.

“Kamanda wa TAKUKURU leta maafisa kutoka mkoani waje wafanye ukaguzi wa kila jambo ambalo limeainishwa. Hatuwezi kuacha Halmashauri iendeshwe kienyeji bila kufuata taratibu. Mkalama inaonekana chafu kumbe tatizo ni mtu mmoja, mnasaini vocha halafu mnamsingizia RAS,” alisema.

“Ajenda ya kikao changu nanyi watumishi wenzangu, nilitaka tuambiane kwamba ni lazima tutunze mali na fedha za Serikali. Waheshimiwa Madiwani ni lazima msimamie Halmashauri yenu na mhoji kila senti imetumika vipi. Kama ni jengo nendeni mkakague, kama ni kisima nendeni mkaangalie,” alisisitiza.

“Pia niwasihi Waheshimiwa Madiwani wenzangu, msikubali kutumika kupitisha matmizi ya fedha ambayo si sahihi,” aliongeza.

Watumishi wa Halmashauri hii mfanye kazi, muache ubabaishaji sababu Serikali hii iko makini sana. Msiishi kwa mazoea, kwa sababu wakati siyo wenyewe na tena muache kutengezeza syndicates,” aliwaonya.

Pia amemuonya Afisa Manunuzi wa wilaya hiyo, Bw. Dickson Mataramba aache kutumika na kufanya kazi kwa mazoea kwa kupandisha bei ya sh. elfu 2000 hadi 3,000 kwenye vifaa wanavyoagiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amekataa kuweka jiwe la msingi la Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya kwa sababu lilikataliwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge na uchunguzi wake bado haujakamilika.

“Jiwe la msingi mlilonipangia kuweka leo kwenye hospitali ya wilaya siweki hadi TAKUKURU wakamilishe kazi ya uchunguzi kuhusu mikataba iliyotumika. Mkikamilisha uchunguzi mniite, nitakuja kulizindua likiwa limekamilika,” amesema.
 
Hawa Ma DED makada wa ccm watasumbua sana.Mtu katoka katika upiga debe wa chama hajui utumishi wa umma unampa ukurugenzi uDc U Rc unategemea nini?lazima achukue chake mapema
Ushahidi RC Dsm
 
Panngo kilo 6,
Umeme 230000
Simu 260000
Salary nasikia emu NNE,dah bongo hii,wakati gradueti WA edukesheni anakula kama kilo tano na semaninni kwa mwezi
Alipe
Luku
Wota
Transpoti
Has
Fuud na development juu, bado hajakamatia totoz ya kujipoza,lazima ufisaji ushamiri tu
 
This is just a "tip of an iceberg". Kila mwaka CAG anaibua madudu mara 5,000,000 ya haya ila hawamsikilizi. Hawa wakurugenzi wengi wamechomekwachomekwa kindugu.
 
Aaah watumbue kotekote sasa na sehemu walizopo ndugu zao kama Ileje huko,mkurugenzi anajilipa tu kiss haguswi na PM ni ndugu yake,nenda na huko
 
Kama ipo kisheria ni haki yake DED, acheni wivu wa kitoto. Alichokisea DED ni kujilipa kabla ya mwezi kuisha. Hiyo ndo audit query.
Posho ya simu 260,000 kwa mwezi? Shikamoo mkurugezi, hivi huwa unaongea na mungu? Umeme laki mbili kwako unakiwanda Cha usindikaji minofu?
 
Hizi nafasi zingekuwa zinatangazwa kama nafasi nyingine za ajira watanzania wanaokidhi vigezo waombe watakaofauli kufika kwenye oral interview, interview ifanyike mubashara tuwaone kwenye luninga ili atakayepita nasi huku tumwone yes anafaa. Wenzetu Kenya wanafanya hivi kwenye nafasi ya jaji mkuu na jaji msaidizi huwa inavutia sana kuona jinsi watu wanavyoulizwa maswali kuntu hadi una-apreciate kuwa mtu aliyepita kweli anafaa. Sasa huu utaratibu wa kupeana vyeo kama namna ya kutoa asante au kulipa fadhila ndio matokeo haya.
 
Kama ipo kisheria ni haki yake DED, acheni wivu wa kitoto. Alichokisea DED ni kujilipa kabla ya mwezi kuisha. Hiyo ndo audit query.
Sheria za kinyonyaji, wakati zinapitishwa na chadema walikuwepo bungeni au walitoka?
 
Hizi nafasi zingekuwa zinatangazwa kama nafasi nyingine za ajira watanzania wanaokidhi vigezo waombe watakaofauli kufika kwenye oral interview, interview ifanyike mubashara tuwaone kwenye luninga ili atakayepita nasi huku tumwone yes anafaa. Wenzetu Kenya wanafanya hivi kwenye nafasi ya jaji mkuu na jaji msaidizi huwa inavutia sana kuona jinsi watu wanavyoulizwa maswali kuntu hadi una-apreciate kuwa mtu aliyepita kweli anafaa. Sasa huu utaratibu wa kupeana vyeo kama namna ya kutoa asante au kulipa fadhila ndio matokeo haya.
Wengine ni kakazao nyumba ndogo tu hata ccm hawajulikani
 
Back
Top Bottom