Kuna tetesi zimeanza kuwa Rais Kikwete huenda akavunja baraza lake la mawaziri baada ya kikao cha Bunge kinachoisha wiki hii. Kuvunja huku kwa cabinet itakuwa ni utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba kwa serikali kama ilivyokuwa kwa chama tawala. Ni ukweli usiopingika kuwa serikali imepwaya sana na kila mwananchi anaonesha kukata tamaa.
Rais, Waziri Mkuu na baraza la mawaziri wote wanaonekana ni legelege. Hivyo basi kuna haja ya kuvunja cabinet na kuunda jipya, mbinu ambayo hutumiwa na viongozi wengi kujaribu kuleta matumaini mapya pale ambapo serikali zao zinapokuwa zimepoteza imani ya wananchi kama ilivyo kwa serikali ya JK.
Tetesi hizi zimenifanya niote jinsi ambavyo nchi yetu ingenyooka kama JK angekuwa na ujasiri wa kumteua John Pombe Magufuli kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania. Magufuli amekuwa na rekodi isiyo na mfano wa kuwa mchapa kazi mahiri tangu serikali ya Mkapa. Si muoga wa kufanya maamuzi, ni mtu vibrant na wananchi wengi wanamkubnali. He is a no-nonsense leader na angeleta uhai mpya serikalini.
Kwa bahati mbaya najua kuwa ndoto zangu za kumuona mtu mwenye calibre ya Magufuli anakuwa PM haziwezi kutimia kwa sababu zifuatazo:
1. Rais Jakaya Kikwete (kama Marais wengi wa Afrika) hataki mtu amzidi umaarufu (outshine). Ndiyo maana alimchagua mtu kama Mizengo Pinda kuwa Waziri Mkuu ambaye amepwaya sana kwenye nafasi hiyo mpaka wengine wanamkumbuka Edward Lowassa licha ya ufisadi wake. JK is a lame duck president, anamaliza kipindi cha mwisho. Hastahili kumhofia Magufuli, lakini bado anamgwaya.
2. Kikwete alitofautiana hadharani na Magufuli kuhusu bomoa bomoa. Wakati Magufuli anataka sheria iwe msumeno, JK anataka ulegelege uendelee.
3. JK hawezi kufanya maamuzi magumu. Hajui tatito la serikali yake liko wapi. Angekuwa kocha wa timu ya mpira, Kikwete unaweza kumfananisha sawasawa na Arsene Wenger ambaye anaona nyumba yake inawaka moto lakini anashindwa kufanya maamuzi magumu ya haraka.
Rais, Waziri Mkuu na baraza la mawaziri wote wanaonekana ni legelege. Hivyo basi kuna haja ya kuvunja cabinet na kuunda jipya, mbinu ambayo hutumiwa na viongozi wengi kujaribu kuleta matumaini mapya pale ambapo serikali zao zinapokuwa zimepoteza imani ya wananchi kama ilivyo kwa serikali ya JK.
Tetesi hizi zimenifanya niote jinsi ambavyo nchi yetu ingenyooka kama JK angekuwa na ujasiri wa kumteua John Pombe Magufuli kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania. Magufuli amekuwa na rekodi isiyo na mfano wa kuwa mchapa kazi mahiri tangu serikali ya Mkapa. Si muoga wa kufanya maamuzi, ni mtu vibrant na wananchi wengi wanamkubnali. He is a no-nonsense leader na angeleta uhai mpya serikalini.
Kwa bahati mbaya najua kuwa ndoto zangu za kumuona mtu mwenye calibre ya Magufuli anakuwa PM haziwezi kutimia kwa sababu zifuatazo:
1. Rais Jakaya Kikwete (kama Marais wengi wa Afrika) hataki mtu amzidi umaarufu (outshine). Ndiyo maana alimchagua mtu kama Mizengo Pinda kuwa Waziri Mkuu ambaye amepwaya sana kwenye nafasi hiyo mpaka wengine wanamkumbuka Edward Lowassa licha ya ufisadi wake. JK is a lame duck president, anamaliza kipindi cha mwisho. Hastahili kumhofia Magufuli, lakini bado anamgwaya.
2. Kikwete alitofautiana hadharani na Magufuli kuhusu bomoa bomoa. Wakati Magufuli anataka sheria iwe msumeno, JK anataka ulegelege uendelee.
3. JK hawezi kufanya maamuzi magumu. Hajui tatito la serikali yake liko wapi. Angekuwa kocha wa timu ya mpira, Kikwete unaweza kumfananisha sawasawa na Arsene Wenger ambaye anaona nyumba yake inawaka moto lakini anashindwa kufanya maamuzi magumu ya haraka.