beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema mkakati wa Ujenzi wa Viwanda ndio jibu sahihi la kupunguza changamoto ya Ajira Nchini kwa ngazi zote.
Amesema, "Changamoto ya Ajira ipo duniani kote ikiwemo hapa kwetu Tanzania. Kila Serikali inaweka utaratibu mzuri wa kukabiliana nayo"
Ameeleza hayo Bungeni wakati akimjibu Mbunge Nusrat Hanje aliyehoji ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inawatambua Vijana wanaokwama kupata Ajira kwa kuulizwa kigezo cha Kidato cha Nne.
Mbunge huyo alisema, "Kuna ugumu wa Vijana waliomaliza Darasa la Saba kupata Ajira hususan kwenye Taasisi za Serikali, hata kama wamepata mafunzo katika fani mbalimbali kwenye Vyuo vya Ufundi huku kigezo kikiwa ni Cheti cha Kidato cha Nne"
#JamiiForums
Amesema, "Changamoto ya Ajira ipo duniani kote ikiwemo hapa kwetu Tanzania. Kila Serikali inaweka utaratibu mzuri wa kukabiliana nayo"
Ameeleza hayo Bungeni wakati akimjibu Mbunge Nusrat Hanje aliyehoji ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inawatambua Vijana wanaokwama kupata Ajira kwa kuulizwa kigezo cha Kidato cha Nne.
Mbunge huyo alisema, "Kuna ugumu wa Vijana waliomaliza Darasa la Saba kupata Ajira hususan kwenye Taasisi za Serikali, hata kama wamepata mafunzo katika fani mbalimbali kwenye Vyuo vya Ufundi huku kigezo kikiwa ni Cheti cha Kidato cha Nne"
#JamiiForums