Waziri Mkuu; Hii ndo dawa ya makazi holela kwenye miji mipya Tanzania

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,047
Utangulizi.
Napenda sana kukusalimu kwa heshima kuu na kukupa pole kwa majukumu mazito uliyo nayo ndani ya taifa hili. Napenda kukupongeza kwa kuwa ninaamini wewe ni mmoja wa watu wachache ninaodiriki kusema mnamuelewa sana Mh Raisi. Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Raisi katika kumuapisha Naibu Waziri alilalamika sana kuhusu baadhi ya watendaji kutomuelewa juu ya nini hasa anakitaka, lile lilikuwa ni jambo zito sana na napenda kukupongeza kwa kuwa ninajua wewe ni mmoja ya watendaji wanaomuelewa sana Mh. Raisi.

Tatizo na ujenzi/makazi holela.
Napenda nirudi kwenye mada inayohusu dawa ya kumaliza makazi holela hasa kwenye majiji makubwa na mikoa mbalimbali hapa Tanzania ( Dar es Salaam,Iringa,Songwe, Simiyu,Kigoma Mwanza, Morogoro, Singida, Mbeya na Arusha) bila kusahau miji unayokua kama Kahama na mingineyo.

Mh Waziri Mkuu, nadhani unafahamu kuwa kati ya maeneo ambayo kama nchi na taifa tulifeli tangu mwanzo ni kwenye kudhibiti makazi holela. Mfano ni maeneo ya magomeni, tandale, mbagala, gongo la mboto, kimara, temeke, mtoni, tabata na mengineyo mengi.

Lakini vilevile kuna maeneo mapya ambayo kutokana na kuanza kuendelezwa kwa kiwango kikubwa hivi karibuni( Mfano Bunju, Madale, Chanika, Goba, Mbezi Makabe, Kibamba, Kinyerezi, Malamba Mawili n.k) serikali ilitakiwa kuja na mipango madhubuti ili kuhakikisha kuwa ingawa hayajapimwa basi yanajengwa vizuri kama kuhakikisha kuwa at least kwenye kila nyumba ya mtu kunakuwa na barabara inayofika kwake kwa kuwa barabara sio tu zinapendeshesha eneo ila zinaleta mpangilio zaidi na kurahisisha huduma kutolewa kipindi cha majanga kama moto na vilevile kipindi inapotokea mkazi wa eneo husika anaumwa.

Dhumuni la kukuandikia Mh. Waziri Mkuu humu sio kwa sababu simuamini Mh. Lukuvi ila naamini ukilisimamia wewe Mh Lukuvi atalisimamia vizuri na litaleta matokeo chanya. Ninapenda kwa jinsi unavomsaidia raisi wetu mpendwa kwa kuibua changamoto na kuzishughulikia. Nakuomba Mh umsaidie Mh raisi ili aweze kukumbukwa kwenye hili maana makazi holela ni moja ya vitu vinavyoharibu sana picha ya taifa letu.

Nini Kifanyike?
Najua kuna watu wanaweza kusema kuwa dawa la tatizo hili ni makazi kupiwa na kutolewa hati lakini changamoto ninayoiona hapa ni kuwa suala la upimaji limezidi kuwa changamoto kiasi ambacho watu wanazidi kujenga na upimaji umekuwa ukifanyik kwa kiwango cha chini sana. Hivyo Muheshimiwa napendekeza kama serikali mfanye mabadiriko yafuatayo na myatengenezee sera kabisa.

1. Mzipe mamlaka na mzielekeze serikali za mitaa na vijiji kuhusu kupanga maeneo yao( Hasa kwenye maeneo mapya mabayo saivi yameanza kupata uendelezwaji wa kasi sana). Kwenye hili mzielekeze serikali za mitaa na vijiji na watendaji wa kata kuhakikisha kwenye mitaa yao kuna barabara zilizopitishwa zinazohakikisha kila nyumba inapitiwa na barabara yenye uwezo wa kupitisha gari kubwa kama la fire na hata magari wawili kuweza kupishana . Hili likifanyika mtawezesha kupatikana kwa mitaa inayoeleweka na iliyo bora hivo makazi yatawezekana kupangika kiurahisi na hata upimaji utawezekana kiurahisi kama ukija kufanyika badae.

2. Mzielekeze mamlaka na serikali za mitaa na vijiji na watendaji wake kuzisajili barabara zote zilizo kwenye mitaa yao na kuzuia ujenzi wowote kufanyika kuziba barabara izo. Mzipe mamlaka kumvunjia mtu yeyote atakayejenga kwenye baarabara izo zilizosajiliwa

3. Mzipe serikali za mitaa mamalaka ya kusimamisha ujenzi wowote ule unaoonekana unakiuka taratibu za makazi bora kama vile mtu kujenga kwenye mto, njia za maji, kwenye barabara, kuziba njia au kujenga tofauti na mpangilio mzuri uliopo.

Mh waziri Mkuu kama suala la upimaji makazi kabla ya watu kujenga litakuwa gumu napenda kukuhakikishia mkitumia njia hizi hatutakuwa na makazi holela kwa kuwa mkifanya hivi mitaa itapangika vizuri na hata upimaji ukija badae utaweza kurasimisha maeneo ambayo yameshapangika vizuri.


Naomba Kuwasilisha.
 
Utangulizi.
Napenda sana kukusalimu kwa heshima kuu na kukupa pole kwa majukumu mazito uliyo nayo ndani ya taifa hili. Napenda kukupongeza kwa kuwa ninaamini wewe ni mmoja wa watu wachache ninaodiriki kusema mnamuelewa sana Mh Raisi. Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Raisi katika kumuapisha Naibu Waziri alilalamika sana kuhusu baadhi ya watendaji kutomuelewa juu ya nini hasa anakitaka, lile lilikuwa ni jambo zito sana na napenda kukupongeza kwa kuwa ninajua wewe ni mmoja ya watendaji wanaomuelewa sana Mh. Raisi.

Tatizo na ujenzi/makazi holela.
Napenda nirudi kwenye mada inayohusu dawa ya kumaliza makazi holela hasa kwenye majiji makubwa hapa Tanzania ( Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha) bila kusahau miji unayokua kama Kahama na mingineyo.

Mh Waziri Mkuu, nadhani unafahamu kuwa kati ya maeneo ambayo kama nchi na taifa tulifeli tangu mwanzo ni kwenye kudhibiti makazi holela. Mfano ni maeneo ya magomeni, tandale, mbagala, gongo la mboto, kimara, temeke, mtoni, tabata na mengineyo mengi.

Lakini vilevile kuna maeneo mapya ambayo kutokana na kuanza kuendelezwa kwa kiwango kikubwa hivi karibuni( Mfano Bunju, Madale, Chanika, Goba, Mbezi Makabe, Kibamba, Kinyerezi, Malamba Mawili n.k) serikali ilitakiwa kuja na mipango madhubuti ili kuhakikisha kuwa ingawa hayajapimwa basi yanajengwa vizuri kama kuhakikisha kuwa at least kwenye kila nyumba ya mtu kunakuwa na barabara inayofika kwake kwa kuwa barabara sio tu zinapendeshesha eneo ila zinaleta mpangilio zaidi na kurahisisha huduma kutolewa kipindi cha majanga kama moto na vilevile kipindi inapotokea mkazi wa eneo husika anaumwa.

Dhumuni la kukuandikia Mh. Waziri Mkuu humu sio kwa sababu simuamini Mh. Lukuvi ila naamini ukilisimamia wewe Mh Lukuvi atalisimamia vizuri na litaleta matokeo chanya. Ninapenda kwa jinsi unavomsaidia raisi wetu mpendwa kwa kuibua changamoto na kuzishughulikia. Nakuomba Mh umsaidie Mh raisi ili aweze kukumbukwa kwenye hili maana makazi holela ni moja ya vitu vinavyoharibu sana picha ya taifa letu.

Nini Kifanyike?
Najua kuna watu wanaweza kusema kuwa dawa la tatizo hili ni makazi kupiwa na kutolewa hati lakini changamoto ninayoiona hapa ni kuwa suala la upimaji limezidi kuwa changamoto kiasi ambacho watu wanazidi kujenga na upimaji umekuwa ukifanyik kwa kiwango cha chini sana. Hivyo Muheshimiwa napendekeza kama serikali mfanye mabadiriko yafuatayo na myatengenezee sera kabisa.

1. Mzipe mamlaka na mzielekeze serikali za mitaa kuhusu kupanga maeneo yao( Hasa kwenye maeneo mapya mabayo saivi yameanza kupata uendelezwaji wa kasi sana). Kwenye hili mzielekeze serikali za mitaa na watendaji wa kata kuhakikisha kwenye mitaa yao kuna barabara zilizopitishwa zinazohakikisha kila nyumba inapitiwa na barabara yenye uwezo wa kupitisha gari kubwa kama la fire. Hili likifanyika mtawezesha kupatikana kwa mitaa inayoeleweka hivo makazi yatawezekana kupangika kiurahisi n ahata upimaji utawezekana kiurahisi kama ukija kufanyika badae.

2. Mzielekeze mamlaka na serikali za mitaa na watendaji wake kuzisajili barabara zote zilizo kwenye mitaa yao na kuzuia ujenzi wowote kufanyika kuziba barabara izo. Mzipe mamlaka kumvunjia mtu yeyote atakayejenga kwenye baarabara izo zilizosajiliwa

3. Mzipe serikali za mitaa mamalaka ya kusimamisha ujenzi wowote ule unaoonekana unakiuka taratibu za makazi bora kama vile mtu kujenga kwenye mto, njia za maji, kwenye barabara n.k

Mh waziri Mkuu kama suala la upimaji makazi kabla ya watu kujenga litakuwa gumu napenda kukuhakikishia mkitumia njia hizi hatutakuwa na makazi holela kwa kuwa mkifanya hivi mitaa itapangika vizuri n ahata upimaji ukija badae utaweza kurasimisha maeneo ambayo yameshapangika vizuri.


Naomba Kuwasilisha.
Ninakuunga mkono 100%
Hili suala la kusibiri bajeti,ndo viwanja vipimwe ni kikwazo,na ndiyo chimbuko la ujenzi holela.
 
Uko sawa kabisa. Nimebahatika kukaa maeneo ambayo muuzaji alikuwa mstaharabu; hadi raha. Barabara zimenyooka utasema kumepimwa. Lakini wenye viwanja wengi hawana ustaharabu. Wanaitaji usimamizi was serikali za mitaa ili kila Nyumba iwe na barabara. Wizara imeshashindwa kupima. Wa decentralize tu. Kwani kupima kienyeji kuna madhara? Watoe muongozo kuwa huruhusiwi kuuza kiwanja kisicho na barabara.
 
Umezungumza vyema sana kijana. Tatizo siasa zinaathiri sana maendeleo ya hii nchi, hapo watu wakizuiliwa kujenga holela holela utasikia CHADEMA wanakuja na kuiita hii serikali kuwa ni ya kidicteta. Kuna kila sababu ya kuangalia upya nia na madhumuni ya hivi vyama vya siasa, maana vyenyewe vipo busy kupinga kila jambo linalofanyika na chama tawala kitu ambacho kinakwamisha sana juhudi za maendeleo kama hizi.
Otherwise wazo lako ni zuri sana bila shaka Mh. waziri mkuu atalifanyia kazi.
 
Ukitaka kupata karaha, tua pale JNIA nyakati za mchana na uwe siti ya dirishani halafu ndege iwe inakata kona kutafuta runway. Hizo bati juu ya slums ni kichekesho. Yaani ni aibu kwamba ile ndio "first impression" wageni wanayoipata wanapoingia Tanzania. Bora kuhamisha ule uwanja uende maporini huko maeneo ya Mkuranga au Kisarawe.

Sasa JNIA is the "heart of the City" sijui "Welcome to the Haven of Peace" sijui huko "mikoani" hali ikoje if viewed with bird's eye. Majigambo meeengi hali halisi sifuri!
 
Kwa mtazamo wangu moja ya mambo muhimu ambayo ni lazima yafanyike ili kuondokana na makazi holela ni yafuatayo:
1. Sheria zote duniani hata hapa Tanzania zinakataza kujenga bila kupima na bila mchoro wa nyumba. Hili litekelezwe Tanzania bila kuoneana aibu su kuangalia wapiga kura kulalamika.
2. Kila kiwanja kilichopimwa ni lazima kiendelezwe ndani ya miaka mitatu. Nadhani hili pia lipo tayari kwenye sheria, basi litekelezwe. Siasa ziachwe!
3. Ni marufuku mtu kumiliki shamba ndani ya mji/jiji la zaidi ya eka moja au mbili. Mapori yote yapimwe au kodi ipandishwe kwa viwanja ambavyo havijapimwa. Umiliki wa kiwanja au shamba ambalo halijapimwa eneo la mjini iwe ni jambo la anasa (ukibwa wa kodi).
4. Viongozi wa Tanzania ndio vikwazo sana kwenye upimaji ardhi Tanzania. Wanamiliki maeneo makubwa makubwa mijini. Mfano, Goba, madale, mapinga, mbweni, kinyerezi, etc. Viongozi wa Tanzania ndio wanaozuia viwanja kupimwa kwa wingi. Maeneo yao yatanyang'anywa, hawapendi hilo.
5. Mkoa mzima wa Dar ni tayari eneo la mji mkubwa, mikoa mingine yatambuliwe maeneo ambayo ni future city areas, ukijenga kiholela huko adhabu ijumuishe na kifungo miaka miwili angalau.
6. Serikali pia ipime barabara tu angalau na izilime. Hili linaweza kufanyika kama kupima viwanja kumewashinda.
7. Serikali za manispaa na majiji ziache kutegemea kuuza viwanja ili kupata mapato. Hili nalo ni kioja cha aina yake. Unakuta manispaa inabuni chanzo cha mapato upimaji wa viwanja! Yaani wawalipe fidia kiduchu wakazi halafu wao waviuze vikiwa vimepimwa kwa bei juu zaidi. Ndio maana wanaacha ardhi isiyopimwa kama mtaji wa kuendeshea serikali zao hapo baadae.
 
Umezungumza vyema sana kijana. Tatizo siasa zinaathiri sana maendeleo ya hii nchi, hapo watu wakizuiliwa kujenga holela holela utasikia CHADEMA wanakuja na kuiita hii serikali kuwa ni ya kidicteta. Kuna kila sababu ya kuangalia upya nia na madhumuni ya hivi vyama vya siasa, maana vyenyewe vipo busy kupinga kila jambo linalofanyika na chama tawala kitu ambacho kinakwamisha sana juhudi za maendeleo kama hizi.
Otherwise wazo lako ni zuri sana bila shaka Mh. waziri mkuu atalifanyia kazi.

Ww ni mpuuzi wa kiwango cha juu, ni wapi umewahi kusikia cdm wakipinga mipango miji? Wanaolalamika kuvunjiwa ni wananchi waliojenga kwa kujinyima bila kujali vyama vyao. Kama unaiwakilisha ccm basi unajishuku kwa upuuzi wa serekali yenu. Huyu mleta uzi ameshauri miji ipangwe mapema na sio kusubiri makada wa ccm wachukue rushwa kwa kuruhusu makazi holela, kisha waje kuvunjiwa na makada wenzao.
 
Mkuu umetoa legislative hoja na inayoendana na hali halisi tulipiganie kuanzia leo tuhakikishe linafika kwa wakubwa tena kwa umuhimu wake naunga mkono hoja
Asante sana mkuu. Kitu ninachoipendea serikali hii ni uharaka wao kwenye kuchukua mawazo chanya. Naamini hili watalifanyia kazi.
 
Kwa mtazamo wangu moja ya mambo muhimu ambayo ni lazima yafanyike ili kuondokana na makazi holela ni yafuatayo:
1. Sheria zote duniani hata hapa Tanzania zinakataza kujenga bila kupima na bila mchoro wa nyumba. Hili litekelezwe Tanzania bila kuoneana aibu su kuangalia wapiga kura kulalamika.
2. Kila kiwanja kilichopimwa ni lazima kiendelezwe ndani ya miaka mitatu. Nadhani hili pia lipo tayari kwenye sheria, basi litekelezwe. Siasa ziachwe!
3. Ni marufuku mtu kumiliki shamba ndani ya mji/jiji la zaidi ya eka moja au mbili. Mapori yote yapimwe au kodi ipandishwe kwa viwanja ambavyo havijapimwa. Umiliki wa kiwanja au shamba ambalo halijapimwa eneo la mjini iwe ni jambo la anasa (ukibwa wa kodi).
4. Viongozi wa Tanzania ndio vikwazo sana kwenye upimaji ardhi Tanzania. Wanamiliki maeneo makubwa makubwa mijini. Mfano, Goba, madale, mapinga, mbweni, kinyerezi, etc. Viongozi wa Tanzania ndio wanaozuia viwanja kupimwa kwa wingi. Maeneo yao yatanyang'anywa, hawapendi hilo.
5. Mkoa mzima wa Dar ni tayari eneo la mji mkubwa, mikoa mingine yatambuliwe maeneo ambayo ni future city areas, ukijenga kiholela huko adhabu ijumuishe na kifungo miaka miwili angalau.
6. Serikali pia ipime barabara tu angalau na izilime. Hili linaweza kufanyika kama kupima viwanja kumewashinda.
7. Serikali za manispaa na majiji ziache kutegemea kuuza viwanja ili kupata mapato. Hili nalo ni kioja cha aina yake. Unakuta manispaa inabuni chanzo cha mapato upimaji wa viwanja! Yaani wawalipe fidia kiduchu wakazi halafu wao waviuze vikiwa vimepimwa kwa bei juu zaidi. Ndio maana wanaacha ardhi isiyopimwa kama mtaji wa kuendeshea serikali zao hapo baadae.
Asante mkuu. Mawazo yako ni chanya pia ila hofu yangu ni kuwa kwenye utekelezaji wake yataturudisha huku huku nyuma tunakotaka kutoka. Kutokana na complications zake kwenye utekelezaji.
 
Namba moja na mbili Tanga inafanyika sana. Kwa kweli tanga mjini wamejitahidi sana katika kupanga mji...
Asante mdau kwa mchango wako. Tupigane haya yafanyike kote kwa muongozo wa serikali. italeta maana zaidi. Tanzania yenye makazi yaliyopangiliwa inawezekana sana.
 
Ukitaka kupata karaha, tua pale JNIA nyakati za mchana na uwe siti ya dirishani halafu ndege iwe inakata kona kutafuta runway. Hizo bati juu ya slums ni kichekesho. Yaani ni aibu kwamba ile ndio "first impression" wageni wanayoipata wanapoingia Tanzania. Bora kuhamisha ule uwanja uende maporini huko maeneo ya Mkuranga au Kisarawe.

Sasa JNIA is the "heart of the City" sijui "Welcome to the Haven of Peace" sijui huko "mikoani" hali ikoje if viewed with bird's eye. Majigambo meeengi hali halisi sifuri!
Kweli kabisa mdau. Kinachouma zaidi watu wengi wanaonekana kutoumia na jinsi makazi yetu yanavoonekana kutopangika vizuri.
 
Uko sawa kabisa. Nimebahatika kukaa maeneo ambayo muuzaji alikuwa mstaharabu; hadi raha. Barabara zimenyooka utasema kumepimwa. Lakini wenye viwanja wengi hawana ustaharabu. Wanaitaji usimamizi was serikali za mitaa ili kila Nyumba iwe na barabara. Wizara imeshashindwa kupima. Wa decentralize tu. Kwani kupima kienyeji kuna madhara? Watoe muongozo kuwa huruhusiwi kuuza kiwanja kisicho na barabara.
Kuna maeneo wauzaji wamejitahidi sana kwa kweli. Hili tukilifanya rasmi kwa mgongo na support ya aerikali litapendezesha sana maeneo mengi mkuu.
 
Utangulizi.
Napenda sana kukusalimu kwa heshima kuu na kukupa pole kwa majukumu mazito uliyo nayo ndani ya taifa hili. Napenda kukupongeza kwa kuwa ninaamini wewe ni mmoja wa watu wachache ninaodiriki kusema mnamuelewa sana Mh Raisi. Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Raisi katika kumuapisha Naibu Waziri alilalamika sana kuhusu baadhi ya watendaji kutomuelewa juu ya nini hasa anakitaka, lile lilikuwa ni jambo zito sana na napenda kukupongeza kwa kuwa ninajua wewe ni mmoja ya watendaji wanaomuelewa sana Mh. Raisi.

Tatizo na ujenzi/makazi holela.
Napenda nirudi kwenye mada inayohusu dawa ya kumaliza makazi holela hasa kwenye majiji makubwa hapa Tanzania ( Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha) bila kusahau miji unayokua kama Kahama na mingineyo.

Mh Waziri Mkuu, nadhani unafahamu kuwa kati ya maeneo ambayo kama nchi na taifa tulifeli tangu mwanzo ni kwenye kudhibiti makazi holela. Mfano ni maeneo ya magomeni, tandale, mbagala, gongo la mboto, kimara, temeke, mtoni, tabata na mengineyo mengi.

Lakini vilevile kuna maeneo mapya ambayo kutokana na kuanza kuendelezwa kwa kiwango kikubwa hivi karibuni( Mfano Bunju, Madale, Chanika, Goba, Mbezi Makabe, Kibamba, Kinyerezi, Malamba Mawili n.k) serikali ilitakiwa kuja na mipango madhubuti ili kuhakikisha kuwa ingawa hayajapimwa basi yanajengwa vizuri kama kuhakikisha kuwa at least kwenye kila nyumba ya mtu kunakuwa na barabara inayofika kwake kwa kuwa barabara sio tu zinapendeshesha eneo ila zinaleta mpangilio zaidi na kurahisisha huduma kutolewa kipindi cha majanga kama moto na vilevile kipindi inapotokea mkazi wa eneo husika anaumwa.

Dhumuni la kukuandikia Mh. Waziri Mkuu humu sio kwa sababu simuamini Mh. Lukuvi ila naamini ukilisimamia wewe Mh Lukuvi atalisimamia vizuri na litaleta matokeo chanya. Ninapenda kwa jinsi unavomsaidia raisi wetu mpendwa kwa kuibua changamoto na kuzishughulikia. Nakuomba Mh umsaidie Mh raisi ili aweze kukumbukwa kwenye hili maana makazi holela ni moja ya vitu vinavyoharibu sana picha ya taifa letu.

Nini Kifanyike?
Najua kuna watu wanaweza kusema kuwa dawa la tatizo hili ni makazi kupiwa na kutolewa hati lakini changamoto ninayoiona hapa ni kuwa suala la upimaji limezidi kuwa changamoto kiasi ambacho watu wanazidi kujenga na upimaji umekuwa ukifanyik kwa kiwango cha chini sana. Hivyo Muheshimiwa napendekeza kama serikali mfanye mabadiriko yafuatayo na myatengenezee sera kabisa.

1. Mzipe mamlaka na mzielekeze serikali za mitaa kuhusu kupanga maeneo yao( Hasa kwenye maeneo mapya mabayo saivi yameanza kupata uendelezwaji wa kasi sana). Kwenye hili mzielekeze serikali za mitaa na watendaji wa kata kuhakikisha kwenye mitaa yao kuna barabara zilizopitishwa zinazohakikisha kila nyumba inapitiwa na barabara yenye uwezo wa kupitisha gari kubwa kama la fire. Hili likifanyika mtawezesha kupatikana kwa mitaa inayoeleweka hivo makazi yatawezekana kupangika kiurahisi n ahata upimaji utawezekana kiurahisi kama ukija kufanyika badae.

2. Mzielekeze mamlaka na serikali za mitaa na watendaji wake kuzisajili barabara zote zilizo kwenye mitaa yao na kuzuia ujenzi wowote kufanyika kuziba barabara izo. Mzipe mamlaka kumvunjia mtu yeyote atakayejenga kwenye baarabara izo zilizosajiliwa

3. Mzipe serikali za mitaa mamalaka ya kusimamisha ujenzi wowote ule unaoonekana unakiuka taratibu za makazi bora kama vile mtu kujenga kwenye mto, njia za maji, kwenye barabara n.k

Mh waziri Mkuu kama suala la upimaji makazi kabla ya watu kujenga litakuwa gumu napenda kukuhakikishia mkitumia njia hizi hatutakuwa na makazi holela kwa kuwa mkifanya hivi mitaa itapangika vizuri n ahata upimaji ukija badae utaweza kurasimisha maeneo ambayo yameshapangika vizuri.


Naomba Kuwasilisha.

Utangulizi.
Napenda sana kukusalimu kwa heshima kuu na kukupa pole kwa majukumu mazito uliyo nayo ndani ya taifa hili. Napenda kukupongeza kwa kuwa ninaamini wewe ni mmoja wa watu wachache ninaodiriki kusema mnamuelewa sana Mh Raisi. Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Raisi katika kumuapisha Naibu Waziri alilalamika sana kuhusu baadhi ya watendaji kutomuelewa juu ya nini hasa anakitaka, lile lilikuwa ni jambo zito sana na napenda kukupongeza kwa kuwa ninajua wewe ni mmoja ya watendaji wanaomuelewa sana Mh. Raisi.

Tatizo na ujenzi/makazi holela.
Napenda nirudi kwenye mada inayohusu dawa ya kumaliza makazi holela hasa kwenye majiji makubwa hapa Tanzania ( Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha) bila kusahau miji unayokua kama Kahama na mingineyo.

Mh Waziri Mkuu, nadhani unafahamu kuwa kati ya maeneo ambayo kama nchi na taifa tulifeli tangu mwanzo ni kwenye kudhibiti makazi holela. Mfano ni maeneo ya magomeni, tandale, mbagala, gongo la mboto, kimara, temeke, mtoni, tabata na mengineyo mengi.

Lakini vilevile kuna maeneo mapya ambayo kutokana na kuanza kuendelezwa kwa kiwango kikubwa hivi karibuni( Mfano Bunju, Madale, Chanika, Goba, Mbezi Makabe, Kibamba, Kinyerezi, Malamba Mawili n.k) serikali ilitakiwa kuja na mipango madhubuti ili kuhakikisha kuwa ingawa hayajapimwa basi yanajengwa vizuri kama kuhakikisha kuwa at least kwenye kila nyumba ya mtu kunakuwa na barabara inayofika kwake kwa kuwa barabara sio tu zinapendeshesha eneo ila zinaleta mpangilio zaidi na kurahisisha huduma kutolewa kipindi cha majanga kama moto na vilevile kipindi inapotokea mkazi wa eneo husika anaumwa.

Dhumuni la kukuandikia Mh. Waziri Mkuu humu sio kwa sababu simuamini Mh. Lukuvi ila naamini ukilisimamia wewe Mh Lukuvi atalisimamia vizuri na litaleta matokeo chanya. Ninapenda kwa jinsi unavomsaidia raisi wetu mpendwa kwa kuibua changamoto na kuzishughulikia. Nakuomba Mh umsaidie Mh raisi ili aweze kukumbukwa kwenye hili maana makazi holela ni moja ya vitu vinavyoharibu sana picha ya taifa letu.

Nini Kifanyike?
Najua kuna watu wanaweza kusema kuwa dawa la tatizo hili ni makazi kupiwa na kutolewa hati lakini changamoto ninayoiona hapa ni kuwa suala la upimaji limezidi kuwa changamoto kiasi ambacho watu wanazidi kujenga na upimaji umekuwa ukifanyik kwa kiwango cha chini sana. Hivyo Muheshimiwa napendekeza kama serikali mfanye mabadiriko yafuatayo na myatengenezee sera kabisa.

1. Mzipe mamlaka na mzielekeze serikali za mitaa kuhusu kupanga maeneo yao( Hasa kwenye maeneo mapya mabayo saivi yameanza kupata uendelezwaji wa kasi sana). Kwenye hili mzielekeze serikali za mitaa na watendaji wa kata kuhakikisha kwenye mitaa yao kuna barabara zilizopitishwa zinazohakikisha kila nyumba inapitiwa na barabara yenye uwezo wa kupitisha gari kubwa kama la fire. Hili likifanyika mtawezesha kupatikana kwa mitaa inayoeleweka hivo makazi yatawezekana kupangika kiurahisi n ahata upimaji utawezekana kiurahisi kama ukija kufanyika badae.

2. Mzielekeze mamlaka na serikali za mitaa na watendaji wake kuzisajili barabara zote zilizo kwenye mitaa yao na kuzuia ujenzi wowote kufanyika kuziba barabara izo. Mzipe mamlaka kumvunjia mtu yeyote atakayejenga kwenye baarabara izo zilizosajiliwa

3. Mzipe serikali za mitaa mamalaka ya kusimamisha ujenzi wowote ule unaoonekana unakiuka taratibu za makazi bora kama vile mtu kujenga kwenye mto, njia za maji, kwenye barabara n.k

Mh waziri Mkuu kama suala la upimaji makazi kabla ya watu kujenga litakuwa gumu napenda kukuhakikishia mkitumia njia hizi hatutakuwa na makazi holela kwa kuwa mkifanya hivi mitaa itapangika vizuri n ahata upimaji ukija badae utaweza kurasimisha maeneo ambayo yameshapangika vizuri.


Naomba Kuwasilisha.
 
Hoja tamu lkn tuko busy na vi wonder kwanza pamoja na kuwashughulikia wapinzani. Kikibaki chama chetu pekee titafanyia kazi hilo.
 
Back
Top Bottom