Waziri Mkuu Bungeni: Serikali haiongozi kibabe na wala haijakataza mikutano ya kisiasa

GRAMAA

JF-Expert Member
Nov 1, 2014
1,155
3,399
Leo bungeni kwenye kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu, mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe aliuliza maswali ya msingi sana kwa Waziri Mkuu. Maswali hayo yakiwepo.

(i) Ni lini Serikali ya CCM itaruhusu vyama vya upinzani vifanye mikutano yao ili vijiandae na uchaguzi mkuu wa mwaka huu?

(ii) Kwanini Serikali ya CCM imejipanga kuleta ubabe kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu?

(iii) Waziri Mkuu haoni umuhimu wa kuwepo na tume huru ya uchaguzi ili kuufanya uchaguzi mkuu wa mwaka huu kuwa huru na haki?

(iv) Je, ni sheria ipi Serikali ya CCM imetumia ili kuzuia mikutano ya kisiasa?

Majibu ya waziri mkuu yalikuwa ni tofauti kabisa na kile alichoulizwa.
Sasa sijui hakuelewa maswali?
Alifanya makusudi?
Au ndiyo mfumo unambana inabidi tu ajibu simple simple tu kwenye mambo ya msingi.

Hongera mh. Mbowe kwa maswali ya msingi japo kuwa yamekosa majibu ya msingi.


Freeman Mbowe (MB): Ni lini mtaruhusu vyama vya siasa vifanye wajibu wake wa uenezi ili kujiandaa na Uchaguzi Mkuu na Serikali ina mpango gani wa kuwezesha taifa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi ili uchaguzi huu uwe wa haki na halali.

Waziri Mkuu: Kwanza nataka nikanushe Serikali haiongozi kibabe, Mbowe ni kiongozi tunazungumza na kubadilishana mawazo na lengo ni kulifanya taifa liwe salama, Watanzania wanahitaji maendeleo na hakuna Mbunge au Diwani aliyezuiliwa kufanya mikutano kwenye maeneo yake.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa: Vyama vya siasa havijazuiliwa kufanya shughuli zake ila tumeweka taratibu muhimu kwa wale viongozi waliopata ridhaa kwenye maeneo yao, ratiba za uchaguzi zitatolewa na kueleza lini shughuli za kampeni zitaanza.

Waziri Mkuu: Tume ya Uchaguzi imeundwa kwa mujibu wa sheria na chombo hiki hakipaswi kuingiliwa na chombo chochote awe Rais wa Nchi au chama chochote, chombo hiki kipo huru.
 
Freeman Mbowe (MB): Ni lini mtaruhusu vyama vya siasa vifanye wajibu wake wa uenezi ili kujiandaa na Uchaguzi Mkuu na Serikali ina mpango gani wa kuwezesha taifa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi ili uchaguzi huu uwe wa haki na halali.

Waziri Mkuu: Kwanza nataka nikanushe Serikali haiongozi kibabe, Mbowe ni kiongozi tunazungumza na kubadilishana mawazo na lengo ni kulifanya taifa liwe salama, Watanzania wanahitaji maendeleo na hakuna Mbunge au Diwani aliyezuiliwa kufanya mikutano kwenye maeneo yake.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa: Vyama vya siasa havijazuiliwa kufanya shughuli zake ila tumeweka taratibu muhimu kwa wale viongozi waliopata ridhaa kwenye maeneo yao, ratiba za uchaguzi zitatolewa na kueleza lini shughuli za kampeni zitaanza.

Waziri Mkuu: Tume ya Uchaguzi imeundwa kwa mujibu wa sheria na chombo hiki hakipaswi kuingiliwa na chombo chochote awe Rais wa Nchi au chama chochote, chombo hiki kipo huru.
 
MAGALLAH R,
Huyu Mbowe katika hotuba zake kwa vyombo vya habari, alisha sifia zuio la mikutano na kujigamba kwamba wametumia mitandao ya jamii na imekuwa very effective kwao! Karibuni hivi amesema hana haja ya kukutana na wapiga kura wake huko Hai maana njia za kuelekezana na kusikiliza kero zao siyo lazima kiongozi awe na wapiga kura wake huko jimboni!

Sasa huyu Mbowe anauliza hilo swali sasa hivi? Mbona pia lilisha jibiwa mara nyingi? Huyu hatendei haki wanachama wake, imebaki miezi 6 tu ndipo anakumbuka kuuliza hayo maswali? Let's be serious man!
 
miss zomboko, Mbona wanasema uongo?Siasa ni wakati wa kampeni pekee?Uhuru wa Tume ya Uchaguzi ni kuhusu sheria iliyoiunda au matendo?

Viongozi wa awamu hii ni shida.Hizi sheria mpya za kufanya siasa katika maeneo walikochaguliwa madiwani/wabunge ilitungwa lini,IPO kifungu gani cha sheria zetu?

Je,maeneo ambako wapinzani hawana madiwani au wabunge watafikiwaje ili wawachague?Muda wa kampeni za Uchaguzi Mkuu unaweza kutumika kuimarisha vyama katika Kata/Majimbo husika?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu nilishamdharau tangu ile siku alipoulizwa 'ni lini serikali itaongeza mishahara kwa watumishi wa umma ambao hali zao ni ngumu'?

Akajibu 'Serikali itaongeza mshahara kimyakimya ili kuepusha wafanyabiashara kuongeza bei bidhaa'
Mimi ni mwenyeji wa Lindi ila huyu waziri mkuu kapwaya kuliko mawaziri wakuu wote waliomtangulia
 
Nadhani ili suala la mikutano ya kisiasa kuwekewa utaratibu wa kiongozi alitepata ridhaa eneo fulani afanye siasa au mikutano eneo lake SI SAWA.

nadhani tulitakiwa kabsa kutambua umuhimu wa mikutano hiyo kwa nchi changa kidemokrasia.

Binafsi naona ilo tamko la rais lililenga kubinya ukuaji wa demokrasia mimi nishauri kwa kuwa yeye anatenda vyema na anajiamini aruhusu watu tumseme yeye ni mwanasiasa kwa nini anawafunga midomo wenzake ilihali anatenda mema?

tafadhali sanaa Mh rais turuhusu hata sisi tusio na majimbo tukuseme,au tuuchambue utendaji wa serikali yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom