Waziri Mkuu azindua Kampeni ya Siku 16 za Uanaharakati Kupinga Ukatili wa Kijinsia. Aagiza Shule za Msingi mpaka Vyuo kuwa na madawati ya jinsia

Imeandikwa mwanaume atatafuta kwa uchungu na mwana mke atazaa kwa uchungu.
Tamko la Beijing! ''Haki sawa kwa wote liheshimiwe!!!'' Ok! waungwana!! Hayaa basi Me hatuna hiana tumekubali, km ni ivo wanawake nanyie muwe na haki ya kutuwowa basi!! muwajibike juu yetu!

Leo hii tena ke wasomi kabisaaa!! Mnaanza kutudhalilisha wanaume, ....mkishirikiana na wanaume zenu vimeo!! mnatupachika majina tena dhalili kabisaa! bila aibu mchana kweupeee!! pee humu JF!!

mkionewa huruma na kuwaondolea upweke sasa leo ndo mnakuja na haya! jmani nyie watu mnataka nini??? Ndo maana hata Mungu aliwashindwa! hivi! hivi!!

Mara Utasikia majina ya hovyo mara '' Ohooo! Mariooo! Mwanaume suruali, jamani sijui nini! Mama wee!! kikashuka!! kikapanda!! ivi mnataka nini nyie viumbe hai??? haya basi kwani huyo Marioo hakukupa hela zake kweli??

Basi sawa je!! Maji ya uhai aliyo kumiminia ukamwaga chooni?? kakupatia buree? basi mpe japo chakula kizuri aongezee hayo maji ili unenepe vizuri!! si anakurudishia bana? eti jamani? taatizo liko wapi?

tena masikini wa Mungu yeye me'' anatoa double, double !! huku na huku! unanenepa nyuma wajameni!! ujue hizi ndude kusema ukweli zina nenepesha sana zina hitaji mlo!! na maneno mazuri mazuri!! utafaidi!!

wanawake wote mliomo ushiriakianoni mnapendeza sana tena mnoo! ajili ya haya mafuta Mafuta adimu!! tunayo wa mwagia bureee! kusema kweli hizi zinawaondolea stress sana tena sana!! sie tunakonda tu siku hadi siku!! nyie mnafurahia,

Chunguza tu! maofisini kotee! hata kwako hapo!! ke anaye patiwa hii huduma pale anapo hitaji na yule asiyeipata huduma hii!! nani mpole, mnyenyekevu!! mwenye afya, furaha, mchangamfu anaesikiliza shida za watu?? hasa hasa Maafisa utumishi ?? jamani!! jamani!! heee!!

Mbaya zaidi wajameni, me ukiwa na makosa halafu Mkutane na Mwalimu asiye kuwa na Mume wala mshikaji haki ya naniliu!! Siku hiyo utayamba kifukuto!!

Mwalimu Malingumu popote ulipo yanakuhusu haya! ulinipa shida sana nyakati zile laiti ningejua ulipo kwa sasa ??! jamani huyu ke alinifukuza vibaya! kwenye kipindi chake miaka yote hiyo!! eti najidai Bitoz!! hakusahau!

kila akiniona tobaaa!! maajabu ya Musa sasa!!! somo lake nikaruka na Msonge hasaaa! tena kavu!! kavu!!, bila kumung'unya maneno!! mchana kweupe!!ee!! pee! kwa hasira akapotea sikumuona tena wala kunipongeza!! mpaka wa leo!! sijui sasa alienda kujinyongaa yule ticha???

Haya basi mtuhongeni Mali zenu, pesa zenu!! nyumba zenu, si ninakupa mbegu bana?? Me tumewapa kipaumbele mpate kazi!! mikopo! mzalishe!! matokeo yake ndo haya!! mara mnatunyang'anya tena, mnatupokonya viji mali vyenu! mnatulaza nje!

Mko tayari hata mchongo wa kazi ulio nifanyia nifukuzwe!! lkn sasa lazima nitafute Bonge la kazi abroad mpaka uonekane ya kwako kilikuwa cha mtoto! halafu narudi kukufadhiri ....hivi nikuulize utakataa huo ufadhili ? au.....

Tukidai haki km hivi!! ndo tunapigwa Majungu km haya!! tena basi na ke'' wasomi hao hao!! pasi na chembe ya aibu mnatudhalilisha weee!! ya sana!! sisi wanaume walio mfano wa Mungu! kweli! na Waziwaz hivi kweli??i!

Tusipo waoa! mnalia lia!! Oooh! wanaume wa siku hizi wamenichezea weee!!! haya njoo tuishi nikuoe basi!!!! Nitakulisha wee!! nitasomesha wee!ee!! najitahidi vimiradi ule! upendeze! nakopa huku na huko!! ili ule!! matokeo yake watoto wakifika chuo kikuu tu!!! una nidondosha gahfla! hasa Machame girls!!

Wanaume mlioko ktk mahusiano km haya mje huku niwape somo Muanana!! jinsi ya kuwafanya hawa viumbe!! sisi ni miungu bana kamwe hautaumia!! saana ndo utatoka!! kivingine! na totoz poa Maradufu!! njoooni bana dawa yao imepatikana usipokuja!! ukiumia shauri yako!!

ole wako KE ujiingize huku!! heee! utaona!!........ natoa nafasi kwa me wenzangu tu naona mnavo dhalilika ivi ivi sijapenda!! kabisa hii makitu!

Haya bana yangu ni hayo!! lkn me mjifunzege kupitia humu JF!! usipo sikia yatakukuta!! ndo maana nilisemaga humu kuwa '' usiamini chozi la Mwanamke! hata kidogo!! mbali na la Mama yako tu baasi!''
 
Anko Shamte baba wa nishike mkono tushindane hajafika kweli ofisini kwa Mh?
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salama, Amos Makalla amesema pamoja na kupokea kero za wanawake wanaokutana na unyanyasaji wa kijinsia wapo wanaume wanaohitaji msaada kutokana na changamoto za aina hiyo.

Akizungumza Alhamisi Novemba 25, 2021 wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, Makala amesema sasa hivi wanaume wamekuwa na malalamiko dhidi ya wanawake wenye fedha.

“Nilikuwa na ziara ya kusikiliza kero za wananchi, asilimia 30 ya kero 927 nilizopokea zinatokana na changamoto za ukatili na unyanyasaji wa kijinsia."

“Kwenye kero nilizozikuta wapo wanaume wanaonyanyaswa. Kuna wanawake wana fedha wanahitaji tu wanaume wa kuwaoa, hivyo anaweza kumpa kitu mwanaume na kumnyang’anya punde wakiachana,” amesema Makalla.

Mkuu huyo wa mkoa ameongeza, “Nimeyaona hayo wale wanaume marioo waliozoea kitonga wanakuja ofisini kulalamika kuwa walipewa mali na wanawake lakini wakanyang’anywa.

“Sasa swali linakuja hii sio ukatili? Naona kuna mjadala mpana katika hili suala la unyanyasaji wa kijinsia ndio mana mjadala mzuri wenye lengo la kuboresha sheria za ndoa,”.

Mwananchi
Ajikite kuleta maendeleo mambo ya mapenzi awaachie wenyewe, kwani alikuwepo wanapotongozana?
 
Kila mtu Kila kiongozi na hata mitandao ya jamii kazi kuwapa kipaumbele wanawake.haya ndo matokeo yake na bado mutaunda Hadi vyama vya kutetea wanaume tunapoelekea.
 
Nia sio kuwanyanyasa wanaume ila kuna sehemu nafasi ya mwanaume ni muhimu na ikipwaya ni hatari sana

Mwanaume ukishauza nafasi yako uliyopewa kiimani, kijamii na desturi lazima uone unanyanyasika

Sikatai mwanaume kutumia mali alizotafuta mke ila nakataa mwanaume kulegea na kuridhika kutafutiwa na mke.




Mwanzo 3: 16 - 19
Mungu akamwambia mwanamke,
Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.

Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.
 
Wenye hekima (wanaume) msaidieni RC wa Dar naona kapungukiwa hekima japo ni mwanaume.

Makalla asianze kufanya mambo kama Makonda kazi itamshinda!!! Wananchi wana kero za maana zaidi za kuzishuhurikia zaidi ya hao marioo; kwa mfano kuna barabara zimefungwa na wenye fedha kule JANGWANI BEACH ambazo husababisha mafuriko wakati wa masika na hilo limefanya viwanja vingi visiendelezwe!!! Hizi ndio kero Makalla anatakiwa azitatue kuwasaidia wananchi!!
 
Makalla asianze kufanya mambo kama Makonda kazi itamshinda!!! Wananchi wana kero za maana zaidi za kuzishuhurikia zaidi ya hao marioo; kwa mfano kuna barabara zimefungwa na wenye fedha kule JANGWANI BEACH ambazo husababisha mafuriko wakati wa masika na hilo limefanya viwanja vingi visiendelezwe!!! Hizi ndio kero Makalla anatakiwa azitatue kuwasaidia wananchi!!
Hizo kero anazijua sana ila kazikwepa kisha kakimbilia kwa hao kina marioo, kwa kweli Dar haina kiongozi kabisa
 
Back
Top Bottom