Waziri Mkuu ashangaa Tanzania kuwa na wachambuzi wengi wa mpira huku haina kocha hata mmoja anayefundisha nje

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,779
18,747
Waziri Mkuu akiongea katika kikao cha maafisa Utamaduni na maafisa michezo Jijini Dodoma, alishangaa kwa nini Tanzania haina kocha hata mmoja anayefundisha nje ya nchi, hata Burundi au Rwanda lakini yenyewe ikiwa inachukua makocha wa kigeni kutoka nchi hizo.

Kinachoshangaza zaidi ni Tanzania ndio nchi inayoongoza kuwa na wachambuzi wengi wa mpira ambao utawasikia wanavyowakosoa makocha wa nje, wanavyokosea kufundisha na kupanga timu zao na wanavyowakosoa wachezaji wa ndani na nje ya nchi wanavyofanya makosa ya kiufundi uwanjani na kuzigharimu timu zao.

Utamsikia mchambuzi wa Tanzania akimchambua kocha kama Mikel Arteta akielezea ni kwa jinsi gani alivyopanga kikosi vibaya hadi kupelekea timu yake kupoteza mchezo, au wachezaji wa Arsenal walivyokuwa wakifanya makosa yaliyopelekea timu yao kufungwa, au wakikosoa kocha wa Yanga au Simba.

Je, ni kwanini Tanzania tuna wachambuzi mahiri sana lakini hatuna makocha?
 
Nikwasababu kocha na uchambuzi ni vitu viwili tofauti we are blessed with wachambuzi ila tuongeze jitihada kwa kwenye kupika makocha..
 
Nikwasababu kocha na uchambuzi ni vitu viwili tofauti we are blessed with wachambuzi ila tuongeze jitihada kwa kwenye kupika makocha..
wachambuzi ni watu wajuvi wa ufundi wa mpira, na kocha anatakiwa kuwa na vigezo hivyo hivyo...
 
Uchambuzi wa soka unahitaji mdomo tu na king'amuzi cha kuangalizia mpira ili mdomo ufanye kazi yake. Yaani hata wewe unaweza kuwa mchambuzi.

ILa ukija kwenye huo ukocha, ni lazima upate mafunzo ya kutosha na ya kitaalam kuhusu mchezo husika. Umenielewa? Au bado umeshupaza shingo?
kwa hiyo wachambuzi ni watu wasiokuwa na utaalam wowote wa mpira ila wanajifanya kujua?
 
Nini mpira , hata boxing tunachambua na Mkuu naye labda huwa anazichambua. Sasa tusiulizane habari za kwenda kupanda ulingoni.
 
Waziri Mkuu akiongea katika kikao cha maafisa Utamaduni na maafisa michezo Jijini Dodoma, alishangaa kwa nini Tanzania haina kocha hata mmoja anayefundisha nje ya nchi, hata Burundi au Rwanda lakini yenyewe ikiwa inachukua makocha wa kigeni kutoka nchi hizo....
Ndio asilia yetu maneno mengi sana.kweli ukisikia wachambuzi utadhani uko uwanjani au wembley.

Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
 
Uchambuzi na ufundishaji ni One and the Same ?

Gary Lineker huenda akashindwa kuifundisha hata timu ya chekecheka ila katika uchambuzi yupo vizuri..., Martin Oneal huenda akiongea usimuelewe ila kwenye Coaching sio wa kubeza

Coaching is a different ball game....
 
Mchambuzi sio mkufunzi ...
Huku ni kujifariji tu. Unadhani ni kwa nini TV za nje wachambuzi karibu wote ni wachezaji au makocha wa zamani? Ukweli ni kwamba Tanzania ni nchi ya ''mdomo'' zaidi kuliko vitendo. Sijui hii tabia tumeitoa wapi.

Imeshakuwa utamaduni na kuiondoa ni ngumu kweli kweli na itachukuwa muda. Halafu kingine... sehemu yenye watu wengi wavivu inakuwa na bla bla bla nyingi sana.
 
Back
Top Bottom