Waziri Mkuu anapohubiri amani wakati Jimboni kwake Wagombea wa Upinzani wakifanyiwa vitendo vya kinyama

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,495
51,089
Leo nimemsikiliza waziri mkuu ndugu Majaliwa akiwa kwenye kongamano la viongozi wa dini la kuisifu serikali.

Waziri Mkuu ameutangazia umma wa Watanzania kuwa serikali italinda Amani wakati wote hata kipindi cha uchaguzi mkuu, na akataka siasa za kistaarabu.

Wakati akiyasema hayo, viongozi wa vyama vya ACT-Wazalendo kwa takribani wiki moja sasa wanalaani vikali vitendo vya kinyama, vya utekaji na kujeruhiwa kwa wagombea wao wa ngazi za ubunge na udiwani katika jimbo la Ruangwa ambalo ndilo jimbo la ubunge la waziri mkuu.

Katika press conference iliyofanyika jana, katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo ndugu Ado Shaibu amemtaka Waziri mkuu ambaye ndiye mwenye dhamana ya utendaji wa kila siku wa serikali atumie mamlaka yake kukomesha vitendo hivi vya kihuni, kinyama na kikatili visiendelee katika jimbo lake.

Sisi wananchi tungependa kufahamu; Je, Waziri Mkuu amechukua hatua gani zilizo ndani mamlaka yake ya kuwabaini waliohusika ili sheria ichukue mkondo wake na kukomesha vitendo hivi vya kinyama visitokee tena?

Wananchi tungependa kujua ili tuweze kuiamini kauli yake aliyoitoa leo mbele ya viongozi wa dini kuwa yeye binafsi ataendesha kampeni za kistaarabu, zisizo za uonevu kwa wengine, maana matendo ya utekaji wa wagombea wengine wasio wa chama cha mapinduzi katika jimbo hilo yanatuogopesha sana!
 
Nape katamka hadharani tena mbele ya waziri mkuu akiomba wamuachie awapige mabuti wapinzani, waziri mkuu alibariki hilo jambo.
Anapokua anahubiri amani ni kudhihirisha kua awamu hii ya hapa kazi tu ina Waziri mkuu mnafiki.

Halafu Waziri Mkuu hakukemea hiyo kauli ya Nape!

Huenda hata yanayoendelea huko Ruangwa ya kutekwa na kuumizwa watu kisa tu wanataka kutumia haki yao ya kuchaguliwa wala hajali!
 
Hivi haya mazee yameingiwa na ugonjwa gani eti hawataki kupingwa wao ni kina nani watu wanampinga mwenyezi Mungu ,ulisikia hata siku moja akawanyima hewa yake wasipumue.Na yangekuwa na uwezo wa kuzuia hewa wapinzani wangekufa kwa kukosa hewa.
 
Halafu waziri mkuu hakukemea hiyo kauli ya Nape!

Huenda hata yanayoendelea huko Ruangwa ya kutekwa na kuumizwa watu kisa tu wanataka kutumia haki yao ya kuchaguliwa wala hajali!

Wanawatumia hao viongozi wa dini ili kuficha uovu wao. Hao viongozi wa dini kama kweli wanaaminika hivyo mbona wamewatoa kwenye kusimamia uchaguzi? Hawataki viongozi wa dini kuona uovu waliopanga kuufanya kwenye uchaguzi.
 
Inaumiza Sana, unajua watu wanapolalamika kuwa tuwe na tume huru ndo katika mambo Kama haya. Unategemea Mheshimiwa atafanya Nini wakati nae nimshindani was nafasi ya ubunge jimboni mwake? Unategemea anaposema atasimamia amani kwamaana ipi? Yaani mvunjifu was amani niyule ambae atafanya siasa dhidi ya chama tawala maana yake amevunja amani!

Yaani mshindani wako alafu anakusimamia eti ufanye siasa za kistaarabu kweli unaona iko sawa? Jamani viongozi was dini hata hili hamkuliona ila utendaji Bora tu was mheshimiwa? Eti nanyie mnaomba vyama pinzani visiwe nakauli chonganishi ila vihubiri amani namshikamano. Miaka you're awamu hi hawakufanya kampeni ila mapinduzi waliendelea nakujinadi nakuvinanga vyaupinzabi wangesemea wapi kujitetea?

Leo Mheshimiwa mkuu anadai wanatengeneza matukio ili kupata huruma zakisiasa, jamani hatuoni aibu? Sisi niwatendaji wakuu waserikali Kama inaushahidi kuwa walitengeneza ili kupata huruma kwanini msiwaprosecute kuhadaa watanzania? Let us not fool people all the time. Enough is enough.
 
Aibu kubwa sana !
Tatizo si kukosekana amani. Tatizo ni kukosekana haki!!! Na kama uchaguzi ukiwa huru na haki, amani itatamalaki. Lakini tusijidanganye kuhubiri amani mchana na huku usiku tunapanga njama za kuwanyima wengine haki wanayostahili!!! Kumbukeni tukio la Hai!!!
 
Back
Top Bottom