Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi mweka hazina wa Halmashauri ya wilaya ya Kibondo, Thomas Chogolo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili za ubadhilifu wa makusanyo ya mapato ya halmashauri hiyo.
Mh. Majaliwa amewataka watendaji wa halmashauri huyo kumaliza haraka migogoro yao ya kiutendaji kabla ya Serikali haijawachukulia hatua kwani wanachokifanya ni kinyume na maelekezo yake.
Amechukua hatua hiyo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo.
“Katika Serikali hii suala la ukusanyaji wa mapato ni jambo nyeti na limepewa kipaumbele, hivyo ni lazima fedha inayokusanywa itumike kama ilivyokusudiwa ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi.”Amesema Waziri Mkuu Majaliwa.
Waziri Mkuu ameongeza kuwa wananchi wa halmashauri hiyo wanalipa kodi kupitia kwa watendaji wa kata katika maeneo yao lakini mweka hazina haingizi kwenye mfumo wa Serikali.
-ITV
Mh. Majaliwa amewataka watendaji wa halmashauri huyo kumaliza haraka migogoro yao ya kiutendaji kabla ya Serikali haijawachukulia hatua kwani wanachokifanya ni kinyume na maelekezo yake.
Amechukua hatua hiyo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo.
“Katika Serikali hii suala la ukusanyaji wa mapato ni jambo nyeti na limepewa kipaumbele, hivyo ni lazima fedha inayokusanywa itumike kama ilivyokusudiwa ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi.”Amesema Waziri Mkuu Majaliwa.
Waziri Mkuu ameongeza kuwa wananchi wa halmashauri hiyo wanalipa kodi kupitia kwa watendaji wa kata katika maeneo yao lakini mweka hazina haingizi kwenye mfumo wa Serikali.
-ITV