Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Katika taarifa ya habari ya jana usiku, Redio One walikuwa na habari kuwa waziri mkuu Mizengo Pinda aliungana na wananchi wa mkoa wa Rukwa kulalamika kwa Rais Kikwete juu ya ukosefu wa soko la nafaka na kuomba serikali iiongezee CGR uwezo ili iweze kununua mahindi mengi zaidi kuliko ilivyo sasa.
Nilishindwa kuelewa kwa sababu nijuavyo Waziri Mkuu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali na nilishikwa na butwaa kusikia hayo, mpaka sasa siamini kama kweli Pinda alifanya hivyo, lakini kama ni kweli basi hii ni sababu nyingine ya kutoichagua CCM kwa sababu imeshindwa kutekeleza wajibu wake. Imebaki kulalamika bila kutupatia ufumbuzi wa matatizo yetu. Na hii haikuwa mara ya kwanza kusikia watendaji wa serikali wakilalamikia juu ya mambo ambayo yako chini yao. Waziri Mkulo naye alishawahi kulalamika hadharani kuwa makampuni ya madini yanaidanganya serikali juu ya mahesabu yao na kwamba wanatoa takwimu za aina mbili, moja kwa ajiri ya serikali na nyingine kwa ajiri ya wanahisa wao. Je hapa kweli tutafika??
Nilishindwa kuelewa kwa sababu nijuavyo Waziri Mkuu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali na nilishikwa na butwaa kusikia hayo, mpaka sasa siamini kama kweli Pinda alifanya hivyo, lakini kama ni kweli basi hii ni sababu nyingine ya kutoichagua CCM kwa sababu imeshindwa kutekeleza wajibu wake. Imebaki kulalamika bila kutupatia ufumbuzi wa matatizo yetu. Na hii haikuwa mara ya kwanza kusikia watendaji wa serikali wakilalamikia juu ya mambo ambayo yako chini yao. Waziri Mkulo naye alishawahi kulalamika hadharani kuwa makampuni ya madini yanaidanganya serikali juu ya mahesabu yao na kwamba wanatoa takwimu za aina mbili, moja kwa ajiri ya serikali na nyingine kwa ajiri ya wanahisa wao. Je hapa kweli tutafika??