Waziri Mkuu aitaka Mikoa kutekeleza agizo kuhusu uwekezaji

mkiluvya

JF-Expert Member
May 23, 2019
802
725
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka mikoa ambayo bado haijatekeleza agizo lake la kuandaa makongamano ya uwekezaji ihakikishe inafanya hivyo mara moja.

Ametoa agizo hilo jana mchana (Jumamosi, Oktoba 19, 2019) wakati akifungua Kongamano la Uwekezaji kwa mkoa wa Pwani katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

“Nitumie fursa hii kuwapongeza viongozi wa mkoa wa Pwani kwa kutekeleza agizo nililolitoa Juni 18, 2018 wakati wa kongamano la tatu la uwezeshaji wananchi kiuchumi la kuhakikisha mikoa yote inaandaa kongamano la uwekezaji na inakuwa na mwongozo wa uwekezaji wa mkoa. Mikoa ambayo haijatekeleza agizo hilo, ifanye hivyo mara moja,” amesema.

Waziri Mkuu amesema mkoa huo umeweza kubaini fursa zilizopo katika mkoa wa Pwani na kuzitangaza kupitia mwongozo wa uwekezaji ambao pia ameuzindua leo.

Amesema kaulimbiu ya kongamano hilo isemayo: ‘‘Ijenge Tanzania, wekeza Pwani mahali sahihi kwa uwekezaji (Build Tanzania, Invest in Pwani, the Best Place for Investment)” ina maana kuwa, licha ya mkoa wa Pwani kubainisha na kutangaza fursa za uwekezaji na biashara zilizopo, unajipambanua vizuri na kuonyesha kuwa ni kwa namna gani umejiandaa na umetengeneza mazingira bora yanayovutia wawekezaji wa ndani na nje.

“Ili kudhihirisha dhamira ya dhati ya kukuza uchumi kupitia viwanda, nimeelezwa kuwa mkoa umetenga hekta 53,016 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda ambavyo vitatumia rasilmali zilizopo ndani ya mkoa na maeneo mengine ya nchi kwa lengo la kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wanachi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wahakikishe wanasimamia miundombinu inayoelekea kwenye viwanda vilivyopo kwenye maeneo yao.

"Kila mmoja ahakikishe maji, umeme na barabara vinafika kila eneo ambalo mwekezaji anataka kujenga kiwanda. Nitumie fursa hii kuwaomba mlete mabadiliko chanya yanayotokana na maboresho yanayofanywa na Serikali ya awamu ya tano."

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Bibi Angella Kairuki alisema kwamba Serikali imeanza kutekeleza mapendekezo ya mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini (Blueprint for Improving Business Environment Regulatory Licensing in Tanzania) kwa kuondoa tozo 163 zilizokuwa zikilalamikiwa na wawekezaji.

“Pia tumetenganisha majukumu ya TBS ya TFDA ambayo sasa ni TMDA. TBS itashughulika na vyakula na TMDA itashughulika na dawa na vifaatiba. Vilevile, tumeondoa ada za usajili sehemu za kazi ambazo zamani ilikuwa ni sh. 28,000 na sasa hivi zinatolewa bure,” alisema.
 
Hili siyo habari kwa sasa. Lete habari ya mjini. Meko amekata moto bado?
 
Hili siyo habari kwa sasa. Lete habari ya mjini. Meko amekata moto bado?
Haya uliyoyaandika siyo sahihi. Siyo maneno ya busara. Pamoja na mapungufu yake km binadamu na zaidi km kiongozi, huyo unayemuita Meko anahitaji kusamehewa na kuombewa. Kumwombea mabaya hakulipi/hakufidii hayo mabaya yanayosemekana alifanya. Lakini pia, ili kuonyesha kuwa wewe ni bora zaidi, unapaswa kufanya vizuri na mazuri zaidi yake. Kwa haya mnayofanya, mnadhihirisha kuwa waovu kuliko huyo Meko.
 
Haya uliyoyaandika siyo sahihi. Siyo maneno ya busara. Pamoja na mapungufu yake km binadamu na zaidi km kiongozi, huyo unayemuita Meko anahitaji kusamehewa na kuombewa. Kumwombea mabaya hakulipi/hakufidii hayo mabaya yanayosemekana alifanya. Lakini pia, ili kuonyesha kuwa wewe ni bora zaidi, unapaswa kufanya vizuri na mazuri zaidi yake. Kwa haya mnayofanya, mnadhihirisha kuwa waovu kuliko huyo Meko.
Mbona umebdilisha ID yako? Weka ya siku zote tuufichue upupu na uduvi uliyo uandika siku za nyuma "wale wengine" walipopatwa na masahibu ya kupangwa. Usijitie una busara Leo. Na kwanza kwa taarifa yako sihitaji nasaha wala ushauri toka kwako
 
Mbona umebdilisha ID yako? Weka ya siku zote tuufichue upupu na uduvi uliyo uandika siku za nyuma "wale wengine" walipopatwa na masahibu ya kupangwa. Usijitie una busara Leo. Na kwanza kwa taarifa yako sihitaji nasaha wala ushauri toka kwako

Sijabadilisha ID. Mimi ni mgeni humu na hii ni post yangu ya kwanza jamii forum. Kwa muda mrefu nimekuwa tu msomaji twenu.

Sijaandika kukupa nasaha, hapana. Km ulivyotumia haki yako kupost humu ndivyo nami nilivyofanya.

Sikudhani km ningekuhudhi na kwa hilo niwie radhi.
Pili, sishabikii maovu yoyote (bila kujali yametendwa nani). Kwa mabaya yote yaliyofanywa na "Meko" au na coherents wake tunapaswa kuyalaani km watu wastaarabu na waelewa kwa manufaa ya nchi yetu sasa na kwa vizazi vijavyo. Lakini kwa viwango hivyo hivyo, vya uelewa na ustaharabu, hatupaswi kushabikia mateso ya wale tunoaihisi walitufanyia vibaya.

Kwa kifupi, ukimuua mtoto wangu kwa sababu niliua wa kwako, tunakuwa tumelingana kwa yote na katika yote, including uovu wetu.

TUSHINDE UBAYA KWA WEMA. LABDA WATAJIFUNZA.
Mwisho, kupata satisfaction kupitia mateso ya mtu mwingine ni udhaifu.
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka mikoa ambayo bado haijatekeleza agizo lake la kuandaa makongamano ya uwekezaji ihakikishe inafanya hivyo mara moja.

Ametoa agizo hilo jana mchana (Jumamosi, Oktoba 19, 2019) wakati akifungua Kongamano la Uwekezaji kwa mkoa wa Pwani katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

“Nitumie fursa hii kuwapongeza viongozi wa mkoa wa Pwani kwa kutekeleza agizo nililolitoa Juni 18, 2018 wakati wa kongamano la tatu la uwezeshaji wananchi kiuchumi la kuhakikisha mikoa yote inaandaa kongamano la uwekezaji na inakuwa na mwongozo wa uwekezaji wa mkoa. Mikoa ambayo haijatekeleza agizo hilo, ifanye hivyo mara moja,” amesema.

Waziri Mkuu amesema mkoa huo umeweza kubaini fursa zilizopo katika mkoa wa Pwani na kuzitangaza kupitia mwongozo wa uwekezaji ambao pia ameuzindua leo.

Amesema kaulimbiu ya kongamano hilo isemayo: ‘‘Ijenge Tanzania, wekeza Pwani mahali sahihi kwa uwekezaji (Build Tanzania, Invest in Pwani, the Best Place for Investment)” ina maana kuwa, licha ya mkoa wa Pwani kubainisha na kutangaza fursa za uwekezaji na biashara zilizopo, unajipambanua vizuri na kuonyesha kuwa ni kwa namna gani umejiandaa na umetengeneza mazingira bora yanayovutia wawekezaji wa ndani na nje.

“Ili kudhihirisha dhamira ya dhati ya kukuza uchumi kupitia viwanda, nimeelezwa kuwa mkoa umetenga hekta 53,016 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda ambavyo vitatumia rasilmali zilizopo ndani ya mkoa na maeneo mengine ya nchi kwa lengo la kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wanachi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wahakikishe wanasimamia miundombinu inayoelekea kwenye viwanda vilivyopo kwenye maeneo yao.

"Kila mmoja ahakikishe maji, umeme na barabara vinafika kila eneo ambalo mwekezaji anataka kujenga kiwanda. Nitumie fursa hii kuwaomba mlete mabadiliko chanya yanayotokana na maboresho yanayofanywa na Serikali ya awamu ya tano."

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Bibi Angella Kairuki alisema kwamba Serikali imeanza kutekeleza mapendekezo ya mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini (Blueprint for Improving Business Environment Regulatory Licensing in Tanzania) kwa kuondoa tozo 163 zilizokuwa zikilalamikiwa na wawekezaji.

“Pia tumetenganisha majukumu ya TBS ya TFDA ambayo sasa ni TMDA. TBS itashughulika na vyakula na TMDA itashughulika na dawa na vifaatiba. Vilevile, tumeondoa ada za usajili sehemu za kazi ambazo zamani ilikuwa ni sh. 28,000 na sasa hivi zinatolewa bure,” alisema.
"wekeza pwani" ushauri mzuri kutoka msoga
 
Back
Top Bottom