chinchilla coat
JF-Expert Member
- May 16, 2016
- 5,107
- 10,961
Waziri mkuu Kassim Majaliwa amekutana na watumishi wa ofisi yake na kuongea nao kuhusu safari ya kuhamia Dodoma.
Amesema wamezoea kuishi Dar lakini sasa hivi wanaondoka na ni kweli wanaondoka, amesema kuhamia Dodoma ni moja ya ahadi zilizopo kwenye ilani ya CCM lakini ilianza mwaka 1973 na Dar itabaki kuwa mji wa biashara.
Ofisi ya waziri mkuu ndio inatakiwa ianze na wengine wafuate ambapo inatakiwa ihamie tarehe moja Septemba.
Amesema wengi wana maswali na wasiwasi kuhusu sehemu ya kwenda kukaa lakini amewatoa wasiwasi na kuwaambia kuwa Dodoma ina majengo mengi sana