Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,036
- 3,929
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema ana mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa.
Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.
Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.
Amesema baadhi ya kada ambazo zinafanyiwa kazi na maprofesa zinatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tofauti.
Waziri amesema wengi wanapata uprofesa wakiwa na miaka 55 na hufanya kazi kwa miaka michache na kutakiwa kustaafu.
"Tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu," amesema.
Amesema haitakuwa na maana kama wasomi hao wanatumia rasilimali za Taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu.
Mkuchika amesema pia atawasilisha maeneo mengine ambayo yana upungufu unaotokana na sheria.
Amesema hayo akijibu changamoto iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Xavier Daudi ambaye ameeleza kuwa sheria inatoa mwanya kwa taasisi nyingine za umma kuajiri bila kupitia sekretarieti hiyo.
CHANZO:Mwananchi
Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.
Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.
Amesema baadhi ya kada ambazo zinafanyiwa kazi na maprofesa zinatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tofauti.
Waziri amesema wengi wanapata uprofesa wakiwa na miaka 55 na hufanya kazi kwa miaka michache na kutakiwa kustaafu.
"Tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu," amesema.
Amesema haitakuwa na maana kama wasomi hao wanatumia rasilimali za Taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu.
Mkuchika amesema pia atawasilisha maeneo mengine ambayo yana upungufu unaotokana na sheria.
Amesema hayo akijibu changamoto iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Xavier Daudi ambaye ameeleza kuwa sheria inatoa mwanya kwa taasisi nyingine za umma kuajiri bila kupitia sekretarieti hiyo.
CHANZO:Mwananchi