Waziri Mkuchika: Nina mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema ana mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa.

Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.

Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.

Amesema baadhi ya kada ambazo zinafanyiwa kazi na maprofesa zinatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tofauti.

Waziri amesema wengi wanapata uprofesa wakiwa na miaka 55 na hufanya kazi kwa miaka michache na kutakiwa kustaafu.

"Tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu," amesema.

Amesema haitakuwa na maana kama wasomi hao wanatumia rasilimali za Taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu.

Mkuchika amesema pia atawasilisha maeneo mengine ambayo yana upungufu unaotokana na sheria.

Amesema hayo akijibu changamoto iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Xavier Daudi ambaye ameeleza kuwa sheria inatoa mwanya kwa taasisi nyingine za umma kuajiri bila kupitia sekretarieti hiyo.

CHANZO:Mwananchi
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema ana mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa.

Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.

Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.
Sawa lakini iwe kwa hiari, umri ubaki vilevile au muwape kwanza mafao yao ndiyo wafanye kazi kwa mikataba
 
No research,no right to speak.

Hiyo haitakuwa suluhu ya kudumu kama mwanasiasa mwenye elimu ya darasa la saba kisa tu ni mbunge au waziri analipwa mshahara mkubwa kuliko profesa.

Ndio maana watu wanapata udhamini wa kusomea hata udokta wanakataa kwasababu hawaoni future yoyote.

Watu wako radhi kusoma masters tofauti tofauti kuliko hata kuchuka PhD kwasababu wanaamini udokta haulipi bongo.

Mkuchika kaa na wasomi hawa wakupe changamoto zinazowakabili ndipo utajua tatizo liko wapi hasa.
 
Hili mie naliunga mkono na lisiishie kwa maprofesa tu bali wataalam mbali mbali ambao bado nchi ina upungufu mkubwa wa wataalam hao. Kwa mfano madaktari, wahasibu wa ngazi ya juu, wahandisi etc.
 
Mzee angalia zana hizi kiki zako hiyo angalia sanausije tokea dirishani. Cheza vizuri muziki Mh waziri.
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema ana mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa.

Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.

Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.

Amesema baadhi ya kada ambazo zinafanyiwa kazi na maprofesa zinatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tofauti.

Waziri amesema wengi wanapata uprofesa wakiwa na miaka 55 na hufanya kazi kwa miaka michache na kutakiwa kustaafu.

"Tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu," amesema.

Amesema haitakuwa na maana kama wasomi hao wanatumia rasilimali za Taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu.

Mkuchika amesema pia atawasilisha maeneo mengine ambayo yana upungufu unaotokana na sheria.

Amesema hayo akijibu changamoto iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Xavier Daudi ambaye ameeleza kuwa sheria inatoa mwanya kwa taasisi nyingine za umma kuajiri bila kupitia sekretarieti hiyo.

CHANZO:Mwananchi
Vile vile umesahau wanasiasa nao wawe na ukomo wa umri kugombea na kuteuliwa katika teuzi mbalimbali. Maana mnashadadia kada zingine na mnajisahau nyie wanasiasa ifikie mahali umri ukizidi muwe washauri tu sio kukimbizana katika kugombea nafasi na kujipendekeza ili mteuliwe wakati umri umeshawatupa mkono.
 
Umewasiliana na JPM?

Asijeakatengua kauli yako ukabaki kulialia.
Kuna mtu anataka kustaafu na watu wake.

Kama kwyeli wanajua kuna upungufu wa watu hao,mbona kila siku wasomi hawa wanateuliwa kufanya kazi sa kisiasa?

Kama kweli wako serious,tunatarajia watakuja na mkakati utakaohamasisha na kuvutia watu kujiendekeza kufikia ngazi ya uprofesa kama vile kutoa ufadhili wa serikali,n.k
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema ana mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa.

Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.

Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.

Amesema baadhi ya kada ambazo zinafanyiwa kazi na maprofesa zinatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tofauti.

Waziri amesema wengi wanapata uprofesa wakiwa na miaka 55 na hufanya kazi kwa miaka michache na kutakiwa kustaafu.

"Tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu," amesema.

Amesema haitakuwa na maana kama wasomi hao wanatumia rasilimali za Taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu.

Mkuchika amesema pia atawasilisha maeneo mengine ambayo yana upungufu unaotokana na sheria.

Amesema hayo akijibu changamoto iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Xavier Daudi ambaye ameeleza kuwa sheria inatoa mwanya kwa taasisi nyingine za umma kuajiri bila kupitia sekretarieti hiyo.

CHANZO:Mwananchi
kama ni Profesa LIPUMBA kwenye Cuf-Lipumba, Profesa Maji marefu kwenye power benki na Profesa J kuendelea kuimba itakuwa ni sawa
 
Kabisa Mkuu.

Naunga mkono hoja.

Mtu anasoma mpaka kupata uwezo wa kuwa profesa ana miaka hamsini, halafu afanye kazi miaka mitano astaafu, hilo halileti tija.

Pia ma Profesa waajiriwe kwa uwezo wao na uzuri wa mafunzo na machapisho yao, sio kwa sababu ya umri.
 
Ni wazo jema kwa kuwaongezea umri maprof.Aangalie pia kada zingine kama madaktari bingwa, Wahandisi washauri,nataaluma nyingine nyeti lakini wataalam wawe wamefikia ngazi za ubingwa au u consultant.Hawa watashauri na kulea taaluma ili ziweze kutoa mchango mkubwa kwenye ujenzi wa taifa.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema ana mpango wa kupeleka bungeni maombi ya kuongezwa muda wa kustaafu maprofesa.

Amesema umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa, hivyo ataomba wastaafu wakiwa na umri wa miaka 65 badala ya 55.

Mkuchika amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo.

Amesema baadhi ya kada ambazo zinafanyiwa kazi na maprofesa zinatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tofauti.

Waziri amesema wengi wanapata uprofesa wakiwa na miaka 55 na hufanya kazi kwa miaka michache na kutakiwa kustaafu.

"Tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu," amesema.

Amesema haitakuwa na maana kama wasomi hao wanatumia rasilimali za Taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu.

Mkuchika amesema pia atawasilisha maeneo mengine ambayo yana upungufu unaotokana na sheria.

Amesema hayo akijibu changamoto iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Xavier Daudi ambaye ameeleza kuwa sheria inatoa mwanya kwa taasisi nyingine za umma kuajiri bila kupitia sekretarieti hiyo.

CHANZO:Mwananchi
Ni kupitia kustaafu ndio nchi kama taasis inaweza kutengeza ajira kwa watu wake wengine, ningemshauri bwana mkuchiaka.ajikite kwenye kuhakikisha nchi inauwezo wa kutengeneza maprofesa wengi zaid na si kung'ang'ania waliopo ili hali wengine wanakuwa maprofesa kila siku.
Tuache uwoga
 
Back
Top Bottom