mr gentleman
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 3,223
- 4,673
Ni rasmi sasa watumishi wa serikali wamepewa ruhusa ya kwenda safari za nje ambazo zilisitishwa na hayati Magufuli.
========
Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mchengerwa amesema kuwa anawaagiza wakuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma kujipanga kwa ajili ya kutoa mafunzo ili kuongeza weledi kwa watumishi wa umma.
Amesema haiwezekani mtumishi afanye kazi kwa miaka mitano bila kupewa mafunzo yoyote ya kuongeza ujuzi kwa kile anachokifanya lazima atafanya kazi kwa mazoea pia wanataka watu wapewe weledi na ufahamu wa kufanya kazi kwa uweledi ili kazi ambayo walikuwa wanaifanya kwa masaa sita basi ifanyike kwa masaa 2 au saa 1 ila kiuweledi zaidi. Amesema wakuu wa Chuo cha Utumishi wa umma waandae semina, warsha kwa ajili ya kutoa mafunzo hayo kwa watumishi.
Wakurugenzi wote wa Halmashauri, Wakuu wa Taasisi wahakikishe wanatumia fursa ya chuo hiki katika kupata mafunzo kama kuwapeleka China au popote duniani basi fursa hizo anazifungua na hakuna sababu ya kufunga milango kwani kuna wafadhili wengine wanakuwa wapo tayari kuwasaidia bila gharama, lakini katika kutekeleza hilo kutumike uzalendo na uataifa.
========
Amesema haiwezekani mtumishi afanye kazi kwa miaka mitano bila kupewa mafunzo yoyote ya kuongeza ujuzi kwa kile anachokifanya lazima atafanya kazi kwa mazoea pia wanataka watu wapewe weledi na ufahamu wa kufanya kazi kwa uweledi ili kazi ambayo walikuwa wanaifanya kwa masaa sita basi ifanyike kwa masaa 2 au saa 1 ila kiuweledi zaidi. Amesema wakuu wa Chuo cha Utumishi wa umma waandae semina, warsha kwa ajili ya kutoa mafunzo hayo kwa watumishi.
Wakurugenzi wote wa Halmashauri, Wakuu wa Taasisi wahakikishe wanatumia fursa ya chuo hiki katika kupata mafunzo kama kuwapeleka China au popote duniani basi fursa hizo anazifungua na hakuna sababu ya kufunga milango kwani kuna wafadhili wengine wanakuwa wapo tayari kuwasaidia bila gharama, lakini katika kutekeleza hilo kutumike uzalendo na uataifa.