Waziri Mchengerwa akemea utendaji usioridhisha wa Watumishi wa Afya

OR TAMISEMI

Ministry
Jul 3, 2024
20
92
images - 2024-07-14T115519.019.jpeg

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amekemea utendaji usioridhisha wa watumishi wa afya katika maeneo ya kutolea huduma nchini kwa kuwa unaenda kinyume na maadili ya utumishi.

Maelekezo ya Mhe. Mchengerwa yametolewa kwa niaba na Mkurugenzi wa Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais-TAMISEMI Dkt. Rashid Mfaume alipotembelea kituo cha Afya Mji Mwema Manispaa ya Songea ambacho hivi karibuni taarifa zilisambaa mtandaoni zikionesha wahudumu wa Afya kutowajibika kumsaidia mama mjamzito.
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amekemea utendaji usioridhisha wa watumishi wa afya katika maeneo ya kutolea huduma nchini kwa kuwa unaenda kinyume na maadili ya utumishi...
Watumishi wasipowajibika basi dawa yake ni kuwatembelea na kuwakemea?
 
Yaani mnawakemea tu? Mawaziri wajifunze kuwajibika pia, waziri wa maji kila alipopita amekuta madudu tu cha ajabu hakuna aliyefukuzwa wala waziri kuwajibika
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amekemea utendaji usioridhisha wa watumishi wa afya katika maeneo ya kutolea huduma nchini kwa kuwa unaenda kinyume na maadili ya utumish...
tuanze na nyie mnawajibika mnatoa huduma kama inavyotakiwa. Mkumbuke mfanyakazi wa serikali wananchi ndio maboss zake ila nyie mmegeuka kua maboss wa wananchi.
 
Back
Top Bottom