Jana trh 02/08/2012 SSRA walitoa tangazo kupitia gazeti la Daily news na website yao wakiuarifu umma kwamba fao la kujitoa limesitishwa kufuatia sheria iliyosainiwa na Rais mwezi June 2012. Kwa uelewa wangu nina mawazo kwamba tangazo hilo ni batili kwani mpaka sasa kwa utafiti niliyoufanya hakuna mwongozo/kanuni wa matumizi ya sheria hiyo(Regulation) kuhusu matumizi ya hiyo sheria mpya hakuna GN (Government Notice) iliyotangaza matumizi ya hiyo regulation.
Kisheria, hakuna sheria yoyote itakayoweza kufanya kazi kama hakuna mwongozo wa sheria hiyo. Mf mpaka sasa sheria inayokataza uvutaji sigara hadharani haina nguvu wala hakuna mtu hata mmoja aliyeshitakiwa kwa kosa hilo kwa sababu hakuna mwongozo wa matumizi ya sheria hiyo. kukosekana kwa mwongozo wa sheria hiyo mpya ya kusitisha fao la kujitoa imethibitishwa pia na Naibu waziri wa nishati na madini Mh. Steven Masele jana Bungeni. Namnukuu
''Katika hatua nyingine, maselealiwataka wafanyakazi wa migodi waliogoma kupinga sheria ya Mifuko ya Hifadhi za jamii kurejea kazini akifafanua kuwa, kanuni zinazoendesha sheria hizo hazijatungwa'' (source mwananchi trh 03/08/2012 at pg 2)
SSRA wapetata wapi nguvu ya kuanza kutumia sheria angali kanuni zinazoendesha sheria hiyo hazijatungwa? SSRA walitakiwa wasubiri mpaka hapo kanuni zitakapotungwa ndipo waanze kutoa matamko. matamko yao kwa umma ni batili kama sio premature. Walichofanya SSRA sio sahihi kabisa na ni upotoshaji. Hii mifuko ya hifadhi ya jamii inaweza kuendelea na utaratibu wa awali kwani bila kujali tangazo la SSRA kwani tangazo lenyewe halina nguvu ya kisheria na halijafuata utaratibu. Labda swali la kujiuliza ni je waziri husika amechukua hatua gani kuhusu hili tangazo?
Naomba kuwakilisha
.
Kisheria, hakuna sheria yoyote itakayoweza kufanya kazi kama hakuna mwongozo wa sheria hiyo. Mf mpaka sasa sheria inayokataza uvutaji sigara hadharani haina nguvu wala hakuna mtu hata mmoja aliyeshitakiwa kwa kosa hilo kwa sababu hakuna mwongozo wa matumizi ya sheria hiyo. kukosekana kwa mwongozo wa sheria hiyo mpya ya kusitisha fao la kujitoa imethibitishwa pia na Naibu waziri wa nishati na madini Mh. Steven Masele jana Bungeni. Namnukuu
''Katika hatua nyingine, maselealiwataka wafanyakazi wa migodi waliogoma kupinga sheria ya Mifuko ya Hifadhi za jamii kurejea kazini akifafanua kuwa, kanuni zinazoendesha sheria hizo hazijatungwa'' (source mwananchi trh 03/08/2012 at pg 2)
SSRA wapetata wapi nguvu ya kuanza kutumia sheria angali kanuni zinazoendesha sheria hiyo hazijatungwa? SSRA walitakiwa wasubiri mpaka hapo kanuni zitakapotungwa ndipo waanze kutoa matamko. matamko yao kwa umma ni batili kama sio premature. Walichofanya SSRA sio sahihi kabisa na ni upotoshaji. Hii mifuko ya hifadhi ya jamii inaweza kuendelea na utaratibu wa awali kwani bila kujali tangazo la SSRA kwani tangazo lenyewe halina nguvu ya kisheria na halijafuata utaratibu. Labda swali la kujiuliza ni je waziri husika amechukua hatua gani kuhusu hili tangazo?
Naomba kuwakilisha
.