Waziri Masauni: Matukio ya mauaji nchini yananinyima usingizi

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,546
1644566248026.png

Picha: Mhandisi Hamad Masauni
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni, amesema tangu ateuliwe kuongoza Wizara hiyo yapo mambo mawili yanayomnyima usingizi ikiwemo mauaji yanayotekelezwa na baadhi ya watu kwenye jamii pamoja na baadhi ya askari kufanya vitendo kinyume na maadili.

Waziri Masauni amesema hayo baada ya kushuhudia onesho la medani za kivita lililoandaliwa na askari wanaotarajia kuhitimu kozi ya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi katika kambi ya kivita ya Kambapori iliyopo wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro.

"Tokea nimeingia, kuna vitu viwili vikubwa sana vinanikosesha usingizi, si mimi tu nina hakika, kwanza Amiri Jeshi Mkuu na watanzania wote walio wema, la kwanza kuna matukio ya mauaji mengi toka nimekabidhiwa hii nafasi nasikia leo mtu amechinjwa ukiuliza sababu unaambiwa ni wivu wa mapenzi mwingine sijui alikuwa amedhurumiwa, la pili kumekuwepo na askari wachache ambao wanatia doa jeshi la polisi," amesema Waziri Masauni

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema kuwa, Jeshi la Polisi nchini limejipanga kukabiliana na matishio mbalimbali ikiwemo ya kutumia silaha za moto na kwamba hakuna mhalifu atakayefanikiwa kutekeleza tukio la kihalifu.

Aidha, IGP Sirro amesema kuwa, kamwe Jeshi la Polisi alitomvumilia askari yeyote atakayekwenda kinyume na kanuni na taratibu za Jeshi hilo.

Chanzo: EATV

Pia soma > Dkt. Mpango: Rais Samia anakerwa na mauaji yanayotokea nchini. Ameagiza Jeshi la Polisi kufanya msako kubaini wanaojiuhusisha na vitendo vya mauaji

- Waziri Masauni: Serikali haiwezi kukaa kimya wakati wananchi wanauawa. Aunda kamati kuchunguza matukio ya mauaji nchini
 
Kuna masheikh zaidi ya 150 wako mahabusu gereza la kisongo kwa zaidi ya miaka 8 kwa mashatka ambayo yamekosa ushaidi eti upelelezi haujakamilika

Nadhani hao ndiyo wanakosa usingizi wakiwa kwenye kuta za gereza pasipo haki kwa zaidi ya miaka 8.
 
"Kuna vitu viwili vikubwa sana vinanikosesha usingizi,la kwanza kuna matukio ya mauaji mengi toka nimekabidhiwa hii nafasi nasikia leo mtu amechinjwa ukiuliza sababu unaambiwa ni wivu wa mapenzi.

“Pili kumekuwepo na askari wachache ambao wanatia doa jeshi la polisi," - Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuff Masauni.
 
Kama mnaendelea kumkumbatia Siro huta pata usingizi hadi utumbukiwe.

Nyie viongozi mnaongea mema Siro ana ongea tofauti.

Kwamba huwa humumuoni au mna muogopa
 
Hapo kuna matukio ambayo polisi wanaweza kuyazuia
Na kuna nyingine jamii inaweza kuzuia

Ova
 
Na WMNN, Kilimanjaro

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, kumletea majina ya askari Polisi wanaojihusisha na matukio yasiyo ya maadili ili aweze kuwashughulikia.

Amesema lengo la kuwashughulikia askari hao wasiowaadilifu ambao ni wachache ndani ya Jeshi hilo kutasaidia kuwa na Jeshi imara, safi na kulifanya liwe hilo na jamii.

Akizungumza wakati akifunga Mafunzo ya Wakaguzi Wasaidizi wa Polisi katika Kambi ya Polisi ya Kilelepori, Wilayani Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, leo, Masauni alisema yeye ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ambayo inashughulikia nidhamu ya Askari, hivyo atawashughulikia skari hao ambao hawana nidhamu.

“Katika kipindi hiki mimi ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi kama kuna askari ambaye atakuwa anafanya vitu vya hovyo, IGP mlete tu tumalizane naye, hatuwezi kucheka na vitu ambavyo havina maslahi na tija katika nchi hii, tutaendelea kusimamia kwelikweli nidhamu, ni kwa dhamira njema kwa wengi ninyi mliowasafi,” alisema Masauni.

Masauni aliongeza kuwa nidhamu ya Askari ni muhimu katika Jeshi la Polisi kwasababu wanategemewa katika jamii na pia wananchi wana imani kubwa na askari, hivyo inasikitisha sana kuona askari anaenda kuua raia, askari anatoa siri jambo hilo amesema halikubaliki ndani ya Jeshi hilo.

“Inasikitisha leo kunakuwa na askari anaenda kuua raia, hata kama ni mmoja, inasikitisha kuna askari leo anapora, askari anabambikia kesi mtu, aibu na dhambi kubwa, askari anatoa siri kwa wahalifu, lazima tufuate maadili, hili halikubaliki na tutawashughulikia wanaofanya matukio hayo, lazima tusimamie nidhamu ya Jeshi,” alisema Masauni.

Aidha, Masauni alizungumzia matukio ya madawa ya kulevya na udhalilishaji hasa upande wa Zanzibar, amewataka Askari waliohitimu mafunzo hayo watakaopangiwa katika kata mbalimbali nchini, kwa watakaopangiwa Zanzibar wahakikishe wanapambana na matukio hayo.

Kwa upande mwingine Masauni amesema matukio ya mauaji yanayoendelea nchini pamoja na baadhi ya Polisi wanaojihusisha na matukio ya uhalifu yanamfanya hakose usingizi hivyo amewataka askari kuwa waadilifu.

Ameongeza kuwa tangu ateuliwe kuiongoza Wizara hiyo ambapo sasa amefikisha mwezi mmoja lakini masuala ya mauaji pamoja na baadhi ya polisi hao kushiriki katika masuala ya uhalifu yanamkosesha usingizi na pia hata Rais Samia Suluhu Hassan naye anakosa suingizi kutokana na matukio hayo.

“Mimi tangu nimeingia ndani ya Wizara hii kwa kipindi hiki cha muda mfupi kama mwezi mmoja hivi, kuna vitu wiwili vikubwa vinanikosesha sana usingizi, na si mimi tu nina uhakika Amiri Jeshi Mkuu Rais Samia Suluhu Hassan, naye anakosaa usingizi, na pia na Watanzania wote waliowema, wazalendo, wanaoipenda nchi yao, watakua wanakosa usingizi. Matukio hayo la kwanza ni mauaji, mara utasikia kachinjwa mtu, ukiuliza sababu unaambiwa sababu ya mapenzi, mara kaenda kwa mganga kadhulumiwa, pamoja na sababu nyingi tu,” alisema Masauni.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro amesema zipo changamoto kama uhalifu unaovuka mipaka, ugaidi na na makosa ya dawa za kulevya kwakushirikiana na vyombo vingine ya ulinzi na usalama vimeendelea kudhibitiwa licha ya kwamba bado zipo changamoto nyingine ikiwemo mmomonyoko wa maadili kwenye jamii.

“Mheshimiwa Waziri tunaendelea kupambana na uhalifu unaovuka mipaka, ugaidi na na makosa ya dawa za kulevya kwakushirikiana na vyombo vingine ya ulinzi na usalama, pia bado zipo changamoto nyingine ikiwemo mmomonyoko wa maadili kwenye jamii,” alisema IGP Sirro.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Polisi Moshi mkoani Kilimanjaro SACP, Ramadhani Mungi amesema jumla ya wanafunzi 1955 wamehitimu mafunzo ya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi na kwamba wahitimu hao wamejifunza mbinu mbalimbali za kukabiliana na makosa ya uhalifu na wahalifu.
 
Back
Top Bottom