fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,380
- 7,905
Hivi ni wapi makamba kasema anataka kubinafsisha tanesco?na hata kama ana huo mpango kwani ana mamlaka gani ya kufanya huo uamuzi peke yake?Waziri wa Nishati January Makamba ajulishwe kuwa kwenye taifa siyo kila kitu ni cha kubinafisishwa kwa masilahi mapana ya taifa.
Baba wa taifa Mwl Nyerere kwenye hotuba yake moja mwaka 1995 alikemea vikali akili ya kuchukua mali ya uma na kuwakabidhi watu wachache, mfano umeme ndiyo injini ya uchumi wa nchi kwa kuvutia kujengwa kwa viwanda vingi na kuzalisha bidhaa za bei ndogo zitakazoshindana kwenye soko, kamwe hatuwezi kuwapa watu wachache watufanyie biashara kwa kutuuzia umeme alafu tukategemea bidhaa zetu zishindane kwenye soko la Dunia.
- Umeme
- Bandari
- Reli
- Viwanja vya ndege
- Mbuga etc
Enzi za Kikwete Tanesco nusura ibinafisishwe baada ya kuwa na madeni makubwa ya kulipia capacity charges kutoka kwenye generator za kampuni la symbion.
Alipoingia Magufuli akafuta baadhi ya mikataba ya hovyo na kuliwezesha shirika kukusanya zaidi ya trillion 2 kwa mwaka hivyo likaacha kujiendesha kwa kutegemea ruzuku ya serikali na kufuta mpango wa kulibinafisisha shirika hili la uma.
Ameingia rais Samia na alipomteua waziri January Makamba tayari ameingia na mentality ileile ya enzi za Kikwete.
1. Pamoja na kwamba Tanesco ya leo hawaagizi nguzo nje ya nchi kama walivyokuwaga wanafanya huko nyuma lakini bado Makamba anataka shirika libinafisishwe.
2. Pamoja na kwamba Tanesco ya leo wanakusanya zaidi ya trillion mbili kwa mwaka lakini bado waziri Makamba anataka shirika libinafisishwe!
3. Pamoja na kwamba kupitia REA Tanesco imetapakaa nchi nzima lakini bado waziri anataka shirika libinafisishwe.
4. Pamoja na kwamba sasa hivi Tanzania inajenga bwawa kubwa kabisa la kufua umeme lakini bado waziri anataka Tanesco ibinafisishwe.
Hii speed ya 4G ya Makamba kutaka Tanesco ibinafisishwe inasukumwa na nini? Hivi kwa akili hii vipi huyu Makamba angeshinda urais mwaka 2015?
Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app