Waziri Maige amsimamisha kazi Mkurugenzi wa Wanyamapori kupisha Uchunguzi!

Kwa hakika kabisa Maige angekuwa muungwana angeachia ngazi. Hii kashfa ni kubwa mno kuuhimili. Hakuna maelezo ya maana hapa wakati watu tuna uchungu na twiga wetu.

sasa mbona baraza lote litaisha!!! maana
Ngereja anaambiwa aachie ngazi kwa sakata la umeme na Jairo.
Nundu aachie ngazi kwa kukubali bajeti ndogo pamoja na sakata la Uda...
Tibaijuka naye sakata la kumilikisha ardhi ovyo ovyo kwa wawekezaji... na kushindwa kutatua migogoro ya ardhi
sasa Maige naye kaja na kutorosha wanyama....

baraza lote kwisheni!
 
sasa mbona baraza lote litaisha!!! maana
Ngereja anaambiwa aachie ngazi kwa sakata la umeme na Jairo.
Nundu aachie ngazi kwa kukubali bajeti ndogo pamoja na sakata la Uda...
Tibaijuka naye sakata la kumilikisha ardhi ovyo ovyo kwa wawekezaji... na kushindwa kutatua migogoro ya ardhi
sasa Maige naye kaja na kutorosha wanyama....

baraza lote kwisheni!

Mkuu wacha waishe tu. Kuisha kwa Mawaziri si kuisha kwa Watanzania. Kama watu wanatuongopea si ni bora wakae pembeni waje wengine huenda wakaweza.
 
katika majumuisho yake waziri maihe amemsimamisha kazi mkurugenzi wa wanyamapori kupisha uchunguzi wa sakata la wanyama kusafirishwa hai!!

Ni sawa ila wasiwasi wangu hii isije ikawa ni njia tu ya kulainisha wabunge wapitishe bajeti ya wizara, pili maamuzi haya yanayochukuliwa ghafla baada tu ya wabunge kusema yaangaliwe. Ni ajabu waziri na raisi wake wanamteua mtu kipumbavu halafu wakikemewa wanamsimamisha! Lazima na wao wachukuliwe hatua kwa maamuzi ya kijinga!!

Safari inaendelea!

ndugu zanguni huyu ni msanii zaidi ya kikwete wetu..na habari tu anawekeza hela agombanie urais 2015..anyway haki ya mtanzania ila kifupi akuna mzigo utakaopitishwa bila waziri kujua hili ni changa la macho na ndio maana wanasema mawaziri wengi wakati wa bajeti wanaendaga kwa waganga kuwapofusha wale wabunge na watanzania wawaone wako safi..kama amuamini nendeni arusha huyubana leo kajipulizia a/c kama kawaida ..kuwa na mawaziri wasio na adabu na uchungu na maliza watu kama hawa unawamwagia maji ya mavi tu wakiwa wanatoka hii ndio soln tumewachoka

aanze kujisimamisha mwenyewekwanza hana adabu kama alie mchagua
 
inasikitisha sana kuona kuwa wanyama wakubwa kama twiga na tembo wanasafirishwa bila watendaji wakuu wa wizara kuwa na taarifa. ni kichekesho na haiingii akilini. tusipokuwa makini maliasili zetu zotepi zitaishia kutajirisha nchi za nje.

pia kuna jambo lingine la ziada- naomba wizara husika ichunguze kambi moja inaitwa 'ndege beach' ambayo iko kigamboni. shughuli zao hazieleweki na wamejificha katikati ya msitu kandokando ya bahari. kuingia mule ndani ni mpaka ruhusa maalum na pale getini wamekaa kiwasiwasi sana. sijui wanaficha nini. tafadhali chunguzeni.


 
..hata mimi niliuliza waziri Membe yuko wapi kuhakikisha wanyama hao wanarudishwa Tanzania?

..kama alikuwa na usongo wa kurudisha pesa za BAE basi lazima awe na usongo hawa wanyama warudishwe.

..ninavyoelewa mimi mizigo ya watu wenye hadhi ya Diplomat huwa haipekuliwi.

..pamoja na hayo kuna exception kwamba ikiwa kuna uhakika wa tendo la uhalifu kuwa limefanyika basi mzigo huo lazima upekuliwe.

..wa-Nigeria walijaribu kumteka nyara waziri wa zamani wa mafuta akiitwa Ummaru Diko na kumtia kwenye sanduku lenye hadhi ya mzigo wa kidiplomasia. Scotland Yard walisisitiza mzigo huo ufunguliwe na wakaweza kumuokoa Diko asifike mikononi mwa Gen.Muhammad Buhari.

..katika tukio la uwanja wa ndege wa Kilimanjaro mzigo ulikuwa ni wanyama walio hai wanaonekana kwa macho sasa sielewi kwanini hawakuzuiliwa.
na hili ndio lilo chini ya membe sio la bae system lilokuwa likisheria zaidi, hapa diplomatic buggage imetumika, sasa kama kweli anaipenda tz na kupinga rushwa na ufisadi tutamsikia
 
Huu ni ujanja tu kama wa TANESCO. Kwa maana hiyo Maige anataka kutuambia kwamba alikuwa hajui kuhusu wanyama wetu kunyakuliwa na kwa maana hiyo amejua jana na kuamua kumsimamisha Mkurugenzi ili aanze uchunguzi? Hata kama ndege zilikuwa na vibali vya kidiplomasia na wanyama wetu toka huko mbugani walikuwa na vibali vya kidiplomasia? Huyu Mkurugenzi anatumiwa tu kama Bangusilo!! Ni ajabu na kweli kwamba Maige alikuwa hajui!! Mkurugenzi atatakaswa tu baada ya budget kupita au huenda amesema tu bungeni na hajamwandikia barua.
Hongera kwa hiyo picha ya Master Sgt Thomas Sankara, mkuu. Unanikumbusha mbali.Back to the issue, jambo hili la Maige kumsimamisha Mkurugenzi ni maigizo tu kwani kiutawala Maige ni Waziri, a mere politician, Hana mamlaka ya kumteua au kubatilisha uteuzi achilia mbali kumsimamisha MKURUGENZI YEYOTE KATIKA WIZARA NZIMA. HE IS NOT THE APPOINTING AUTHORITY. Tunayo mifano mingi tuuuu hapa hapa Danganyika ya waliowahi kujidai eti wanayo mamlaka ya kusimamisha watendaji lakini Amri zao Ziliishia
kuwa nguzo za mipapai! Mkumbukeni Lowassa na issue ya maghorofa feki/fake chang'ombe, Diallo Anthony Ng'wandu akiwa hapo hapo Maliasili ya Yule jamaa sijui yuko wapi siku hizi. Wenye mamlaka hula ni Katibu Mkuu Luhanjo kwa mjibui wa ofisi yake na jakayaa mrishoo kikwete kwa mjibu wa ofisi yake
 
August said:
na hili ndio lilo chini ya membe sio la bae system lilokuwa likisheria zaidi, hapa diplomatic buggage imetumika, sasa kama kweli anaipenda tz na kupinga rushwa na ufisadi tutamsikia

August,

..Tanzania ni nchi ya ajabu kwelikweli.

..waziri Maige aache visingizio na ubabaishaji.

..diplomatic buggage gani inaweza kubeba twiga??

..kwa mtizamo wangu Membe anapaswa kuingilia[take the lead] kwasababu tu wanyama hao wametoroshwa kwenda nchi ya kigeni.
 
magamba ni magamba tu......alikuwa wapi siku zote hadi asubiri mashinikizo kutoka bungeni??????????????????
 
Kwani Maige ndo anajua leo hilo sakata la kusafirishwa Wanyama! Kwanini hakuwasimamisha hao watu kabla ya leo! Hii inaonyesha kama si wabunge kutishia kuikwamisha Bajeti ya Wizara yake, asingesimamishwa mtu.

Lakini bado tusisherehekee ushindi, kwani hata Ngereja aliwazuga hivi hivi Wabunge kwa kutuletea umeme kwa muda wa wiki mbili, lakini bajeti yake ilipopita tu, sasa Mgao ndo mara mbili ya ule wa mwanzo. (Waulize Mwanza).

Maana mkishangaa sana msije mkaanguka presha siku mtakaposikia Jairo mtu huru hana tatizo lolote.

Hii ndiyo serikali ya Magamba

mkurugenz wa wanyapori ndg Erasmus Tarimu alishasimamishwa tangu mwez wa nne
 
Iko sehemu gani ya Kigamboni? Nataka kuifanyia kazi
inasikitisha sana kuona kuwa wanyama wakubwa kama twiga na tembo wanasafirishwa bila watendaji wakuu wa wizara kuwa na taarifa. ni kichekesho na haiingii akilini. tusipokuwa makini maliasili zetu zotepi zitaishia kutajirisha nchi za nje.

pia kuna jambo lingine la ziada- naomba wizara husika ichunguze kambi moja inaitwa 'ndege beach' ambayo iko kigamboni. shughuli zao hazieleweki na wamejificha katikati ya msitu kandokando ya bahari. kuingia mule ndani ni mpaka ruhusa maalum na pale getini wamekaa kiwasiwasi sana. sijui wanaficha nini. tafadhali chunguzeni.


 
Huyo mkurugenzi ni kondoo wa kafara tu wapo Vigogo wanaohusika. Wamemsimasha Mkurugenzi ili kuficha ukweli wa jambo zima! Hivi kitengo chetu cha Usalama wa Taifa Kimefia wapi? mbona kipindi cha miaka ya themanini kilikua maarufu sana Duniani pote? Nijuavyo mimi Airport zote watu wa usalama huwa wapo,kwanini na wao wasiwajibishwe?
Nchi yetu imekwisha! Hao ni wanyama ambao wanaonekana kwa macho,je visivyoonekana inakuaje?
 
Naomba niwaulize kweli mnataka kujua au mnataka kuridhika? Niliwahi kuuliza huko nyuma tunajua zaidi ili kiwe nini? Lakini zaidi pi ani kuwa hawa walichaguliwa kutawala na hakuna jambo lolote linalofanywa leo ambalo hawajawahi kulifanya nyuma na watu walikuwa wanajua haya yote sasa wanakasirika nini?
 
Anaongea point sana kama itafanyika kama anavoongea, nimempenda japo ni magamba naona ni bora zaidi ya Pinda, kwa mnaoangalia TBC Kasema ndege ya jeshi liyochukua wanyama ilikuwa na kibali cha diplomatic haikustahili kufanya uhalifu na anajirizisha na ushahidi kabla hajaituhumu nchii nyingine kufanya uhalifu

Hakuna point yoyote uliyoongea hapa,
Hata kama atachukua hatua bado haitasaidia, inafaa awajibishwe.
Hii skendo haikuanza leo, alikua wapi muda wote huo?
Na hizo ndege zinazoingia na kuchukua mizigo na kutoweka kimyakimya, tunajua zilileta nini?
Ulichukulia ni ndege za kijeshi
 
Naomba jjamii forumu iruhusu mtu kufunguka maana bila mtu kufunguka kisawasawa ujumbme haufiki! Nina hasira maana kila kiyu kimenipiga chini sababu ya umeme
 
hiyo ni janja tu bajeti ipite , matokeo ya uchunguzi ndiyo yatakayomaliza igizo kwani hakutakuwa na ushahidi wa moja kwa moja hivyo atarudishwa kazini
 
Back
Top Bottom