Daimler
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 556
- 973
Ubalozi wa Ujerumani nchini, umebandika ukutani, Ramani ya Tanzania inayoonyesha Ziwa Nyasa likiwa ndani ya Mipaka ya Malawi badala ya Mpaka wa Tanzania na Malawi kuwa katikati ya Ziwa.
Ujerumani ndiyo Mtawala wa kwanza wa Tanzania, kipindi hicho ikiitwa German East Africa (DOAG), kupitia Mkataba wa 1886 (Anglo-German Agreement) ulioweka Mipaka ya ukanda wa Pwani na Kenya, kabla ya Mkataba wa 1890 (Helgoland Treaty) kumalizia kuweka mipaka ya Uganda, DRC, Zambia (Rhodesia), Malawi (Nyasaland) na Msumbiji (Mozambique). Heligoland Treaty ndiyo ililiweka Ziwa Nyasa kwa Wamalawi.
Hata hivyo, baada ya Waingereza kuiweka Tanganyika Territory chini ya Mandate, alijikuta akitawala Malawi na Tanganyika na hapo ndipo walipobadili Mpaka na kuuweka katikati ya Ziwa Nyasa.
Anyway, siko hapa kurefusha mada hii, muhimu ni lazima marafiki wa Tanzania, i.e. wote wenye Ubalozi hapa Tanzania, wahakikishe Ramani zinazoonekana kwenye Ofisi zao ni zile zinazotolewa ama kukubaliwa na Tanzania na si mwingine yeyote.
So, Waziri wa Mambo ya Nje, Augustine Mahiga shughulikia haraka suala hilo.
https://cdn.auckland.ac.nz/assets/humanrights/Research/MalawiTanzania-NZCHRLPP-final.pdf
Ramani ya Tanzania.