Waziri Magufuli amwagiwa sifa

Ng'wamapalala

JF-Expert Member
Jun 9, 2011
6,808
6,500
Mawaziri wa wizara mbalimbali serikalini, wametakiwa kuiga mfano wa Waziri wa Ujenzi,Dk John Magufuli wa kugawa rasilimali za nchi kwa watu wote.

Ushauri huo ulitolewa juzi na Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe wakati akichangia hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka 2013/14.

Filikunjombe ambaye siku zote amekuwa na kigugumizi cha kukubali bajeti kwa urahisi,juzi alikubali kuunga mkono moja kwa moja Makadirio ya Wizara ya Ujenzi akisema kuwa mgawanyo wake umelenga maslahi ya nchi na maslahi ya watu wachache kama ilivyo kwa wizara zingine.

“Kutokana na hili, mimi na wananchi wangu wa Ludewa tunakuombea sana ndugu Magufuli na tunasema kuwa ikiwa utakuwa na uhitaji wa nafasi nyingine ya juu zaidi ya hii uliyonayo, usisite kutuambia nasi tutakuunga mkono kwani tuko pamoja na wewe,”alisema Filikunjombe.

Mbunge huyo aliwataka mawaziri wajaribu kuiga mfano wa Magufuli ambaye anapeleka miradi kwa nchi nzima na hafanyi kazi ya kurundika miradi katika jimbo lake pekee.

Hata hivyo alimtaka Magufuli kufanya haraka katika kukamilisha miradi ya ujenzi wa barabara katika Wilaya ya Ludewa ambayo haijawahi kupata lami tangu Uhuru hivyo ikijengwa lami wananchi wa huko nao utakuwa mwaka wao wa kwanza kusherehekea uhuru licha ya kuwa Watanzania wengine watakuwa wanasherehekea zaidi ya miaka 53 ya Uhuru.

Kwa hisani ya Mwananchi.
 
Kwanza nianze kwa kusema, naukubali sana utendaji wa Waziri Magufuli lakini pamoja na kuukubali, bado nina RESERVATION pale ninapoangalia picha ya serikali kwa mapama.

Nina wasi wasi na kiwango cha utendaji wa serikali yetu iwapo kama utendaji wa Waziri Magufuli unakuwa ndiyo kipimo cha kiwango cha juu kinachopata pongezi kutoka pande zote za wabunge wetu bungeni.

Katika serikali isiyokuwa na neno BUSINESS AS USUAL, utendaji wa Waziri Magufuli ungeonekana niwa kawaida kabisa across the entire government.

I'm afraid, We have set our government perfomance standard as a country at second-rate mpaka AVERAGE tunaiona kwa sasa kama ni EXCELENT.

Hili tatizo haliishii kwa serikali peke yake. Hata vyama vyetu vya siasa navyo ni wale wale. Tunahangaika na siasa za UDAKU na PERSONALISED POLITICS kana kwamba jamii imeishavuka kiwango cha mahitaji ya lazima kwa mwanadamu. Political standard in Tanzania is leaving much to be desired.

Tunatakiwa tujitambue na kuona kilichopo kwa sasa katika vyama na serikali hakikubaliki tukilinganisha na mbio za maendeleo katika nchi zingine duniani.
 
Mawaziri wa wizara mbalimbali serikalini, wametakiwa kuiga mfano wa Waziri wa Ujenzi,Dk John Magufuli wa kugawa rasilimali za nchi kwa watu wote.

Ushauri huo ulitolewa juzi na Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe wakati akichangia hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka 2013/14.

Filikunjombe ambaye siku zote amekuwa na kigugumizi cha kukubali bajeti kwa urahisi,juzi alikubali kuunga mkono moja kwa moja Makadirio ya Wizara ya Ujenzi akisema kuwa mgawanyo wake umelenga maslahi ya nchi na maslahi ya watu wachache kama ilivyo kwa wizara zingine.

"Kutokana na hili, mimi na wananchi wangu wa Ludewa tunakuombea sana ndugu Magufuli na tunasema kuwa ikiwa utakuwa na uhitaji wa nafasi nyingine ya juu zaidi ya hii uliyonayo, usisite kutuambia nasi tutakuunga mkono kwani tuko pamoja na wewe,"alisema Filikunjombe.

Mbunge huyo aliwataka mawaziri wajaribu kuiga mfano wa Magufuli ambaye anapeleka miradi kwa nchi nzima na hafanyi kazi ya kurundika miradi katika jimbo lake pekee.

Hata hivyo alimtaka Magufuli kufanya haraka katika kukamilisha miradi ya ujenzi wa barabara katika Wilaya ya Ludewa ambayo haijawahi kupata lami tangu Uhuru hivyo ikijengwa lami wananchi wa huko nao utakuwa mwaka wao wa kwanza kusherehekea uhuru licha ya kuwa Watanzania wengine watakuwa wanasherehekea zaidi ya miaka 53 ya Uhuru.

Kwa hisani ya Mwananchi.

Kusema Ukweli BAGAMOYO kuna

--- BOTI ya KISASA inajengwa
--- Reli ya EXPRESS
--- Two Way Line
--- Kiwanja cha NDEGE cha Kimataifa
--- Sattellite CITY - UHURU CITY

Achana na Mabomba ya GAS hayo sio vya kwake huyo MAGUFULI

Kwahiyo ndio anagawa UCHUMI wa NCHI kiuhalali???
 
Mawaziri wa wizara mbalimbali serikalini, wametakiwa kuiga mfano wa Waziri wa Ujenzi,Dk John Magufuli wa kugawa rasilimali za nchi kwa watu wote.

Ushauri huo ulitolewa juzi na Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe wakati akichangia hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka 2013/14.

Filikunjombe ambaye siku zote amekuwa na kigugumizi cha kukubali bajeti kwa urahisi,juzi alikubali kuunga mkono moja kwa moja Makadirio ya Wizara ya Ujenzi akisema kuwa mgawanyo wake umelenga maslahi ya nchi na maslahi ya watu wachache kama ilivyo kwa wizara zingine.

Kutokana na hili, mimi na wananchi wangu wa Ludewa tunakuombea sana ndugu Magufuli na tunasema kuwa ikiwa utakuwa na uhitaji wa nafasi nyingine ya juu zaidi ya hii uliyonayo, usisite kutuambia nasi tutakuunga mkono kwani tuko pamoja na wewe,alisema Filikunjombe.

Mbunge huyo aliwataka mawaziri wajaribu kuiga mfano wa Magufuli ambaye anapeleka miradi kwa nchi nzima na hafanyi kazi ya kurundika miradi katika jimbo lake pekee.

Hata hivyo alimtaka Magufuli kufanya haraka katika kukamilisha miradi ya ujenzi wa barabara katika Wilaya ya Ludewa ambayo haijawahi kupata lami tangu Uhuru hivyo ikijengwa lami wananchi wa huko nao utakuwa mwaka wao wa kwanza kusherehekea uhuru licha ya kuwa Watanzania wengine watakuwa wanasherehekea zaidi ya miaka 53 ya Uhuru.

Kwa hisani ya Mwananchi.
Huyu jamaa ni mtendaji asiye na longolongo
 
Back
Top Bottom