Waziri Maghembe azomewa na wananchi Gallapo-Babati

Antar bin Shaddad

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
202
101
Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe amezomewa na wananchi wa mji mdogo wa Gallapo wilayani Babati wakati wa mkutano wa hadhara baada ya waziri huyo kuktaa kuulizwa maswali na wananchi kuhusu kero ya maji na mgogoro wa muda baina yao na mamlaka ya maji ya mji huo GAWASA.Baada ya maghemmbe kuktaa kuulizwa maswali na wananchi walianza kumzomea pamoja na maafisa wa serikali alioandamana nao na mkutano ulivunjika ambapo waziri huyo aliondoka huku polisi wakiwazuia watu wasimdhuru pamoja na msafara wake.

Kwa muda mrefu mji wa Gallapo umekumbwa na uhaba wa maji kwa kile kinachoelezwa kuwa mamlaka hiyo imeshindwa kuwajibika na kutegemea chanzo kimoja cha ambacho kilianzshwa na wananchi hao miaka karibu ishirini iliyopita huku idadi ya watu ikiwa tayari imeongezeka kwa asilimia 100 katika kipindi hicho.
 
Duh! pole yake. Itabidi hizi ziara za mikoani waziache, naona hata wananchi vijijini wameshawashtukia!
 
Nape na Kinana wake waende huko! Maprofesa wengine kwa kujidhalilisha.
 
Hivi kumbe huyu prof bado ni Waziri!. Nina kipindi kirefu sijamsikia akiongea wala kufanya chochote muhimu kama waziri Mwakyembe au Magufuli. Nadhani anastahili kuamshwa kidogo.
 
Huyu maghembe anaogopa maswali kiasi hicho??
TZ ya sasa sio ya mazezeta, hichi chama cha majangili kinahitaji kujipanga mno.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkwele anayatuma tu yaende kwa wananchi kufanya mikutano, nayo kama mazezeta yanakwenda tu bila kufikiri.
Wananchi safi sana, zomea zomea mpaka wakimbie.
 
yaani kwa kifupi elimu kubwa ikiingia kwenye siasa inazidiwa hata na elimu ya darasa la form 4 angalieni maprofessor wetu kama Mwandosya, Msola, etc wanafanya nini bungeni nje ya kuzomea hoja za mashiko za upinzani?
 
Hawa wakimbia midahalo hawawezi kukubali kuulizwa maswali. Huwa kuna uongo wao wameupanga kuwaambia wananchi wakiulizwa maswali hawataweza kuutetea uongo huo, yanaamua yakimbie.
 
professor magembe, eeh, ati professor! Kama yule wa akina masanja. Mmesema ana u'professor' wa maji au?
 
eti wakajibu mapigo... teh teh teh! sasa badala ya kujibu mapigo wanapokelewa kwa mapigo,watakoma!
 
Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe amezomewa na wananchi wa mji mdogo wa Gallapo wilayani Babati wakati wa mkutano wa hadhara baada ya waziri huyo kuktaa kuulizwa maswali na wananchi kuhusu kero ya maji na mgogoro wa muda baina yao na mamlaka ya maji ya mji huo GAWASA.Baada ya maghemmbe kuktaa kuulizwa maswali na wananchi walianza kumzomea pamoja na maafisa wa serikali alioandamana nao na mkutano ulivunjika ambapo waziri huyo aliondoka huku polisi wakiwazuia watu wasimdhuru pamoja na msafara wake.

Kwa muda mrefu mji wa Gallapo umekumbwa na uhaba wa maji kwa kile kinachoelezwa kuwa mamlaka hiyo imeshindwa kuwajibika na kutegemea chanzo kimoja cha ambacho kilianzshwa na wananchi hao miaka karibu ishirini iliyopita huku idadi ya watu ikiwa tayari imeongezeka kwa asilimia 100 katika kipindi hicho.

Hii ndio sura halisi ya viongozi wa ccm. Uoga, kiburi, dharau na ufupi wa kifikra.
Rest in hell ccm!
 
Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe amezomewa na wananchi wa mji mdogo wa Gallapo wilayani Babati wakati wa mkutano wa hadhara baada ya waziri huyo kuktaa kuulizwa maswali na wananchi kuhusu kero ya maji na mgogoro wa muda baina yao na mamlaka ya maji ya mji huo GAWASA.Baada ya maghemmbe kuktaa kuulizwa maswali na wananchi walianza kumzomea pamoja na maafisa wa serikali alioandamana nao na mkutano ulivunjika ambapo waziri huyo aliondoka huku polisi wakiwazuia watu wasimdhuru pamoja na msafara wake.

Kwa muda mrefu mji wa Gallapo umekumbwa na uhaba wa maji kwa kile kinachoelezwa kuwa mamlaka hiyo imeshindwa kuwajibika na kutegemea chanzo kimoja cha ambacho kilianzshwa na wananchi hao miaka karibu ishirini iliyopita huku idadi ya watu ikiwa tayari imeongezeka kwa asilimia 100 katika kipindi hicho.

sasa nin maana ya yeye kuwa waziri na asingepewa uwaziri angmlaumu mwenyekiti wake?huyo rais wake anasikiliza kero za wananchi wake y maghembe?
Ila sishangai maghembe utotoni mwake hata baba yake hakuwa akimsikiliza alikua mtoro sana wa shule,anatoroka kwao haendi shule hadi bakora,huenda suala la kupuuzia bado linaendelea
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom