MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Waziri Magembe azomewa UDSM,jasho zamtoka!
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof. J4 Magembe jana alijikuta akitokwa jasho mpaka za miguu kwa aibu baada ya kozomewa na Madenti wenye hasira wa Chuo Kikuu cha Dsm (UDSM),tena mbele ya Rais wa Uganda Mh.Yoweri Museveni.
Magembe, ambaye alihudhuria hafla ya kuzinduliwa kwa Chuo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii (UDCASS), alikumbwa na
zahma hilo mara tu alipotambulishwa na MC wa shughuli hiyo, Prof Amandina Liambama.
J4 ambaye aliambatana na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, alionekana kushitushwa na jambo hilo na kuanza kunong'onezana mara kwa mara na Membe.
Tofauti na alivyozomewa Magembe, wanafunzi hao ambao walikuwa wamejazana kwenye ukumbi wa mikutano wa Nkrumah, Membe na baadhi ya maprofesa walishangiliwa kwa sauti ya juu na hasa alipotambulishwa makamu mkuu wa chuo hicho, Prof Rwekaza Mkandara.
Hata hivyo, Magembe ambaye alikuwa anatakiwa amkaribishe mgeni rasmi kwa mujibu wa ratiba, alizomewa tena wakati
Mkandara alipoeleza kuwa atamkaribisha mgeni rasmi huku Magembe akiwa ameketi kiti kimoja tu toka alipokuwa
Museveni.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof. J4 Magembe jana alijikuta akitokwa jasho mpaka za miguu kwa aibu baada ya kozomewa na Madenti wenye hasira wa Chuo Kikuu cha Dsm (UDSM),tena mbele ya Rais wa Uganda Mh.Yoweri Museveni.
Magembe, ambaye alihudhuria hafla ya kuzinduliwa kwa Chuo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii (UDCASS), alikumbwa na
zahma hilo mara tu alipotambulishwa na MC wa shughuli hiyo, Prof Amandina Liambama.
J4 ambaye aliambatana na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, alionekana kushitushwa na jambo hilo na kuanza kunong'onezana mara kwa mara na Membe.
Tofauti na alivyozomewa Magembe, wanafunzi hao ambao walikuwa wamejazana kwenye ukumbi wa mikutano wa Nkrumah, Membe na baadhi ya maprofesa walishangiliwa kwa sauti ya juu na hasa alipotambulishwa makamu mkuu wa chuo hicho, Prof Rwekaza Mkandara.
Hata hivyo, Magembe ambaye alikuwa anatakiwa amkaribishe mgeni rasmi kwa mujibu wa ratiba, alizomewa tena wakati
Mkandara alipoeleza kuwa atamkaribisha mgeni rasmi huku Magembe akiwa ameketi kiti kimoja tu toka alipokuwa
Museveni.