Waziri Lwenge: Kupata makazi Dodoma ni changamoto kwa watumishi waliohamia kutoka Dar

jerrytz

JF-Expert Member
Oct 10, 2012
5,960
4,209
Siku moja baada ya Serikali kuwataka watumishi waliohamia Dodoma kutokea Dar kuuona mji huo kuwa ni kituo chao cha kazi, Waziri wa Maji na Umwagiliaji ndugu Gerson Lwenge amesema kuwa hakuna makazi ya kutosha na wafanyakazi wengi wanaishi kwenye nyumba za wageni (Guest House).

Siku ya alhamisi Katibu mkuu Kiongozi ndugu John Kijazi alisema kuwa njozi ya Serikali kuhamia Dodoma inaelekea kutimia baada ya idara nyingi kutoka Wizara 18 kuhamia na kuanza kazi Dodoma.

Lakini akiongea mkoani hapa jana Waziri Lwenge amesema kuwa kupata nyumba(makazi) mkoani hapa ni changamoto kwa watumishi waliohamia.
Wizara anayoongoza imeshahamisha wafanyakazi waandamizi 102 katika hatua za kwanza za kuhamia Dodoma.

Alisema kwamba wizara yake ina jumla ya wafanyakazi 422 ambao wanatarajiwa kuhamia Dodoma. Kwa sasa wizara hiyo imepanga ofisi kwenye jengo la Benki wakati Serikali ikijipanga kujenga jengo kwa ajili ya wizara hiyo.

Awali Katibu mkuu alinukuliwa akisema kuwa "tutakutana na changamoto nyingi mwanzoni ila tuwe tayari kuzikabili."

The Guardian 3rd March 2017
 
Misuse of funds and resources.Hakuna majengo unahamisha majengo unaishia kupanga
 
Wakurupukaji wanahamia alafu hawajui wanaenda kutua wapi
 
Unamaanisha The Guardian au Waziri Lwenge?

Labda ungeitazama hii kama taarifa na sio ukosoaji.



Endeleeni kukosoa nyinyi huwa hamna jema, ila kumbuka changamoto zipo katika kila hatua ya maendeleo
 
Bajeti za wizara kwa ajili ya maendeleo ziko hoi alafu wanajilazimisha kuifurahisha ikulu kwa kuenda kupanga kwenye majengo kwa gharama za serikali huku watumishi wakilazimishwa kutumia mishahara yao kupata malazi kwa gharama kubwa.
 
Changamoto ni kawaida

Ukitaka kuzaa kuna changamoto ya uchungu.

Hata ukifanya mapenzi kuna changamoto ya kuishiwa nguvu wakati wa kufika kileleni.

Acha serikali iende dodoma
 
Wakati watumishi wa serikali wanaishi kwa taabu na wasiwasi viongozi wa serikali wanaishi kama malaika! Wakati watumishi wa serikali wanaishi kama watumwa viongozi wanaishi kama wafalme!

Watumishi wa serikali wanaishi kwa masimango kama vile nchi hii si yao, wavamizi, wakimbizi! Viongozi wanataka kazi zifanyike bila kujali watumishi wamelala wapi na wamekula nini! Hatma za familia za watumishi wa serikali hazina dira wala hazijui kesho yao!!

Wengi wa watumishi wa serikali wanajuta kuzaliwa na kuishi Tanzania!!
 
Changamoto ni kila mahali hata nyumbani zipo, hata hapa Dar baadhi ya Wizara zilipanga sio kwamba zilikua na majengo yake so mnaolalama onyesheni mcngi wa malalamiko yenu
 
Ina maana kauli aliyotoa waziri kuwa kuna tatizo la makazi ni ya uongo?
Sio uongo, hizo ndio changamoto ambazo baada ya kuhamia zitapatiwa majibu, kumbuka hili zoezi limesitishwa kwa zaidi ya miaka 40. Ulishawahi kuhamia kwenye nyumba yako ambayo umeijenga mwenyewe ? Marekebisho mengi hufanyika baada ya kuhamia ndani ya nyumba na si kabla ya kuhamia
 
Tatizo la elimu ya yetu ya nadhalia

"Kila jambo kama lilivyoandikwa kwenye kitabu alichonifundosha Professor naniliu"

Kazi kweli kweli
 
Endeleeni kukosoa nyinyi huwa hamna jema, ila kumbuka changamoto zipo katika kila hatua ya maendeleo
Maendeleo gani hayo? Yaani nchi ipo katika wakati mgumu kiuchumi, maamuzi ya Dodoma yanafuata. Hivi angehamisha wizara chache chache, nini kingepungua?
 
Sio uongo, hizo ndio changamoto ambazo baada ya kuhamia zitapatiwa majibu, kumbuka hili zoezi limesitishwa kwa zaidi ya miaka 40. Ulishawahi kuhamia kwenye nyumba yako ambayo umeijenga mwenyewe ? Marekebisho mengi hufanyika baada ya kuhamia ndani ya nyumba na si kabla ya kuhamia
Hii si nyumba. Wale si kwamba walishindwa kuhamia Dodoma bali walibaini kuna vipaumbele zaidi ya Dodoma.
 
Back
Top Bottom