Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,438
- 3,333
Wizara wa Mambo ya Ndani ya nchi imekemea kushamiri kwa matukio ya watu kujichukulia sheria mkononi ikiwemo kupiga, kujeruhi na kuuawa.
Waziri Lugola amesema hayo jana Jumapili Septemba 2, 2018 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.
Ametaja matukio ya walimu kuwaadhibu, kujeruhi na kusababisha vifo vya wanafunzi wao pamoja na mgambo wa Jiji la Dar es Salaam kuwajeruhi wananchi wanaposimamia suala la usafi kuwa miongoni mwa matukio yasiyokubalika mbele ya macho ya sheria.
"Suala la mgambo waliowekwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kuwapiga na kuwajeruhi wananchi limewaondolea sifa ya kuendelea kuwatumikia wananchi, ni vema halmashauri ikatafuta njia mbadala ya kushughulikia suala hilo la usafi na kudhibiti matukio hayo," amesema Waziri Lugola
Ameagiza halmashauri nchini kuanzisha kitengo cha huduma ya askari polisi chini ya sheria sura ya 322 ili kupunguza matukio ya mgambo ambao baadhi hawajui namna ya kusimamia utekelezaji wa sheria kutumika na hatimaye kukiuka sheria.
Akizungumzia adhabu kwa wanafunzi, Waziri Lugola amewataka walimu kutoa adhabu kwa mjibu wa sheria kwa lengo la kuwarekebisha wanafunzi na si kuwakomoa.
Ameuhakikishia umma kuwa Serikali kupitia mamlaka husika itachukua hatua dhidi ya wote waliohusika katika matukio yote ya kujichukulia sheria mkononi.
"Mahakama pekee ndicho chombo cha kutoa adhabu kwa mujibu wa Katiba na sheria. Tutawashtaki wote waliohusika bila kujali vyeo, majina wala umaarufu wao kwa sababu hakuna aliye juu ya sheria," amesema Lugola.
Chanzo; Mwananchi
Waziri Lugola amesema hayo jana Jumapili Septemba 2, 2018 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.
Ametaja matukio ya walimu kuwaadhibu, kujeruhi na kusababisha vifo vya wanafunzi wao pamoja na mgambo wa Jiji la Dar es Salaam kuwajeruhi wananchi wanaposimamia suala la usafi kuwa miongoni mwa matukio yasiyokubalika mbele ya macho ya sheria.
"Suala la mgambo waliowekwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kuwapiga na kuwajeruhi wananchi limewaondolea sifa ya kuendelea kuwatumikia wananchi, ni vema halmashauri ikatafuta njia mbadala ya kushughulikia suala hilo la usafi na kudhibiti matukio hayo," amesema Waziri Lugola
Ameagiza halmashauri nchini kuanzisha kitengo cha huduma ya askari polisi chini ya sheria sura ya 322 ili kupunguza matukio ya mgambo ambao baadhi hawajui namna ya kusimamia utekelezaji wa sheria kutumika na hatimaye kukiuka sheria.
Akizungumzia adhabu kwa wanafunzi, Waziri Lugola amewataka walimu kutoa adhabu kwa mjibu wa sheria kwa lengo la kuwarekebisha wanafunzi na si kuwakomoa.
Ameuhakikishia umma kuwa Serikali kupitia mamlaka husika itachukua hatua dhidi ya wote waliohusika katika matukio yote ya kujichukulia sheria mkononi.
"Mahakama pekee ndicho chombo cha kutoa adhabu kwa mujibu wa Katiba na sheria. Tutawashtaki wote waliohusika bila kujali vyeo, majina wala umaarufu wao kwa sababu hakuna aliye juu ya sheria," amesema Lugola.
Chanzo; Mwananchi