Waziri Lawrence Masha hana uwezo

mzawa5000

Member
May 30, 2006
7
3
Ndugu wana-forum hivi viongozi wetu watajua kuwajibika kwa wananchi lini?

Au ndiyo yale yale ya kudanganyana majukwaani? Walalahoi na wenye uchungu na ile nchi nafikiri mtaniunga mkono kwa hili.

Kinachojionyesha sasa ni kwamba tuna kopi za akina Sumaye, Kigoda kwenye hili baraza la mawaziri la JK. Tofauti ni kuwa hatuna kopi ya BM. Maana JK anajitahidi kuongea lugha ya kuonyesha kuwa anawajali wananchi wakati akiwakumbatia kina Karamagi, Rita Mlaki, Masha na wengine wa aina hiyo.

JK unatupeleka wapi? Mbona unawageuka wavuja jasho wa nchi hii ya TZ?

Sasa hivi kuna watu wanawacheka Nigeria (Mafuta), Wanamcheka Koni wa Uganda. Lakini hakika nakwambia JK kwa mwendo huo wa Mawaziri wako na Serikali iliyopita ya BM tutayapata ya Nigeria na Uganda usipokuwa makini.

Mbona umewatengeneza kina Kigoda na Sumaye tena? Ogopa sana wananchi waliokata tamaa. Maana wao hungojea mwanzilishi.

Mtu mmoja tu katika baraza lako la mawaziri anayetupa matumaini ni Magufuli tu. Anadiriki kuwanyooshea kidole hata mawaziri wenzake. Kinakuzuia nini kumpa uwaziri mkuu huyo mtu? Tanzania inahitaji PM mwenye guts kama hizi.

PM wako ni playboy hamna kitu. Sawa na Sumaye tu. Mng'oe kabla hajakutia aibu. Mambo yake yoote yanajulikana.

Sasa huyu Rita Mlaki unamkawizia nini kumwambia atangaze kujiuzulu? Soma hapo chini.

========

Magufuli Kiboko!

2006-08-11 17:06:29
Na Usu-Emma Sindila, Dodoma


Katika hali inayodhihirisha kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa John Pombe Magufuli ni kiboko, amemchenjia hata Naibu Waziri wake Mama Rita Mlaki.

Waziri Magufuli ambaye huwa hamwonei mtu haya awapo kazini, amemtoa michozi Mama Mlaki kwa kumpokonya kiwanja chake.

Kiwanja hicho ni miongoni mwa vile ambavyo havijaendelezwa na wamiliki wake.

Magufuli amethibitisha hilo wakati akijibu hoja za wabunge walizozitoa wakati wakichangia hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha wa 2006/07.

Katika watu walionyanganywa viwanja hata Naibu wangu naye yumo,akasema bila hofu.

Akaongeza kuwa watu walionyanganywa viwanja hivyo walipewa notisi ya siku tisini kujieleza ni kwa nini hawaviendelezi katika kipindi chote hicho.

Lakini cha ajabu ni kwamba watu hao wakiulizwa viwanja hivyo ni vya kina nani wanakana na hata Naibu wangu naye alipoulizwa ni cha nani akasema kiwanja hicho sio cha kwake, Mhe. Magufuli akawaambia wabunge.

Katika hatua nyingine, Waziri Magufuli amewapa mwezi mmoja maafisa ardhi wanaohusika na zengwe la nyumba za NHC Tabora kuhakikisha wanazikabidhi hati hizo kwa wenyewe mara moja.

Kuhusu migogoro iliyojaa Wizara ya Ardhi, Mhe. Magufuli amesem ma mingine imedumu kwa miaka zaidi ya 40.

“Mingine imeanza hata kabla sijazaliwa”, akasema.

Amesema katika hali ya kushangaza matapeli yanadiriki kuuzia watu viwanja huko Mbezi hata kwa shilingi milioni 200.

Tunawaomba wabunge watupe nguvu kuchambua migogoro...mingi imejaa matapeli watupu, akasema.

Aidha amesema maofisa ardhi wengine ni matatizo na kero na amewataka wananchi na wabunge kupeleka majina yao ili watimiliwe kazi mara moja.
Mimi siogopi kufukuza kazi watu wazembe, akatamba.

SOURCE: Alasiri
 
Magufuli ni kidampa na mropokaji. Rita amedai kiwanja siyo chake, sasa Magufuli kwanini analitangazia bunge kwamba kiwanja ni mali ya Rita?

Bado hatujasahau kashfa za Magufuli za kutetea uuzwaji wa nyumba za serikali kwa bei poa. Zoezi hilo limeitia hasara kubwa nchi yetu na wananchi mtasaga meno siku mtakapotajiwa hasara hiyo.

Tunahitaji Mawaziri wenye uwezo wa kufikiri na kuchanganua mambo kulingana na ulimwengu wa kileo. Magufuli hana analolojua zaidi ya bomoa-bomoa na upraji wa viwanja.
 
Huyu Magufuli ni kanyaboya. Kama kawaida anatafuta sifa. Wenzake wamemuingiza mkenge. Wamemuacha afanye mambo hayo ya kunyanganya watu viwanja ili wananchi wamchukie na atoke katika mioyo ya watu. Watanzania wangapi wenye uwezo wa kujenga nyumba in 3 years kama sio hao mawaziri na vigogo wengine serikalini? Acha awakera watu ili atakaponyang'anywa uwaziri watu wasilalamike!
 
Jokakuu kabla sijaendelea pamoja na umbumbu wa Magufuli na kupenda sifa kama ilivyo kwa Rais wetu na Waziri Mkuu wake , wewe nawe umepoteza kiwanja ????
 
Muganyizi,
sijapoteza kiwanja.......lakini huyu Magufuli ni mpumbafu, na sifa yake kubwa ni uropokaji,bomoa-bomoa, na huo unyang'anyi anaofanya sasa hivi.

Magufuli anapaswa kutatua migogoro ya umiliki wa viwanja, siyo kunyang'anya viwanja ambavyo vimepatikana kihalali, ila watu wanasuasua kuviendeleza.

Sasa Magufuli anamuumbua Msaidizi wake bungeni ni kwa faida ya nani? Kwanini anajaribu kujengea jina baya Msaidizi wake?

Kama mtu anayeelewa misingi ya mahusiano na maelewano katika sehemu za kazi, naamini kwamba Magufuli amepotoka na kuvuka mpaka.
 
mzawa ,

Ulianza vizuri kujenga hoja zako ila umeniudhi sana pale uliposema ya kuwa Magufuli ndio mtu pekee tunayetakiwa kumpa credit .Magufuli ni mmoja kati ya viongozi washenzi na ambao wako out of touch with the reality !

Magufuli anaendelea kuwa kiongozi simply kwa sababu watanzania ni mambumbu na awajui haki zao , Matatizo ya ardhi hayawezi by simply confiscating those plots , huyu ni mshenzi tuu aliyeweka maslahi yake mbele.
 
JK na EL wanapenda sifa kwa hiyo this guy is perfect one kuwazuka wa TZ wao akina JK na EL wanapeta. Karamagi & co hawawezi kufukuzwa maana waliwekeza mapesa mengi mno kwenye uchaguzi kumpa JK ushindi hana namna na ndiyo maana anatoa hata matamko ambayo hata sasa si Ikulu wala Serikai au CCM imesema hapana.

JK yuko kimya na EL. Kasema Mhindi anatakiwa na JK watu kimyaaaaaaa. Waandishi hakuna wa kuhojI baada ya tamko lile. He went as far as kutukana Watanzania wawekezaji watu kimyaaaaaaaaaa.

JK anaruka mikoani kutembelea Chini anatoa hotuba zenye maneno ambayo walala hoi wanataka kusikia lakini Nchi si walala hoi pekee tuko hapa pia ambao tunataka mambo yaende ya kumuokoa mlala hoi .
 
Hakuna cha ajabu hapa, Mzawa utakutana na upinzani sana ukitaja jina la mtu kuwa waziri mkuu wakati. Kamuulize mmasali mollel aliyekuwa mkuu wa mkoa bado anao? na huyo ni home boy! Kamuulize mtoto wa Sokoine huko USA kwa nini haendi kugombea ubunge Monduli!

baada ya hayo maswali ninasema binadamu ni wagumu kuongozwa! kwa maana wezi, siku zote watalinda wizi wao, wala rushwa watalinda ulji rushwa wao at any cost, (human right nk).

Ni nani asiyejua watu walivyokuwa wamejilimbikizi viwanja Dar na sehemu nyingine TZ?

Sasa leo magufuli ameanza tu kusafisha hata robo ya matatizo hajatatua! watu wanamuita jambazi, mwizi, dicteta mbinafsi nk.

Ninajua inauma sana kama mtu atanyang'anya kiwanja chake cha haraki eti kwa kuwa ameshindwa kujenga. lakini hii isiwe sababu kubwa
ninadhani hilo kosal linarekebishika kama ni kweli ulikuwa na hicho tu!

kumbukeni hata Mkapa alitetea sana 3% ya fedha za madini tena kwa nguvu ZOTE!!

AMETETEA HILO HADI NOVEMBER MWAKA JANA!!

LAKINI LEO TUNASIKIA AMEANZA KUBADILI MSIMAMO!

Bahati nzuri jana nimesikia Rais JK amesema yeye yuko pamoja na Magufuli!
Na amemtaka endelee ili tuwe na miji misafi.Na amesema baada ya miaka 2 watasajijisha what you guys call makosa!

Yangu ni hayo lakini sisemi awe waziri mkuu, time will tell.
 
Nafikri bwana Mzawa5000 alitakiwa apendekeze watu kama Nchimbi, na Basil Mramba. Labda waroho wa madaraka na mafisadi wenzao wengi wangefurahia sana. Hii ni hali ya kawaida katika jamii yoyote, ni vigumu sana kiongozi anayetetea maslahi ya wengi kupendwa na kikundi kidogo kinachojineemesha kutokana na ufisadi,udhaifu,ulafi na ubinafsi, wa watawala.
Enzi ya Kenyatta, watu kama hao walikuwa wanachinjwa kama kuku(rejea kifo cha J.M. Kariuki na wengineo). Tunaamini Kikwete hatafafanya hivyo. Ndiyo maana yuko bega kwa bega kumpa nguvu Magufuli, soma
Maafisa ardhi njia panda:
http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2006/08/16/72527.html,
Lakini, watu kama Lowassa, Nchimbi, Karamagi na Mramba (wanafiki na ma-suicide bombers) wakipata Urais watawachinja au kutowapa nafasi watu kama Magufuli. Ikifika hapo, nafikiri namuunga mkono Mzawa5000 kuwa mambo ya Nigeria na Uganda yataibuka TZ. Nafikiri Kikwete analijua hilo, ndiyo maana jana amepigilia msumari kwa kumpa nguvu zaidi Magufuli.
Mungu ibariki Tanzania.
 
Huyu Magufuli ni kanyaboya. Kama kawaida anatafuta sifa. Wenzake wamemuingiza mkenge. Wamemuacha afanye mambo hayo ya kunyanganya watu viwanja ili wananchi wamchukie na atoke katika mioyo ya watu. Watanzania wangapi wenye uwezo wa kujenga nyumba in 3 years kama sio hao mawaziri na vigogo wengine serikalini? Acha awakera watu ili atakaponyang'anywa uwaziri watu wasilalamike!



wmwansiasa mbona hili umeliangalia kwa upande mmoja tuuu?

labda ungelifanyia critical analysis kisha tujue ukweli uko wapi
 
Ingawaje sipindi hili suala la kunyanganya plots zilizogawiwa miaka ya 80 na early 90's ila hapa waungwana ni lazima maswali tujiulize.
1. Kwa nini wenye viwanja vyao wanavikana?
2. Kwa nini suala hili limefanywa maeneo ya wilaya ya kinondoni tu??

Maeneo ambayo yameshajengwa na kuwa na maendeleo. Mimi nilidhani wangelenga hasa maeneo ambayo ya mapori au watu wenye ekari 10au zaidi kule kibaha, mbagala, mbezi kavu na kwingineko ambako maendeleo yake sio sawa na Mbezi Beach, Mbweni, Goba n.k...!!!
 
Magufuli ndiye waandishi wabongo wanapaswa kumwita kiboko! Perfomance yake inaonekana na ilijidhihirisha akiwa ujenzi,waziri aliyekuwa na data zote za barabara,fedha za kuzijenga,etc. ilifikia tz tukawa model kwa nchi nyingine kuja kuiga mafanikio ya design and build.Tatizo kulikuwa na uvunjaji wa sheria sana watu tuka normalize disorders hivyo magufuli kuleta order ilibidi ije bomoa bomoa,magari ya serikali yaheshimiwe,uzito wa magari usiharibu barabara,etc.Yote haya yaligusa masilahi ya vigogo na ndo hizo propaganda za kumchafua!Nyumba aliuza kwa kuwa ilikuwa sera ya cabinet yote including jk na pia shinikizo la wb. yeye akawa mtekelezaji,lakini pia aliweza kujenga nyuma zingine huko dom na dar,which makes sense.
Rationale ya kunyang'anya watu viwanja ndo tunapaswa kuijua na ni vizuri mwanakijiji amtafute tujue.Kama sikosei nia yake ni kupunguza rushwa maana maafisa ardhi wamehodhi viwanja kibao pasipo nia ya kujenga but just to raise the demand na kuviuza baadae kwa bei kubwa tena mara mbili mbili.
Huyo el ana perfomance background yoyote ya kujivunia kuliko magufuli? Mbona el dikteta mzuri sana kwa control media na wabunge,leave alone kuwa ni corrupt? Magufuli would fit as a pm kuleta discipline na high perfomance maana wabongo tuko wazembe na watu wa maneno mengi pasipo vitendo,bla blah....
Hebu tuone vision ya magufuli kuunganisha tz kwa lami 2007 na daraja la kigamboni kama itakuwa reality!
Long live Pombe wa Magufuli!
 
MUGENYIZI,
Hivi yule meneja mchapakazi,mare.MUGANYIZI wa mradi wa viwanja 20,000 aliyepata ajali jana pale mbuga za serengeti na KUFARIKI NI NDUGU yako?
kama ndie pole saana ,jamaa alikuwa really ! ni kati ya watanganyika ninaowakubali...kwa wale walionunua viwanja wanamfahamu,i remember nimewashauri na nimewasaidia hata rafiki zangu wawili hapo uk na us ,wamenunua viwanja wamejenga so hawataogopa kurudi home kutokana na kuwepo kwa mradi huu.peace and love.RIP!!!!!!
 
MUGENYIZI,
Hivi yule meneja mchapakazi,mare.MUGANYIZI wa mradi wa viwanja 20,000 aliyepata ajali jana pale mbuga za serengeti na KUFARIKI NI NDUGU yako?
kama ndie pole saana ,jamaa alikuwa really ! ni kati ya watanganyika ninaowakubali...kwa wale walionunua viwanja wanamfahamu,i remember nimewashauri na nimewasaidia hata rafiki zangu wawili hapo uk na us ,wamenunua viwanja wamejenga so hawataogopa kurudi home kutokana na kuwepo kwa mradi huu.peace and love.RIP!!!!!!


Ndugu; labda nikuulize huyo meneja mimi namfahamu kwa jina la MUGEMUZI sasa ni mimi nimekosea au wewe ndio umekosea jina au hao ni watu 2 tofauti. Ningependa kujua...Thanks
 
Ni kweli invicible sometimes dr.who anaboa.Mbona amekomalia sana hili suala na ku divert attention yetu kwenye issue za muhimu? Acha majungu toa hoja za kujenga nchi yetu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom