Waziri Kivuli wa Afya Mbassa akomalia mgomo wa madaktari bungeni

ivi lukuvi kaishia levo gani ya elimu?kwan kuna kauli ya serikali na kauli ya mawaziri?au anadhani serikali inaongozwa na nani akiondoa mawaziri?pia kwel govt iko serious mpaka leo kimya?madaktari ebu ungana tena kieleweke.
 
Kwa hiyo Spika anona ni sawa kuendelea na mambo mengine kama kujadili sera ya michezo wakati watu wanakufa?!
Sina hakika kama wabunge wa ccm wanajua hili lakini Spika Makinda atawaletea balaa 2015. Mtindo wake wa kujigeuza serikali na kutotoa kipaumbile mambo ya msingi unawafanya wabunge wa CCM waonekane kama hawajali. Na wengi watazama 2015.
 
Nadhani kuonyesha kuwa chadema wao wako serious na hii issue ya mgomo, kesho ni kukataa kujadili agenda nyingine yoyte isipokuwa hii ya mgomo. Wanapoingia tu bungeni ni kuomba mwongozo na wakiukataa nikutoka nje na kwenda kuongea na waandishi wa habari namna ambavyo wangeshughulikia swala hili kama wao wangekuwa na serikali.
 
Waziri Kivuli wa Afya na Ustawi wa Jamii Gervas Mbassa akomalia mgomo wa madaktari bungeni kwa kutaka Bunge lieleze ni kwanini taarifa ya serikali haipo kwenye ratiba ya bunge. Mbassa aliomba muongozo huo kutokana na maelekezo yaliyotolewa jana na Spika kufuatia hoja ya dharura iliyoanza iliyotolewa na Zitto Kabwe naibu kiongozi wa upinzani bungeni. Katika maelekezo yake Spika alielekeza kwamba kabla ya hoja hiyo ya Zitto tayari Spika alishakubaliana na serikali iwasilishe kauli kuhusu mgomo wa madaktari. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge akitoa maelezo ya nyongeza kufuatia maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Bunge George Simbachawene alisema kwamba serikali itawasilisha kauli yake katika siku itakayopangwa na Spika. Mfululizo huu wa wabunge wa kambi rasmi ya upinzani kuhoji kuhusu suala hilo kunaelekea kuwa ni utekelezaji wa tamko lilotolewa na CHADEMA kwamba “Chama kimewasiliana na kimeitaka kambi rasmi ya upinzani bungeni inayoongozwa na CHADEMA kufanya uchambuzi wa kina kuhusu maelezo hayo na kutumia njia za kibunge katika kuisimamia serikali kushughulikia migogoro kati yake na madaktari, maslahi ya watumishi wa umma katika sekta ya afya pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na sekta ya afya nchini.”

Nimeipenda hiyo
 
swala la msingi ni kwa serikali kutekeleza madai ya msingi ya madaktari,serikali isiyo makini siku zote haijali wananchi wake CDM msirudi nyuma jalini sana matatizo ya wananchi,wananchi wamekosa mtetezi,kama swala la posho wasitishe za wabunge wawape madaktari
 
Hawa Wabunge ni wa hovyo na hawana maana yoyote.

Badala ya kujadili hali tete ya hospitali kukosa madaktari, wanaenda kujadili upumbafu wa Michezo ya Vijana Afrika? Walaaniwe na wafie mbali kabisa. Nimewatoa maanani kwa ujumla.

Ningependa mmoja wao apate ajali ya gari akimbizwe hospitali akute hamna madaktari, labda ndipo wataelewa!

 
Serikali ya wajanja imejaa ujanjaujanja kama wa kina Lukuvi, kukwepesha mambo na changamoto za msingi za nchi si njia ya kutatua matatizo ni bora masuala haya yangejadiliwa wazi na kwa mapana yake ili kufikia ufumbuzi kamili, ukimya, ukwepaji wa changamoto si njia sahihi kutatatua masuala kama haya. JK shtuka, ngoma inazama mkuu........:hatari:

Mkuu Bukanga umesema vyema sana lakini umekosea kumwambia mzee Stuka hawezi ndiyo alivyo alio waweka ndiyo mfano wake yeye yaani ndege wa aina moja huruka pamoja .Wanacho kifanya wao ndicho na yeye anapenda huyu si wa kuamka leo yeye anaulizia kongamano jingine liko wapi Duniani akaonane na matajiri aombe mkuu .
 
Bunge limeshindwa kufanya kazi ya waTZ kwa sababu wamepumbazwa na posho mpya.

Posho ni chombo kinachotumiwa na serikali kuitawala bunge. Inabidi tubadilishe hii hali katika katiba mpya. Mapendekezo yangu ni yafuatayo;
  • Katiba iuwe kabisa ktu kianitwa posho ya vikao
  • Kwenye katiba mpya kuwe na vyumba viwili vya bunge, Senate na Congress,
  • Mshahara wa Senate upangwe na Congress na kupitishwa na Rais
  • Mshahara wa Congress upagwe na Senate na kupitishwa na Rais
  • Senate ya leo ipange mshahara ya Congress lijalo, na sio lililopo madarakani. Vile vile, Congress ipange mshahara wa Senate Ijayo, siyo iliyopo madarakani.
 
Sugu kawaambia leo kipaumbele chao ni vazi la taifa, mgomo wa daktari na maisha ya watanzania si sehemu ya vipaumbele
 
Nchii hii hatuna Bunge, ila tunakundi la wanasiasa wa chama tawala na waupinzani wakiwa pamoja.

Si wabunge tu,nchi haina watu kwani kama sisi ni watu kwa vigezo vya utu tusingewapeleka hawa watu kusimamia mambo yetu.Sasa naamini hawa ni 'sample' yetu, hivyo wanawakilisha tabia yetu sie tuliowachagua.Kwani hata mimi badala ya kuchukua hatua itakayofanya watu hawa wawajibike naishia kuandika hapa kisha basi na ndivyo wengi tulivyo-TUMEKWISHA.
 
ivi lukuvi kaishia levo gani ya elimu?kwan kuna kauli ya serikali na kauli ya mawaziri?au anadhani serikali inaongozwa na nani akiondoa mawaziri?pia kwel govt iko serious mpaka leo kimya?madaktari ebu ungana tena kieleweke.

Lukuvi's intelligence is always questionable!! naomba nao awe inluded kwenye list ya mawaziri 6 wanaotakiwa kuachia ngazi la sivyo sihihi 70 zipatikane.
 
Back
Top Bottom