Waziri Kiongozi kaamua kuwa mfagiaji...

Kibunango

Platinum Member
Aug 29, 2006
8,419
2,270
Waziri Kiongozi wa SMZ ameamua kuwa mfagiaji wa barabara katika Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar. Hatua yake hii imetokana na barabara katika halmashauri hiyo kukithiri wa michanga kiasi cha kushindwa kutofautisha iwapo ni za lami au la!

Aidha watafiti wa mambo ya siasa wanasema hatua hiyo ni sehemu ya mpango wake wa kujiweka karibu na wananchi wa visiwa hivyo katika kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, huku baadhi ya watendaji wa Manispaa wakidai ni njia yake ya kukwamisha ununuaji wa mtambo wa kisasa wa kusafisha barabara visiwani humo... Kwa maelezo zaidi cheki hapa
 
Waziri Kiongozi wa SMZ ameamua kuwa mfagiaji wa barabara katika Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar. Hatua yake hii imetokana na barabara katika halmashauri hiyo kukithiri wa michanga kiasi cha kushindwa kutofautisha iwapo ni za lami au la!

Aidha watafiti wa mambo ya siasa wanasema hatua hiyo ni sehemu ya mpango wake wa kujiweka karibu na wananchi wa visiwa hivyo katika kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, huku baadhi ya watendaji wa Manispaa wakidai ni njia yake ya kukwamisha ununuaji wa mtambo wa kisasa wa kusafisha barabara visiwani humo... Kwa maelezo zaidi cheki hapa

Watafitiwa wa mambo ya siasa wakisema na wewe kibungo kwa kutuwekea blog yako ya propaganda ni sehemu ya mkakati wako wa kugombea uwakilishi ili uchukue nafasi ya Shamsi 2010 au umenunuliwa kumchafua utapinga?
 
Watafitiwa wa mambo ya siasa wakisema na wewe kibungo kwa kutuwekea blog yako ya propaganda ni sehemu ya mkakati wako wa kugombea uwakilishi ili uchukue nafasi ya Shamsi 2010 au umenunuliwa kumchafua utapinga?
Hapo hakuna kununuliwa wala propaganda, Waziri Kiongozi ameamua kufagia barabara, labda ni kutokana na kupungukiwa na kazi za kufanya katika Ofisi yake. Hii si mara yake ya kwanza kuweka majukumu yake pembeni na kukimbilia kufanya kazi za manispaa ingawa manispaa hiyo haipo chini ya Ofisi yake.
 
Du.... Kama WK kaamua kufagia barabara hiyo mbona poa tuu. Nikiwa shule ya msingi iliyoko jirani na Ubalozi wa China, ambapo ubalozi ndio hapo hapo na makazi ndio hapo hapo.
Mesenja mmoja akatumwa apeleke ujumbe wa siri kwa balozi ila ahakikishe anampa balozi mwenywe mkononi.
Mesenja kufika, kupitia geti la grill, aliona wachina wengi wanafanya shughuli za usafi ubalozini hapo, ndipo akabonyeza kengele na kuja kufunguliwa na mmoja wao huku ameshika ufagio mkononi.
Mchina huyo akamkaribisha kwa lugha ya Kiswahili na kumuuliza shida yake.
Mesenja akajibu namuhitaji balozi mwenyewe, Mchina akamjibu "sawa, sema shida yako". Jamaa akasita baadaye akajibu siwezi kukwambia wewe hii shida anatakiwa aisikilize balozi mwenyewe na sio mfanyakazi wa ubalozini.

Ndipo Mchina akamjibu "Mimi ndiye balozi mwenyewe". Jamaa akapigwa na butwaa na kubaki ameduwaa asijue la kufanya ndipo Mchina akamwambia tena sema shida yako, ndipo mesenja akaomba msamaa na kukabidhi ujumbe.

Hivyo ya WK kufanya usafi poa sana tena afike mpaka soko kuu hapo darajani na kuelekea ule upande wa soko la samaki, atakuwa ameisaidia sana ZnZ na 2010 rais yeye!.
 
Hivyo ya WK kufanya usafi poa sana tena afike mpaka soko kuu hapo darajani na kuelekea ule upande wa soko la samaki, atakuwa ameisaidia sana ZnZ na 2010 rais yeye!.
Patakuwa hapakaliki hapo Zenj...
 
Huyu WK ni nationalist mno. Akigombea na akapata tusahau muungano
 
Huyu WK ni nationalist mno. Akigombea na akapata tusahau muungano
MMhm, hapana ila itakuwa ni kinyume chake, Zanzibar kama nchi itatoweka na kuwa mkoa fulani hivi.... Tatizo hana ubavu wa kusimama mbele ya Watanganyika... hivyo atakuwa akiburuzwa tu!
 
Kibunango acha propaganda...

Kama unamjua vizuri Nahodha ni wazi utakubalia this is more that political expedience. This guy has always been simple person hata alipokuwa mwakilishi wa kawaida alikuwa na kibaskeli kake na mpanda daladala. Uteuzi wake ulimkutia njiani akikokota baiskeli.Na hii ni hulka ya kizanzibari ambayo tunaiona kwa viongozi wengi watokao huko. Hulka hii ndio asset muhimu ya wazanzibari hadi sasa inayowafanya kuaminika zaidi kuliko wanasiasa wengine nchini. Ingawa wakati mwengine huwa sababu ya kuzorota kwa mikakati ya kimaendeleo na kwa wengine kuonekana kama kujirahisisha mbele ya jamii ya enzi za "waheshimiwa"

Kwangu mimi huu ni ujumbe mkali kwa watendaji wa manispaa ya Zanzibar kuwajibika ipasavyo.

Omarilyas
 
Huyu WK ni nationalist mno. Akigombea na akapata tusahau muungano

Kuwa Zanzibar Nationalist hakuna maana ya kutokuwa na muungano isipokuwa kuhakikisha kuwa na muungano wenye kuheshimiana na ku-recognize all union parties interests and aspirations.

omarlyas
 
Kibunango acha propaganda...

Kama unamjua vizuri Nahodha ni wazi utakubalia this is more that political expedience. This guy has always been simple person hata alipokuwa mwakilishi wa kawaida alikuwa na kibaskeli kake na mpanda daladala. Uteuzi wake ulimkutia njiani akikokota baiskeli.Na hii ni hulka ya kizanzibari ambayo tunaiona kwa viongozi wengi watokao huko. Hulka hii ndio asset muhimu ya wazanzibari hadi sasa inayowafanya kuaminika zaidi kuliko wanasiasa wengine nchini. Ingawa wakati mwengine huwa sababu ya kuzorota kwa mikakati ya kimaendeleo na kwa wengine kuonekana kama kujirahisisha mbele ya jamii ya enzi za "waheshimiwa"

Kwangu mimi huu ni ujumbe mkali kwa watendaji wa manispaa ya Zanzibar kuwajibika ipasavyo.

Omarilyas

Iwapo anataka Manispaa iwajibike angeweza kufagia mara moja tu na kuwataka waheshimu kazi zao. Hii ni mara ya pili kwa waziri kiongozi kufagia barabara huku akiweka kando matatizo ya msingi ambayo yanasababisha barabara hizo kuendelea kuwa chafu.

Waziri huyo amewahi kuwa miongoni mwa wanzanzibari ambao walishiriki katika programu ya miji endelevu, hivyo anajua nini maana ya kutatua tatizo. Na iwapo anafikili kama yeye ni Waziri Kiongozi na akishika ufagio barabara zitakuwa safi kila siku anakosea sana tena sana. Ni wajibu wake kujua ni kwa nini barabara hizo ni chafu ilhali zinafagiliwa kila siku. Ni wajibu wake kabla ya kukimbilia kushika ufagio kujua kifanyike nini iwapo panahitajika barabara zisizokuwa na michanga mjini humo.

Awali kitengo cha wasafisha barabara kilikuwa na wafagiaji zaidi ya 60 na sasa wapo ishirini tu. Barabara nyingi zimejengwa katika hali ya kuruhusu michanga kuingia barabarani. Kama kweli alikuwa anataka kuona kuwa tatizo la vumbi barabarani linakwisha ilimpasa kuwashirikisha wataalumu katika fani hiyo na sio kusimama kifua mbele mbele ya Baraza la Wawakilishi na kusema kuwa atafagia barabara zote chafu!

Ina maana yeye akishika fagio barabara hizo hazitochafuka tena?
 
Patakuwa hapakaliki hapo Zenj...
WK is a down to earth man of the people. Watu wa aina yake kama alivyo RZ na MBM yaani watu wa kupelekwa pelekwa tuu ndio watadumisha Muungano kwa kuvumilia na kustahimilia ubabe wa Bara.
Kwa wapenda demokrasia ya kweli, alichotaka kufanya Jumbe na Dourado ndicho ZnZ inachotaka. Tuliyaona yaliyomkuta.
Dr. Gharib Bilal pia ni MZnZ wa kweli, yaliyomkuta tunayajua ndio maana kila siku Seif anashinda lakini hapewi nchi, kisa bara yaogopo Seif hata pelekwa pelekwa.
2010 kama sio Mwinyi ni Seif Khatib, lazima wabara wawapangie. Walahi WZnz wakichoka, hata wana CCM wataipa CUF, na ndipo Muungano afanyiwe mapitio kwa ZnZ kupewa haki zake stahili kama mbia mwenye haki sawa na sio mmoja kumburuza mwingine.
 
Ni safi sana WK kufagia na kupata feeling ya kazi za walalahoi.Kuna viongozi ambao wakishachaguliwa tu kumwona kwa karibu ni kwenye gari la 4WD la kiyoyozi.
Baada ya muda anatakata kama katoka kwenye neema, wacha kibarua kiote nyasi ndo utamwaona akisalimia hata wananchi wake.
Tuwe karibu na watu, tufanye kazi zao cheo ni dhamana.
 
Ni safi sana WK kufagia na kupata feeling ya kazi za walalahoi.Kuna viongozi ambao wakishachaguliwa tu kumwona kwa karibu ni kwenye gari la 4WD la kiyoyozi.
Baada ya muda anatakata kama katoka kwenye neema, wacha kibarua kiote nyasi ndo utamwaona akisalimia hata wananchi wake.
Tuwe karibu na watu, tufanye kazi zao cheo ni dhamana.
Kufagia kwa WK sio kuwa anataka kuwa karibu na walala hoi au kupata feeling au kutoa mfano, bali ni kuwapa taarifa kuwa hawawezi kazi na yeye ndio anayeweza kufagia barabara vizuri zaidi yao.

Hafagii barabara kama motisha kwa wafanyakazi hao, ambao wanafanya kazi hiyo katika mazingira magumu bali ni sehemu yake ya kukataa wazo la kununuliwa kwa mtambo/mashine/gari la kuweza kusafisha barabara na hivyo kuziba pengo la upungufu wa wafanyakazi katika kitengo cha wasafisha barabara wa Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar.

Rejea hotuba yake ya kufunga kikao cha Baraza la Wawakilishi aliyoitoa mwishoni mwa mwezi wa kwanza mwaka huu.
 
Watafitiwa wa mambo ya siasa wakisema na wewe kibungo kwa kutuwekea blog yako ya propaganda ni sehemu ya mkakati wako wa kugombea uwakilishi ili uchukue nafasi ya Shamsi 2010 au umenunuliwa kumchafua utapinga?
Duh.Akipigania Kib. kura ya kwanza ya kwangu. Na nitampiogia debe kamanda.
 
Kibunango acha propaganda...

Kama unamjua vizuri Nahodha ni wazi utakubalia this is more that political expedience. This guy has always been simple person hata alipokuwa mwakilishi wa kawaida alikuwa na kibaskeli kake na mpanda daladala. Uteuzi wake ulimkutia njiani akikokota baiskeli.Na hii ni hulka ya kizanzibari ambayo tunaiona kwa viongozi wengi watokao huko. Hulka hii ndio asset muhimu ya wazanzibari hadi sasa inayowafanya kuaminika zaidi kuliko wanasiasa wengine nchini. Ingawa wakati mwengine huwa sababu ya kuzorota kwa mikakati ya kimaendeleo na kwa wengine kuonekana kama kujirahisisha mbele ya jamii ya enzi za "waheshimiwa"

Kwangu mimi huu ni ujumbe mkali kwa watendaji wa manispaa ya Zanzibar kuwajibika ipasavyo.

Omarilyas
Usipake mafuta kwa mgomgo wa chupa
 
WK is a down to earth man of the people. Watu wa aina yake kama alivyo RZ na MBM yaani watu wa kupelekwa pelekwa tuu ndio watadumisha Muungano kwa kuvumilia na kustahimilia ubabe wa Bara.
Kwa wapenda demokrasia ya kweli, alichotaka kufanya Jumbe na Dourado ndicho ZnZ inachotaka. Tuliyaona yaliyomkuta.
Dr. Gharib Bilal pia ni MZnZ wa kweli, yaliyomkuta tunayajua ndio maana kila siku Seif anashinda lakini hapewi nchi, kisa bara yaogopo Seif hata pelekwa pelekwa.
2010 kama sio Mwinyi ni Seif Khatib, lazima wabara wawapangie. Walahi WZnz wakichoka, hata wana CCM wataipa CUF, na ndipo Muungano afanyiwe mapitio kwa ZnZ kupewa haki zake stahili kama mbia mwenye haki sawa na sio mmoja kumburuza mwingine.
Du Pasco I like the way u talk.
 
Kufagia kwa WK sio kuwa anataka kuwa karibu na walala hoi au kupata feeling au kutoa mfano, bali ni kuwapa taarifa kuwa hawawezi kazi na yeye ndio anayeweza kufagia barabara vizuri zaidi yao.

Hafagii barabara kama motisha kwa wafanyakazi hao, ambao wanafanya kazi hiyo katika mazingira magumu bali ni sehemu yake ya kukataa wazo la kununuliwa kwa mtambo/mashine/gari la kuweza kusafisha barabara na hivyo kuziba pengo la upungufu wa wafanyakazi katika kitengo cha wasafisha barabara wa Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar.

Rejea hotuba yake ya kufunga kikao cha Baraza la Wawakilishi aliyoitoa mwishoni mwa mwezi wa kwanza mwaka huu.

Hata hivyo, Kinu it is all in the positive side kwa wananchi,viongozi wangapi wanjishusha?
 
Hata hivyo, Kinu it is all in the positive side kwa wananchi,viongozi wangapi wanjishusha?
Nahisi ujanifahamu. Kuna tatizo la muda mrefu la uchafu wa barabara, na kinachotakiwa ni uvumbuzi wa kudumu kuona kuwa barabara hizo haziwi chafu tena.

Sasa iwapo WK atafagia barabara ambapo hardly itakuwa chini ya nusu saa, bado hatakuwa ametatua tatizo hilo ambalo limeripotiwa katika Baraza la Wawakilishi. Anachojaribu kufanya ni sawa na kejeli kwa wafagiaji wa kila siku wa barabara hizo na sio kujishusha kama unavyodai.
 
Nahisi ujanifahamu. Kuna tatizo la muda mrefu la uchafu wa barabara, na kinachotakiwa ni uvumbuzi wa kudumu kuona kuwa barabara hizo haziwi chafu tena.

Sasa iwapo WK atafagia barabara ambapo hardly itakuwa chini ya nusu saa, bado hatakuwa ametatua tatizo hilo ambalo limeripotiwa katika Baraza la Wawakilishi. Anachojaribu kufanya ni sawa na kejeli kwa wafagiaji wa kila siku wa barabara hizo na sio kujishusha kama unavyodai.

Kamanda - nafikiri ni kejeli. Kwa kweli kama amedhamiria ilikuwa akae kikao na wafagiaji wamueleze shida zao. Azisikilize. Halafu pamoja na kutumia teknologia ya kisasa (hayo magari ya kuzoa taka na kufagia taka) na nguvu kazi-ya wafagiaji- iliyohamasishwa bila ya shaka mji ungengara. Lakini Shamsi -anapuyanga tu.
 
Back
Top Bottom