Waziri Kiongozi apasua jipu wapinzani hoi !!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Waziri Kiongozi awakoromea wapinzani
2008-06-29 12:26:42
Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, imesema kamwe haiwezi kuwakaribisha wapinzani katika Kamati ya Mazungumzo ya kutatua kero za Muungano.

Akifunga mjadala wa makisio ya bajeti ya Ofisi yake kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 Waziri Kiongozi Bw. Shamsi Vuai Nahodha, alisema baadhi ya viongozi wa upinzani ndio wahusika wakuu wa hizi zinazoonekana sasa kuwa kero za Muungano hivi sasa.

Alisema suala la mafuta liliingizwa katika orodha ya mambo ya Muungano wakati huo kiongozi wa hivi sasa wa upinzani katika Baraza la Wawakilishi, Bw. Abubakar Khamis Bakar, akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar miaka ya 1980.

Waziri Kiongozi alisema wakati ule Waziri Kiongozi wa serikali ya Zanzibar alikuwa Maalim Seif Sharif Hamad ambaye hivi sasa ni Katibu Mkuu wa Chama cha CUF.

Alisema kutokana na hali hiyo, anaamini viongozi hao na wengine wa upinzani, walichangia kuongezeka kwa kero za Muungano zinazopigiwa kelele hivi sasa na wao wakiwa mstari wa mbele.

Hata hivyo, alisema serikali ipo tayari kupokea maoni yao, na utaratibu unaotumika sasa wa kuzungumzia kero za Muungano ndio utakaoendelea kutafuta ufumbuzi wa matatizo yaliopo.

Akigusia kero hizo, Waziri Kiongozi alisema kwa vile suala la mafuta liliingizwa ndani ya Muungano kinyemela, basi njia nzuri ya kulitoa ilikuwa ni ile ya kinyemela.

Kauli hiyo ya Waziri Kiongozi ilikuwa ikijibu maswali yaliyotolewa na kiongozi wa upinzani, Bw. Bakara aliyesema kuwa kero za Muungano ni masuala ya kitaifa, hivyo ni vyema na watu wengine wakakaribishwa katika mazungumzo hayo.

Alisema inashangaza kuwa Tume ya Pamoja ya Fedha haijatoa ripoti yoyote ya shughuli zake tokea kuundwa kwake miaka mitatu iliyopita.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa upinzani, inaonekana ni vyema na hiyo tume ikaundiwa tume kuchunguza shuguli zake.

Waziri Kiongozi alisema kuwa mgao wa mafuta na gesi, ripoti yake inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, mwaka huu.

Lakini kabla ya mshauri elekezi kuanza kazi, atakutana na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ili kubadilishana mawazo na kupata maoni yao.

Alisema jumla ya shilingi 328 milioni zinatarajiwa kutumika kwa hizo shughuli za mshauri elekezi za kufanya utafiti na kuweka utaratibu wa mgao wa mapato ya mafuta na gesi kati ya pande mbili za Jamhuri ya muungano.

Alisema kwa hivi sasa Kamati ya Mazungumzo inaendelea kufanyia kazi utaratibu wa kuchangia gharama za Muungano.

Hata hivyo, akaunti ya pamoja kati ya Serikali ya Muungano na ya Zanzibar itayosimamia suala hili bado haijaanzishwa.

Waziri Kiongozi alikiri kuwa ni kweli Tume ya Pamoja ya Fedha imechelewa kutoa ripoti yake juu ya mgawanyo w amapato,lakini hii inaeleweka kwa kuwa suala hili ni zito na linahitaji kufanyiwa kazi kwa umakini.

Hivi sasa, alidokeza, yapo maoni tafauti juu ya mgao huo. Baadhi ya watu wanasema Zanzibar ipewe asilimia 10 na wengine wanaona ni vyema ikapatiwa asilimia 15, badala ya mgao wa asilimia 4.5 unaotumika hivi sasa.

Nahodha alikataa kuwepo ubaguzi wa ina yoyote kati ya Visiwa vya Unguja na Pemba isipokuwa bajeti ya kisiwa ya Unguja inaonekana kuwa kubwa kwa vile ndio makao makuu ya nchi.

SOURCE: Nipashe
 
Mtu wa Pwani,
alisema baadhi ya viongozi wa upinzani ndio wahusika wakuu wa hizi zinazoonekana sasa kuwa kero za Muungano hivi sasa.
Alisema suala la mafuta liliingizwa katika orodha ya mambo ya Muungano wakati huo kiongozi wa hivi sasa wa upinzani katika Baraza la Wawakilishi, Bw. Abubakar Khamis Bakar, akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar miaka ya 1980
Waziri Kiongozi alisema wakati ule Waziri Kiongozi wa serikali ya Zanzibar alikuwa Maalim Seif Sharif Hamad ambaye hivi sasa ni Katibu Mkuu wa Chama cha CUF.
Alisema kutokana na hali hiyo, anaamini viongozi hao na wengine wa upinzani, walichangia kuongezeka kwa kero za Muungano zinazopigiwa kelele hivi sasa na wao wakiwa mstari wa mbele.
Hapa mkuu nitakuwa upande wa Wapinzani na Mh. Shamsi Vuai kasema maneno yanayopotosha na hata kuhatarisha zaidi Muungano.
Kulingana na maelezo ya Shamsi hao watu wawili wakati wa miaka ya 80 walikuwa ktk ngazi za juu kisheria kama viongozi wa Zanzibar.. Kikatiba walikuwa na madaraka makubwa sana ktk kutafuta suluhu ya hizo KERO...Swala la wao walipo upande gani leo hii sii akili nzuri kabisa!... inashangaza kuona viongozi wetu wanavyofikiria..
Kama kweli anaamini kuwa hawa watu waliingiza kero hizi kinyemela kwa sababu tu leo hii wapo Upinzani basi hii ni hatari kubwa sana ktk usalama wa nchi yetu kwa sababu inaonyesha wazi hakuna sababu ya kuwa na Bunge! hawa watu wako nje ya Utawala wa CCM hivyo walipoondoka wameondoka na hoja zao hata kama zina haki...
Sasa tazama, Je, ikiwa hawa wako nje ya CCM na hoja hizi hazina nguvu tena, itakuwaje kuhusu Muungano wenyewe ambao waanzilishi wake wote wamesha KUFA?...WHY keep MUUNGANO ambao uliwekwa na vyama vya TANU na ASP ambavyo vyote havipo tena ktk orodha ya vyama vyetu?...Je Muungano huo haukuingizwa kinyemela?...kuna haja gani ya kuwepo mazungumzo badala ya kuuondoa pia Kinyemela maanake walioutunga wako makaburini, huo Muugano tuupelekee huko huko!
Haya ni maswali ambayo yanafuatia kutokana na usemi wa Mh. Shamsi..Na hakika Kikwete hana watu kabisa walioiva Kisiasa!.. a bunch of Idiot!

Binafsi nachokataa ni suala la kero za Muungano kuhusishwa vyama viwili tu yaani CCM na CUF. Hizi kero za Muungano ni swala la Jamhuri nzima ambalo lilikubalika toka Mwalimu akiwa hai na limepewa kipaumbele sii kwa sababu ya kero za Viongozi wanaogombea madaraka - laa! isipokuwa tofauti zilizopo kati ya Bara na Visiwani ndani ya Muungano pia ktk kuheshimu Sovereignty ya nchi hizi mbili zilizoungana.. Ni matatizo yanayotokana na Katiba sio tofauti zilizopo kati ya uongozi wa Mh. Karume na Sharrif Hamad!..muafaka kati ya CCM na CUF ndio makosa makubwa yanayotaka kufanyika Kikatiba!
CCM ni lazima wawe makini sana ktk swala hili mwalimu hakuwa mjinga alipokubali baadhi ya kero hizi kutafutiwa Ufumbuzi ambao hadi leo hii unafanyiwa mazingaombwe na viongozi wenye imani za Kichawi..Not all Tanzanians are dumb, tunaona kabisa mnavyobadilisha sindano kuwa fedha midomoni mwenu, huu ni mchezo ambao wananchi pia wanauweza...
 
Karume na huyu vuai wameshindwa kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanziabar wamebakia kupiga soga na kuogopa hata vivuli vyao. IQ 7 personalities
 
Back
Top Bottom