Waziri Kijaji: Sitakuwa mvumilivu kwa yeyote atakayeandika habari zenye viashiria vya uvunjifu wa amani

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,582
6,627
Septemba 16, 2021

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kijaji amesema hatakuwa tayari kuvumilia Vyombo vya Habari na Waandishi watakaoandika habari za kutaka kulichafua Taifa.

Waziri Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua mafunzo ya Kamati ya Ukaguzi ya Wizara hiyo jijini Dodoma.

"Lazima katika utendaji kazi wa Waandishi wa Habari watangulize uzalendo kwa Taifa."

"Niwahakikishie, sitakuwa mvumilivu kwa yeyote atakayejaribu kufanya hivyo kuandika habari zenye viashiria vya Uvunjifu wa Amani, tutachukua hatua," amesema.

Chanzo: Dk. Kijaji avipiga mkwara vyombo vya habari
 
Mbona hajafafanua aina ya viashiria au ndio mhemuko wa kuanza kutishana mapeema asubuhi.

Kwani viongozi wateuliwa wa Tanzania maadili ya kazi hawana ni kulazimisha badala ya kukaa na wadau husika kupeleka taifa mbele!

Nani anapenda kuleta taharuki kama sio wenyewe na polisi wao.!

Fanyeni kazi kwa weledi.
 
Hii nchi wanaume tunapenda kulelewa... Kama hadi ulinzi nao anasimamia mama basi tena!

Kilichobaki waziri mkuu apewe mwanamama biashara yisheeee
 
Ameanza kulipa fadhila mapema sana, anaonesha wazi atakuwa analinda maslahi ya CCM kwa mgongo wa kutokuwa wazalendo, badala aseme vyombo vitakavyoenda kinyume na sheria ndio vitachukuliwa hatua, huu muendelezo wa kubadilisha sura za watu lakini akili zinabaki zilezile unalidumaza taifa.
 
19E52BCA-AC6D-440A-9F10-EEE5400DE316.jpeg
 
Dodoma. Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini Tanzania, Dk Ashatu Kijaji amesema hatakuwa na uvumilivu kwa wanahabari watakaojihusisha na habari zinazolichafua Taifa.

Hii ni mara ya kwanza kwa Dk Kijaji kuzungumza na umma baada ya kuteuliwa na kuapishwa Septemba 13 2021.

Dk Kijaji ameyasema hayo leo Alhamis Septemba 16 2021 wakati akizindua kamati ya ukaguzi ya Tehema.

Waziri huyo ametaka kupunguzwa kwa malalamiko yanayohusiana na idara ya Habari waliongezewa katika wizara hiyo Septemba 12 2021.

“Wanahabari lazima tuelewane hapa lazima tuchuje nini watanzania wanataka kukisikia, kile unachokiandika, kile unachokitangaza kiwe na maslahi mapana,” amesema.

Amesema kwa kila mmoja kujivunia kuwa Mtanzania kutasaidia katika kuepusha vishawishi vya kulichafua Taifa.

Amesema pia kutaepusha vishawishi vya kuwafanya watanzania wasikie wasichotarajia kukisikia.

“Na kwa hili niseme sitokuwa na uvumilivu tutasimamia maadili na kamati tuwezesheni ili Taifa lipate taarifa zinazohitajika tu na zisizohitajika hazuzitaki,” amesema
waziri-wa-habaripicc.jpg
 
Aache mihemko,
Kwanza anajua sheria za habari, teknolojia na mawasiliano?

NB: Dk.Bajaji huwezi kushindana na kasi ya TEHAMA.
 
Septemba 16, 2021

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kijaji amesema hatakuwa tayari kuvumilia Vyombo vya Habari na Waandishi watakaoandika habari za kutaka kulichafua Taifa.

Waziri Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua mafunzo ya Kamati ya Ukaguzi ya Wizara hiyo jijini Dodoma.

"Lazima katika utendaji kazi wa Waandishi wa Habari watangulize uzalendo kwa Taifa."

"Niwahakikishie, sitakuwa mvumilivu kwa yeyote atakayejaribu kufanya hivyo kuandika habari zenye viashiria vya Uvunjifu wa Amani, tutachukua hatua," amesema.

Chanzo: Dk. Kijaji avipiga mkwara vyombo vya habari
Shida ya kua umeondolewa antena chanel zinapotea,kondoa moja
 
Back
Top Bottom