Cannabis
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 8,937
- 25,279
Waziri wa Wizara ya utalii na maliasili Dr. Hamis Kigwangalla amsifu na kumshukuru Rais. Dr. John Pombe Magufuli wa uamuzi wa kuruhusu ndege za watalii kuanza kuingia nchini Tanzania hivi karibuni na kutowaweka watalii karantini kwa siku 14 na baadala yake kuwapima tu joto na kuwaruhusu waendelee na mapumziko nchini.
Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter Dr. Kigwangalla alisema "Tunampongeza sana na kumshukuru Mhe. Rais, Dr. John Pombe Magufuli kwa hotuba yake ya leo kule Chato. Hotuba imetupa mwongozo mzuri wa kutupeleka mbele. (1.) Anga sasa linafunguliwa kwa ndege za abiria, ndege zinaanza kutua na (2.) Wageni hawatowekwa karantini ya siku 14!"
Vile vile alisisitiza kwamba ni muhimu kwa watanzania kukubali hali halisi na kuendelea kuishi na ugonjwa huu wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya corona. Dr. Kigwangalla aliuhakikishia umma kuwa atakuja na Standard Operating Procedures (SOP) wiki ijayo katika sekta hii muhimu ya utalii kwa kusema "Korona ipo na sasa tuishi nayo tu kwa tahadhari zote.
Kama tunavyojikinga na malaria na HIV/UKIMWI (ambao upo pabaya kabisa!), hatupaswi kushindwa kujikinga dhidi ya Korona. Tumeandaa Mwongozo (SOPs) wa biashara ya utalii zama za korona, ambao ntautangaza rasmi wiki ijayo" na akisisitiza zaidi kuwa wamejipanga kuwalinda watalii dhidi ya maambukizi ya virusi hivi hatarishi vya corona "Tunafungua biashara ya utalii kwa tahadhari zote dhidi ya korona.
Tumejipanga vizuri kuhakikisha tunadhibiti maambukizi mapya ya korona kwenye mnyororo wote wa utalii. "
Waziri Kigwangalla ambaye pia ni mwanasayansi mbobezi katika masuala ya afya, amesisitiza kwamba anajua anachokisema na kama mtaalamu hakuna haja ya kuendelea kujifungia huku watu wakikosa pato la fedha za kigeni.
Amewasihi wadau wa sekta ya utalii kujiandaa kupokea watalii huku wakizingatia hatua zote za kujikinga.
Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter Dr. Kigwangalla alisema "Tunampongeza sana na kumshukuru Mhe. Rais, Dr. John Pombe Magufuli kwa hotuba yake ya leo kule Chato. Hotuba imetupa mwongozo mzuri wa kutupeleka mbele. (1.) Anga sasa linafunguliwa kwa ndege za abiria, ndege zinaanza kutua na (2.) Wageni hawatowekwa karantini ya siku 14!"
Vile vile alisisitiza kwamba ni muhimu kwa watanzania kukubali hali halisi na kuendelea kuishi na ugonjwa huu wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya corona. Dr. Kigwangalla aliuhakikishia umma kuwa atakuja na Standard Operating Procedures (SOP) wiki ijayo katika sekta hii muhimu ya utalii kwa kusema "Korona ipo na sasa tuishi nayo tu kwa tahadhari zote.
Kama tunavyojikinga na malaria na HIV/UKIMWI (ambao upo pabaya kabisa!), hatupaswi kushindwa kujikinga dhidi ya Korona. Tumeandaa Mwongozo (SOPs) wa biashara ya utalii zama za korona, ambao ntautangaza rasmi wiki ijayo" na akisisitiza zaidi kuwa wamejipanga kuwalinda watalii dhidi ya maambukizi ya virusi hivi hatarishi vya corona "Tunafungua biashara ya utalii kwa tahadhari zote dhidi ya korona.
Tumejipanga vizuri kuhakikisha tunadhibiti maambukizi mapya ya korona kwenye mnyororo wote wa utalii. "
Waziri Kigwangalla ambaye pia ni mwanasayansi mbobezi katika masuala ya afya, amesisitiza kwamba anajua anachokisema na kama mtaalamu hakuna haja ya kuendelea kujifungia huku watu wakikosa pato la fedha za kigeni.
Amewasihi wadau wa sekta ya utalii kujiandaa kupokea watalii huku wakizingatia hatua zote za kujikinga.