Choi Kang Ta
Member
- Aug 25, 2014
- 86
- 54
Unauhakika kuwa yesu aliwahi kuwepo duniani na si imaginary figure!? Una uhakika yesu ndiye mwanzilishi wa ukristo duniani!? Unafahamu mini juu ya uyahudi, ukristo na uislamu!? Unaweza kunichambulia kwa kina ufanano na utofauti wa imani/dini hizo kwa kuzingatia historia na misingi mikuu ya imani hizo na unieleze kipi kina nguvu zaidi kati ya ufanano na utofauti huo kwa ushahidi!? Je ukweli juu ya imani hizo unaweza kupatikana pia nje ya vitabu vya imani hizo na kwa ushahidi!?Misingi ya Ukristo na Uislamu ipo katika Uyahudi.
Yesu niuzaowa Wayahudi, Ukristo umetokea kwa Yesu, Ukristo umetokana na Uyahudi.
Vitabu vya Agano la KAle vipo kwenye biblia ya Wayahudi kabla Yesu hajazaliwa.
Quran Muhammad katohoa sehemu kubwa tukwenye historia iliyowekwa na Wayahudi.
Na zaidi, hizi habari za Ukristo, Uislamu na matambiko ya asili ya Afrika, zote ni sawa tu.
Zote ni habari za kuamini katika supernatural powers bila ya uthibitisho.
Sasa utaanzaje kubagua kwamba haya wanaofanya waafrika ni shirka, ni ushenzi, wakati hata wakristo na waislamu nao wana symbolism hizo hizo za kuwekwa wakfu ina supernatural context, ambazo ukizifuatilialogically huwezi kupata uthibitisho kwamba zina lolote zaidi ya symbolism?
Sasa tunatukana matambiko ya Kiafrika kwamba ni shirka, wakati Uislamu na Ukristo ni yale yale tu?
Au ndiyo kasumba ya inferiority complex ya "Uafrika ni ushenzi".
Mimi naweza kusema hiyo symbolism haina maana zaidi ya syymbolism, kama mtu anavyoweza kubatizwa kanisani au kupata maji ya zamzam kwenye Hijja.
Vyote ni symbolism tu.
Sasa tunabagua symbolism za Kiafrika tunaziita shirka, za Waarabu na Wayahudi tunaziita dini?
Afrika hatuwezi kuendelea bila kupita kigingi hiki.
Tutaendeleaje wakati tushajikubalia wenyewe kwamba waliochaguliwa na Mungu ni Warabu, Wayahudi na Wazungu, sisi tunawasindikiza na tunawatumikia tu?
Ukristo na uislamu ni wa wazungu na waarabu tu. Na ndio waanzilishi na wanufaika wakuu.