Waziri Kapuya aibiwa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Nilishawahi kusikia Mkapa na yule aliyekuwa anampigia debe kwenye kinyang'anyiro cha 2005, A. Kigoda nao wana mgodi wao wa dhahabu. Nilidhani ni porojo tu lakini baada ya kuona hii article inawezekana ikawa ni kweli

Waziri Kapuya aibiwa

na David Frank, Arusha
Chanzo: Tanzania Daima

MGODI wa madini ya rubi unaomilikiwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Profesa Juma Kapuya, uliopo wilayani Longido, mkoani Arusha, umeibiwa mashine ya kupulizia hewa ndani ya mgodi (compressor).

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Basilio Matei, zinaeleza kuwa wizi huo ulitokea Septemba 16, mwaka huu, wakati wa usiku katika mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Kiseeriani.

Kamanda Matei alisema kwamnba kutokana na tukio hilo, watu wanne wanashikiliwa na polisi. Aliwataja watu hao kuwa ni Nyinyila Mwambasa (31), dereva wa gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T 826 AJT, mkazi wa Makao Mapya, Arusha, Daniel Barnabas (2, mkazi wa Lendikinya wilayani Monduli, Lomayani Kalea (25), mkazi wa Buguruni Namanga na Jumanne Ramadhani (26), mkazi wa Arusha.

Akielezea tukio hilo, Kamanda Matei alisema kwamba watu hao baada ya kuiba mashine hiyo walitoroka kwa kutumia gari hilo, lakini walikamatwa walipofika maeneo ya Namanga.

Alisema kwamba wizi huo ulipangwa kwa muda mrefu na baadhi ya watumishi wa mgodi huo kwa kuwa si rahisi kwa watu wa nje kuweza kuingia ndani ya mgodi bila mwenyeji.

Katika tukio jingine, Kamanda Matei alisema kwamba majambazi watatu wakiwa na silaha za moto, jana, walimjeruhi kwa risasi Mhasibu wa kampuni ya Utalii ya Abacombe and Kent ya Arusha, Fabiana Mhindi, wakati akiwa katika gari la kampuni hiyo lililokuwa na fedha alipokuwa akitokea benki ya NBC.

Alisema tukio hilo ambalo majambazi hao hawakufanikiwa kupora fedha zilizokadiriwa kuwa sh milioni 2.8 lilifanyika jana saa 9.45 alasiri, nje ya lango kuu la kuingilia ofisi za kampuni hiyo.

Alisema baada ya mhasibu huyo kufika katika lango hilo akiwa na dereva Athuman Mnyombe (35), aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili T869 AFL wakisubiri kufunguliwa lango hilo, ghafla walitokea watu watatu wakiwa katika pikipiki yenye namba T199 AMB na kuwavamia.

Baada ya kuvamia walifyatua risasi moja hewani ili kuwatisha kabla ya kupiga risasi nyingine katika kioo cha mbele cha gari hilo, iliyomjeruhi mhasibu huyo begani.

Mara baada ya kutokea kwa jambo hilo mhasibu huyo alitoa taarifa polisi waliofanikiwa kuwakamata majambazi wawili kati ya watatu katika eneo jirani na hoteli ya kitalii ya Impala.

Aliwataja watu wanaoshikiliwa kuwa ni Samuel Lucas (23), mkazi wa Sakina Kiranyi na Emmanuel Willium (23), mkazi wa Ekenywa wilayani Arumeru.
 
What is so special kwa Kapuya kuibiwa. Watanzania wangapi wanaibiwa kila siku?
 
What is so special kwa Kapuya kuibiwa. Watanzania wangapi wanaibiwa kila siku?

Nia hasa ya kupost article hii ni hiyo habari kwamba mgodi huo unamilikiwa na Waziri. Je mawaziri na Vingunge wangapi katika nchi yetu wana migodi yao binafsi? Je ni halali kwa mtu binafsi kuwa na mgodi wake badala ya rasilimali hizi kuwa za Watanzania wote?
 
Nia hasa ya kupost article hii ni hiyo habari kwamba mgodi huo unamilikiwa na Waziri. Je mawaziri na Vingunge wangapi katika nchi yetu wana migodi yao binafsi? Je ni halali kwa mtu binafsi kuwa na mgodi wake badala ya rasilimali hizi kuwa za Watanzania wote?


Du Mzee naona sasa baadhi ya watanzania tumeingiwa na sumu. sikukufikiria haraka hiyo thread on that angle. Kweli, nadhani mwandishi angesema tu Kapuya naye anamiliki mgodi!
 
Waandishi wana "sense of news" wanapima na kuona kuwa ni kitu gani kinaweza kufanya jambo kuwa habari. Kwa harakaharaka mimi naona aliyeandika habari hiyo ana high sense of news; Bila shaka kaangalia mambo/vigezo matatu kutengeneza hiyo habari 1. Kapuya ni waziri 2. Alipata ajalijuzijuzi 3. Suala la kumiliki mgodi. Tukianza na kigezo cha kwanza, kwa kuwa Prof. Kapuya ni waziri, tena wa ulinzi anajulina na ana uzito katika jamii, kwa hivyo hata kama angeibiwa nyumbani kwake ingeandikwa na bado ikawa na uzito. Kigezo cha pili kinaweza kutumika kwa lengo la kuionesha jamii juu ya namna gani anazidi kuandamwa na masahibu. Na Kigezo cha tatu bila shaka kinazingatia ukweli kuwa suala la migodi/madini kwa sasa linazungumzwa/liko katika mjadala mkubwa katika jamii yetu.


Kuhusu kumiliki kwake mgodi kama waziri mimi sioni kama kuna tatizo sana. Kwa jinsi ninavyoelewa, mara nyingi madini ya rubi yanachimbwa na wachimbaji wadogo wadogo na mtu yeyote kwa nafasi yake nadhani anaweza kufanya hivyo.
 
Waandishi wana "sense of news" wanapima na kuona kuwa ni kitu gani kinaweza kufanya jambo kuwa habari. Kwa harakaharaka mimi naona aliyeandika habari hiyo ana high sense of news; Bila shaka kaangalia mambo/vigezo matatu kutengeneza hiyo habari 1. Kapuya ni waziri 2. Alipata ajalijuzijuzi 3. Suala la kumiliki mgodi. Tukianza na kigezo cha kwanza, kwa kuwa Prof. Kapuya ni waziri, tena wa ulinzi anajulina na ana uzito katika jamii, kwa hivyo hata kama angeibiwa nyumbani kwake ingeandikwa na bado ikawa na uzito. Kigezo cha pili kinaweza kutumika kwa lengo la kuionesha jamii juu ya namna gani anazidi kuandamwa na masahibu. Na Kigezo cha tatu bila shaka kinazingatia ukweli kuwa suala la migodi/madini kwa sasa linazungumzwa/liko katika mjadala mkubwa katika jamii yetu.


Kuhusu kumiliki kwake mgodi kama waziri mimi sioni kama kuna tatizo sana. Kwa jinsi ninavyoelewa, mara nyingi madini ya rubi yanachimbwa na wachimbaji wadogo wadogo na mtu yeyote kwa nafasi yake nadhani anaweza kufanya hivyo.


Kwa maana nyingine kama Buzwagi inakuwa owned na Karamagi hakuna tatizo! Mapato yote ya mgodi huo yakiwa ya Karamagi badala ya kuwa mapato ya Taifa hakuna tatizo! Mwe! Kazi kweli kweli!
 
Jamani na mimi nataka Plot huko Longido kwenye madini in particular, nifanyeje nipate, au mpaka niwe kwenye Cabinet
 
Jamani na mimi nataka Plot huko Longido kwenye madini in particular, nifanyeje nipate, au mpaka niwe kwenye Cabinet


kaka ukiona wanagombea na kutakiana mabaya wenyewe kwa wenyewe ..usifikiri wana uchungu na wewe ..faida ni nyingi zikiwemo kugawiwa migodi buuure..
 
Wa Tanzania tulie tuuu maana hata hizo ardhi kidoogo tunazojaribu kuzimiliki kwa jasho letu in the formof mashamba n ardhi twanyanganywaa..lakini vigogo wana hadi plot za migodi..

No wonder why hatutaendelea kamwe ni kama tumelaaniwa,Tanzanite ni mostly yapatikana Tz tu lakini nchi zinazoongoza kwa ku export tanzanite Tz is not even in the top 3 of them..i find it as ni utani kama sio joke
 
What is so special kwa Kapuya kuibiwa. Watanzania wangapi wanaibiwa kila siku?

Du Mzee naona sasa baadhi ya watanzania tumeingiwa na sumu. sikukufikiria haraka hiyo thread on that angle. Kweli, nadhani mwandishi angesema tu Kapuya naye anamiliki mgodi!

Jamani na mimi nataka Plot huko Longido kwenye madini in particular, nifanyeje nipate, au mpaka niwe kwenye Cabinet

Hakuna jipya lolote Mh. Kapuya kumiliki mgodi, wala hakuna ubaya wowote, labda tu mwandishi kaamua 'kutuuzia' gazeti.

Mwaka 1995 nilibahatika kutembelea sehemu za 'machimbo' ya madini kule Tunduru, enzi hizo jiwe lilokuwa linatoka lilikuwa ALEXANDERLITE, na kule maeneo ya babati -KANGALA ambako vijana walikuwa wanachimba RODLITE. Niliyoyaona huko mpaka leo nimeamini jinsi watu wakiamua, wanavyojituma na migodi yao kuitafuta shilingi. (Japo kuna waliokufuru mfano jamaa mmoja ambaye baada ya kuuza mawe yake ya ALEXANDERLITE kwa Tshs 500,000,000/=, YES, Millioni Mia tano!, jamaa alinunua Landrover hapo hapo Tunduru, na kulikosha kwa bia!)

Wajemeni, Tanzania imebarikiwa madini ya kila aina kwa aina, na sehemu zote hizo nilizokwenda kuna wachimbaji wadogo wanaoendesha maisha yao kwa huo uchimbaji 'wa kubahatisha', na kuuza 'mawe' yao kwa wa-thai kuanzia kule kule Tunduru mpaka pale Upanga, nk.

Biashara ya madini ngumu wazee asikwambie mtu. Ukiona Sunda, au Askofu nk waliibua 'mawe' ya TANZANITE ya mamilioni ya shilingi jua cha moto walikiona, kwani kazi hiyo hawakuifanya kwa siku au mwezi mmoja! (Askofu alipochanganyikiwa na kuanza kuzimwaga pesa toka ghorofani pale Palsons Hotel, ilikuwa ni mfano tosha wa 'wazimu' wa mawe!)

Sehemu nyingi nchini Tanzania bado kuna wachimbaji wengi wadogo walojianzishia 'migodi' yao,... na serikali sana sana inatumia watendaji wa vijiji ku control, kwani kinachopatikana sana sana kinamfaa huyu mchimbaji na kidogo mfanyabiashara (middle man) anayelipeleka kuuza jiwe mjini.

Kwahiyo ndugu yangu AUGUST kama kweli unataka plot, jifungashe ukaweke kambi huko Longido,...ila ujue mgodi mpaka 'uteme', kazi umeifanya, na kati ya hayo mawe utayoyapata tegemea ma rejekti kibao na kulaliwa kwa sana na wa thailand.
 
jamani hiyo ni mwanzo tu ,,mungu atawaonyesha yote pamoja na yanayomilikiwa na JK NA ROSTAM AZIZ,,ACHA ILE YA JAMAA WETU WA MWANZA NAIBU WAZIRI,,MUNGU TUOKOE KAMA SI MAPENZI YAKO UTUEPUSHE NA VIKOMBE HIVI
 
August Migodi Ipo Kama Mchingoma Alivyosema Aacha Kulaliwa Mpaka Uteme..usishangae Kuambiwa Ukamkate Kichwa Mama Yako Au Ndugu Yoyote Chimbo Liteme Utaweza ,,anachofanya Kapuya Na Jk Na Ra Wanajua Wenyewe Wewe Utaweza?????karibu
 
August Migodi Ipo Kama Mchingoma Alivyosema Aacha Kulaliwa Mpaka Uteme..usishangae Kuambiwa Ukamkate Kichwa Mama Yako Au Ndugu Yoyote Chimbo Liteme Utaweza ,,anachofanya Kapuya Na Jk Na Ra Wanajua Wenyewe Wewe Utaweza?????karibu

Kama kuna masharti ya Mganga , au kumchinja Mama Yangu, Basi Ngoja niwaachie wenyewe, mimi niwe msindikizaji tu.
 
Hakuna jipya lolote Mh. Kapuya kumiliki mgodi, wala hakuna ubaya wowote, labda tu mwandishi kaamua 'kutuuzia' gazeti.

Mwaka 1995 nilibahatika kutembelea sehemu za 'machimbo' ya madini kule Tunduru, enzi hizo jiwe lilokuwa linatoka lilikuwa ALEXANDERLITE, na kule maeneo ya babati -KANGALA ambako vijana walikuwa wanachimba RODLITE. Niliyoyaona huko mpaka leo nimeamini jinsi watu wakiamua, wanavyojituma na migodi yao kuitafuta shilingi. (Japo kuna waliokufuru mfano jamaa mmoja ambaye baada ya kuuza mawe yake ya ALEXANDERLITE kwa Tshs 500,000,000/=, YES, Millioni Mia tano!, jamaa alinunua Landrover hapo hapo Tunduru, na kulikosha kwa bia!)

Wajemeni, Tanzania imebarikiwa madini ya kila aina kwa aina, na sehemu zote hizo nilizokwenda kuna wachimbaji wadogo wanaoendesha maisha yao kwa huo uchimbaji 'wa kubahatisha', na kuuza 'mawe' yao kwa wa-thai kuanzia kule kule Tunduru mpaka pale Upanga, nk.

Biashara ya madini ngumu wazee asikwambie mtu. Ukiona Sunda, au Askofu nk waliibua 'mawe' ya TANZANITE ya mamilioni ya shilingi jua cha moto walikiona, kwani kazi hiyo hawakuifanya kwa siku au mwezi mmoja! (Askofu alipochanganyikiwa na kuanza kuzimwaga pesa toka ghorofani pale Palsons Hotel, ilikuwa ni mfano tosha wa 'wazimu' wa mawe!)

Sehemu nyingi nchini Tanzania bado kuna wachimbaji wengi wadogo walojianzishia 'migodi' yao,... na serikali sana sana inatumia watendaji wa vijiji ku control, kwani kinachopatikana sana sana kinamfaa huyu mchimbaji na kidogo mfanyabiashara (middle man) anayelipeleka kuuza jiwe mjini.

Kwahiyo ndugu yangu AUGUST kama kweli unataka plot, jifungashe ukaweke kambi huko Longido,...ila ujue mgodi mpaka 'uteme', kazi umeifanya, na kati ya hayo mawe utayoyapata tegemea ma rejekti kibao na kulaliwa kwa sana na wa thailand.

Kwa maoni yangu kuna tofauti kubwa ya wachimbaji wadogo wadogo kujitafuria riziki na viongozi wa juu wa Chama na Serikali kuwa wanahodhi machimbo ya madini ya aina yeyote. Leo wanaown machimbo ya Rubi kesho itakuwa machimbo ya almasi na dhahabu. Hii rasilimali ni ya Watanzania wote hivyo pato lake linastahili kuingia kwenye mfuko wa Taifa badala ya watu binafsi. Kwa maoni yangu si haki kwa watu binafsi kuown rasilimali za Watanzania (migodi ya madini) Si tulishasikia hapa kwamba Yona na Mkapa wanaown Kiwira Coal Mining? Je nani aliwapa haki ya kuown KCM? Walilipa kiasi gani na kwa nani?
 
Take five Bubu ataka Kusema
Na pia kama hiyo allocation ya plot ilifanyika kihalali au ndio kuwafukuza wachimbaji wadogo, mfano ni huko merererani wakapewa Tanzania One na Akina Retired General Mboma etc etc
 
Nilikuwa sijui kuwa hata kapuya ana mgodi!Jamani sasa CCM ni chama cha Mabusiness!Kwa nini bado tunawachagua hawa wakati inaonekana wazi kuwa wote wako kwenye siasa kufanya biashara!Huu ujinga wetu watanzania utaisha lini?
 
Kiswahili kinakuwa tatizo hata kwa waswahili wenyewe... WAZIRI KAPUYA AIBIWA! mbona taarifa nilizonazo ni kuwa waziri Kapuya leo kapelekwa India kwa matibabu zaidi sasa ataibiwa vipi naomba ufafanuzi hapo..

Kilichoibwa ni hivyo vitu sio waziri...

Teh teh teh teh
 
Kwa maoni yangu kuna tofauti kubwa ya wachimbaji wadogo wadogo kujitafuria riziki na viongozi wa juu wa Chama na Serikali kuwa wanahodhi machimbo ya madini ya aina yeyote. Leo wanaown machimbo ya Rubi kesho itakuwa machimbo ya almasi na dhahabu. Hii rasilimali ni ya Watanzania wote hivyo pato lake linastahili kuingia kwenye mfuko wa Taifa badala ya watu binafsi. Kwa maoni yangu si haki kwa watu binafsi kuown rasilimali za Watanzania (migodi ya madini) Si tulishasikia hapa kwamba Yona na Mkapa wanaown Kiwira Coal Mining? Je nani aliwapa haki ya kuown KCM? Walilipa kiasi gani na kwa nani?

Ndugu,

Viongozi nao ni raia wa nchi hii na wana HAKI ya kumiliki migodi. Madini ni rasilimali ya WATANZANIA (including hawa viongozi) wote.

Migodi ni kama biashara yoyote ile, pato lake linaingia kwenye mfuko wa Taifa kupitia KODI. Naona tunataka kwenda kwenye enzi ambayo mtu akijituma na kujitahidi kujipatia riziki yake kupitia MIGODI awe adui wa nchi.

Hao wanaolalamika hawajui hata jinsi ya kutafuta claim na kumiliki mgodi. Huo ni uvivu wa fikra...Jitumeni Wajameni.
 
Kiswahili kinakuwa tatizo hata kwa waswahili wenyewe... WAZIRI KAPUYA AIBIWA! mbona taarifa nilizonazo ni kuwa waziri Kapuya leo kapelekwa India kwa matibabu zaidi sasa ataibiwa vipi naomba ufafanuzi hapo..

Kilichoibwa ni hivyo vitu sio waziri...

Teh teh teh teh

wewe nae......mali zilizoibiwa ni za Kapuya. kwahivo basi kapuya kaibiwa!!!!!! wapi hapo ambiguity!!??? au ulitaka kutupa hizo habari kwamba kapuya kaenda udosini kwa matibabu zaidi.....si useme tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom