Waziri Kamwelwe atangaza mkakati wa kupambana na ugonjwa wa Coronavirus kwenye vyombo vya usafiri

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,744
141,609
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi a mawasiliano ameitaka mamlaka ya udhibiti usafiri wa ardhini ( Latra) kukutana mara moja na kutoa mwongozo juu ya idadi ya abiria wanaoruhusiwa kusimama ndani ya daladala na Mwendo kasi ili kupunguza msongamano.

Waziri Kamwele ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa anaelezea hatua zinazochukuliwa na wizara yake ili kujikinga na virusi vya korona.

Chanzo: ITV habari
-----

March 18, 2020

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mh.Eng. Isack Kamwelwe atoa tamko kufuatia Coronavirus Covid-19.

Tamko hilo la Waziri Isack Kamwelwe linahusu sekta ya usafiri wa barabara, reli, anga na majini linataka wenye vyombo vya usafiri na watumiaji kuchukua tahadhari kubwa kufuatia ugonjwa huo kufuatia tangazo la Wizara ya Afya kuthibitisha ugonjwa huo upo Tanzania.



  1. Kampuni za usafiri wafungue vituo zaidi vya kukatia tiketi nje ya vituo vikuu vya usafiri.
  2. Tiketi za kieletroniki ziamzishwe kupunguza msongamano.
  3. Wafanyakazi na abiri watumie sanitizier mara kwa mara kusafisha viganja vyao washikapo nauli, chenji, kushika viti n.k
  4. LATRA, TBS, na wizara ndani ya siku tatu waamue ni idadi gani ya abiria wawemo katika chombo cha usafiri ili kupunguza uwezekano wa maambukizi.
  5. TAZARA na TRC wahakikishe vifaa vya kusafisha mikono viwepo stesheni na katika treni.
  6. Mamlaka za usimamizi wa bandari na zile za viwanja vya ndege kwahakikishe kuwapo na vifaa vya kusafisha mikono n.k katika maeneo yao.
  7. Taasisi zote za usafiri zishirikiane na wizara ya Afya ili kuweza kuchapisha na kubandika matangazo yenye habari sahihi juu ya namna ya kuwa safi na pia kuzuia kusambaa ugonjwa wa Covid19 Coronavirus.

Source: Global TV online
 
Daladala zinajaza kupita kiasi, katika mazingira hayo ni rahisi ugonjwa kuenea. nashangaa kwamba leo ndo wameligundua hilo
 
Hakuna idadi yoyote ya abiria wanaouruhusiwa kusimama katika gari yoyote ya abiria,hakuna muongozo wowote unaohitajika hapo,acheni kupoteza muda.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi a mawasiliano ameitaka mamlaka ya udhibiti usafiri wa ardhini ( Latra) kukutana mara moja na kutoa mwongozo juu ya idadi ya abiria wanaoruhusiwa kusimama ndani ya daladala na Mwendo kasi ili kupunguza msongamano.

Waziri Kamwele ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa anaelezea hatua zinazochukuliwa na wizara yake ili kujikinga na virusi vya korona.

Source ITV habari

Maendeleo hayana vyama!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wataalamu wa afya wanasema TB inaambukizwa kwa njia ya hewa, na imekuwepo siku zote hapa Tz, na kila siku kuna zaidi ya watu 500 wanakufa au kuambukizwa TB hapa Tanzania na hakuna hatua zozote za kupambana na msongamano wa kwenye basi au daladala zimekuwepo ili kupunguza maambukizi ya TB.

Sasa waziri anataka kusema nini haswaa?
Corona ndio inatushinikiza hivi?
Hivi waziri anajua Corona si kitu mbele ya TB?
 
Wataalamu wa afya wanasema TB inaambukizwa kwa njia ya hewa, na imekuwepo siku zote hapa Tz, na kila siku kuna zaidi ya watu 500 wanakufa au kuambukizwa TB hapa Tanzania na hakuna hatua zozote za kupambana na msongamano wa kwenye basi au daladala zimekuwepo ili kupunguza maambukizi ya TB.

Sasa waziri anataka kusema nini haswaa?
Corona ndio inatushinikiza hivi?
Hivi waziri anajua Corona si kitu mbele ya TB?
Corona si kitu mbele ya TB?
 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi a mawasiliano ameitaka mamlaka ya udhibiti usafiri wa ardhini ( Latra) kukutana mara moja na kutoa mwongozo juu ya idadi ya abiria wanaoruhusiwa kusimama ndani ya daladala na Mwendo kasi ili kupunguza msongamano.

Waziri Kamwele ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa anaelezea hatua zinazochukuliwa na wizara yake ili kujikinga na virusi vya korona.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
FB_IMG_1584562513048.jpg
 
Back
Top Bottom