NI KWELI WIZARA YA HABARI HAINA KAZI, NA WATANZANIA HATUHIHITAJI
Kuna wanaolalamika kwamba ni kuionea CCM kudai kuwa serikali yake ni kubwa mno na viongozi hawana uwezo wa kumsimamia kila mtu.
Ingawa kuna wanaoamini kwamba ukweli ndio huo. Tanzania haihitaji wizara 30 na ushee. Na ushahidi kutokana na majibu ya Waziri wa Habari, Utamaduni na nanihino unatosha kudhihirisha ukweli huu. Ni wizara ambayo ipo ipo tu kwa ajili ya sababu za kisiasa. Kukataa sheria ya Uhuru wa Habari na kutaka kwake kuanzisha sheria/chombo cha kudhibiti vyombo vya habari ni tangazo la kumtaka Mheshimiwa Rais kuifuta wizara hiyo.
Yapo madai ambayo bado sijayathibitisha kuwa Wizara nyingi zipo ili kuipitishia CCM fedha zinazoisadia kufanya vitu vyake ili ishinde uchaguzi kila baada ya miaka mitano. Nyingi kati ya Wizara zinaweza kufanywa kama BRELA, TRA, TCRA na zikawajibika na kufanya kazi nzuri kuliko kuwa wizara zinazokula kodi ya wananchi bila ya sababu japokuwa zinamwagiwa fedha kedekede na wafadhili kama vile Wachina, Wakuba, Wajapani na Wahindi.
Waziri anabisha kwamba TBC haina mwanabodi Mwislamu hivi anamdanganya nani. Atuletee kumbukumbu za vikao vya bodi kama vitaonesha kama kuna siku hata moja huyo bwana Hassan Mitawi keshawahi kuhudhuia vikao vya bodi hiyo toka iundwe. Kwani wabunge wanadanganywa kama watoto ?
MATANGAZO mengi ya serikali, japo waziri kapiga chenga swali hili ni kweli kabisa wanapewa wanasiasa wenye magazeti na tunawajua fika. Na inakuwa hivyo ili baadaye kiasi cha fedha fulani kilicholipwa kirudi tena CCM.
Waziri anapovilaumu vyombo huru vya habari na kisha wao kuwafanyia wenye vyombo hivyo uonevu na dhuluma waziwazi juu anaona raha gani na anakijengea heshima gani chama chake ambacho baadhi ya wanachama wake ni wamiliki pia wa vyombo vya habari visivyonufaika sana na matangazo toka serikalini.
Katika miaka hii ya SIMU ZA MKONONI serikali inaweza isitoe tangazo hata moja kwenye magazeti wala redio ila kwenye SIMU ZA MKONONI tu na matangazo hayo yakawafikia Watanzania wengi zaidi kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa Rais kama unang'ang'ania kuwa na Wizara ya Habari basi chagua waziri kijana anayejua dunia ya habari na mawasiliano ya umma inakwenda wapi na sio waziri wa enzi za ujamaa anayejua tu kutetea umoja na mshikamano. Huo umoja na mshikamano wa uongo na kweli kila Mtanzania sasa hivi anajua hawezi kuufanya ugali wala maharagwe. Hawezi kuula huo umoja na mshikamano wa danganya toto, ila umoja na mshikamano huo upo ili kumla yeye. Hii hali ya kuwa na 'wajamaa' kwa maneno, lakini mabepari wa kutisha kwa vitendo hakuna anayeikubali tena. Na uanasiasa bora siku hizi mtu asikudanganye sio maneno na hotuba nzuri bali vitendo na tabia inayoendana na kile jamii inachokitarajia toka kwa viongozi waadilifu na waliopo madarakani kwa ajili ya wananchi na sio kwa ajili yao wenyewe na jamaa zao.
Na kichekesho cha mwaka ni pale inaposemwa waandishi wa habari wawezeshwe kuanzisha vyombo vyao wenyewe vya habari wakati sheria na projecti zote za waziri anazozianzisha na alizozianzisha ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anawazuria waandishi wa habari kujiunga na kuanzisha biashara zao za habari wao wenyewe. Hkuna sisi waandishi wa habari zuri tunalotegemea kutoka kwa serikalli hii au nyingine vya CCM zikiendelea kuwa na watu kama hawa ila sisi kuendelea kutumiwa tu na kisha kutupwa baada ya watu hawa kurudi tena madarakani.
Kuna wanaolalamika kwamba ni kuionea CCM kudai kuwa serikali yake ni kubwa mno na viongozi hawana uwezo wa kumsimamia kila mtu.
Ingawa kuna wanaoamini kwamba ukweli ndio huo. Tanzania haihitaji wizara 30 na ushee. Na ushahidi kutokana na majibu ya Waziri wa Habari, Utamaduni na nanihino unatosha kudhihirisha ukweli huu. Ni wizara ambayo ipo ipo tu kwa ajili ya sababu za kisiasa. Kukataa sheria ya Uhuru wa Habari na kutaka kwake kuanzisha sheria/chombo cha kudhibiti vyombo vya habari ni tangazo la kumtaka Mheshimiwa Rais kuifuta wizara hiyo.
Yapo madai ambayo bado sijayathibitisha kuwa Wizara nyingi zipo ili kuipitishia CCM fedha zinazoisadia kufanya vitu vyake ili ishinde uchaguzi kila baada ya miaka mitano. Nyingi kati ya Wizara zinaweza kufanywa kama BRELA, TRA, TCRA na zikawajibika na kufanya kazi nzuri kuliko kuwa wizara zinazokula kodi ya wananchi bila ya sababu japokuwa zinamwagiwa fedha kedekede na wafadhili kama vile Wachina, Wakuba, Wajapani na Wahindi.
Waziri anabisha kwamba TBC haina mwanabodi Mwislamu hivi anamdanganya nani. Atuletee kumbukumbu za vikao vya bodi kama vitaonesha kama kuna siku hata moja huyo bwana Hassan Mitawi keshawahi kuhudhuia vikao vya bodi hiyo toka iundwe. Kwani wabunge wanadanganywa kama watoto ?
MATANGAZO mengi ya serikali, japo waziri kapiga chenga swali hili ni kweli kabisa wanapewa wanasiasa wenye magazeti na tunawajua fika. Na inakuwa hivyo ili baadaye kiasi cha fedha fulani kilicholipwa kirudi tena CCM.
Waziri anapovilaumu vyombo huru vya habari na kisha wao kuwafanyia wenye vyombo hivyo uonevu na dhuluma waziwazi juu anaona raha gani na anakijengea heshima gani chama chake ambacho baadhi ya wanachama wake ni wamiliki pia wa vyombo vya habari visivyonufaika sana na matangazo toka serikalini.
Katika miaka hii ya SIMU ZA MKONONI serikali inaweza isitoe tangazo hata moja kwenye magazeti wala redio ila kwenye SIMU ZA MKONONI tu na matangazo hayo yakawafikia Watanzania wengi zaidi kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa Rais kama unang'ang'ania kuwa na Wizara ya Habari basi chagua waziri kijana anayejua dunia ya habari na mawasiliano ya umma inakwenda wapi na sio waziri wa enzi za ujamaa anayejua tu kutetea umoja na mshikamano. Huo umoja na mshikamano wa uongo na kweli kila Mtanzania sasa hivi anajua hawezi kuufanya ugali wala maharagwe. Hawezi kuula huo umoja na mshikamano wa danganya toto, ila umoja na mshikamano huo upo ili kumla yeye. Hii hali ya kuwa na 'wajamaa' kwa maneno, lakini mabepari wa kutisha kwa vitendo hakuna anayeikubali tena. Na uanasiasa bora siku hizi mtu asikudanganye sio maneno na hotuba nzuri bali vitendo na tabia inayoendana na kile jamii inachokitarajia toka kwa viongozi waadilifu na waliopo madarakani kwa ajili ya wananchi na sio kwa ajili yao wenyewe na jamaa zao.
Na kichekesho cha mwaka ni pale inaposemwa waandishi wa habari wawezeshwe kuanzisha vyombo vyao wenyewe vya habari wakati sheria na projecti zote za waziri anazozianzisha na alizozianzisha ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anawazuria waandishi wa habari kujiunga na kuanzisha biashara zao za habari wao wenyewe. Hkuna sisi waandishi wa habari zuri tunalotegemea kutoka kwa serikalli hii au nyingine vya CCM zikiendelea kuwa na watu kama hawa ila sisi kuendelea kutumiwa tu na kisha kutupwa baada ya watu hawa kurudi tena madarakani.