Waziri Jumaa Aweso ndiye Waziri pekee anayepigania vijana wapate ajira

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,550
44,702
Katika mawaziri wote wa Serikali ni Juma Aweso Waziri wa Maji ndiye anayesimama kidete kutetea wahitimu wa fani ndani ya Wizara yake.

Hatua ambazo ameshachukua ni pamoja na kuagiza Mkurugenzi wa RUWASA awatumie wahitimu wa Chuo Cha Maji kujenga miradi,kuisimamia na kuiendesha.

Tatizo linaloonekana na katika ngazi za chini yake watendaji wanachelewesha Mambo bila kutoa sababu Ni Nini lakini kwa kuwa Ni mwanzo mzuri Juma aweso ameendelea kushikilia msimamo wake kuwa Ni lazima hizi taasisi za kitaaluma ambazo ziko chini ya wizara mbalimbali ziangalie namna ya kuwatumia wahitimu kwenye kazi.

Natamani nisikie na mawaziri wengine wakitetea vijana wao. Suala la ajira mchakato wake unatakiwa uwe wa haraka ili kunusuru Hili janga la vijana waliojikatia tamaa.hongera Sana Waziri wa maji Juma Aweso (MB).
 
Tatizo la ajira nchini ni matokeo ya kushindwa kwa sera za ccm.Wakoloni wangekuwepo tatizo hilo lisingekuwepo.
Raslimali zote hizi eti tumeshindwa kuzigeuza pesa.
 
Hatukatai viongozi wasidokoe kidogo ila wawe wanaangalia na watu wengine sio Sasa kujilimbikizia..katika bilioni moja akipiga milioni 12 sio mbaya Sana
Hao unaowapigia debe la ajira wana mawazo wizi-wizi wa mali ya umma kama wewe?!? Kama ni hivyo , basi wabaki walipo.
 
Back
Top Bottom