Waziri Jumaa Aweso, kanisa lililojengwa bila kibali lajiunganishia maji na kuiba maji ya Tuwasa mchana kweupe

King Kisali

JF-Expert Member
Nov 20, 2019
1,042
1,349
Kama mtakumbuka mwezi mmoja au miwili iliyopita nilileta taarifa ya kanisa lililojengwa katikati ya barabara na kupiga muziki mkubwa sana masaa 24 mtaa Kariakoo kata ya Kitete.

Baada ya viongozi wa mkoa, wilaya, afisa mipango miji manispaa, mtendaji kata, mwenyekiti wa mtaa, afisa mtendaji wa mtaa kuwaendekeza kwa sababu ya rushwa wamewekwa mfukoni, sasa wameamuia kuiba maji, kujiunganishia maji bila kibali, bila kulipia wala kufuata utaratibu wowote ule, waziri wa maji, ardhi kazi kwenu huku Tabora kuna viongozi wa ajabu sana.

Ninavyoandika wapo wanaendelea na shughuli ya kujiunganishia maji mchana kweupe, Meneja amepigiwa simu anasema atafuatilia wakati watu wapo saiti sasa hivi wanafanya uhalifu, Tabora oyeeeee.
 
Kama mtakumbuka mwezi mmoja au miwili iliyopita nilileta taarifa ya kanisa lililojengwa katikati ya barabara na kupiga muziki mkubwa sana masaa 24 mtaa Kariakoo kata ya Kitete...
Kazi yako ni kuchunguza kanisa hili linafanya nini. Asante kwa ajira nzuri. Wewe unajua mamlaka zinazohusika na maji. Toa taarifa, kama rushwa nenda takukuru maana unao ushahidi wote. Hapa FB leta hoja za msingi
 
Kazi yako ni kuchunguza kanisa hili linafanya nini. Asante kwa ajira nzuri. Wewe unajua mamlaka zinazohusika na maji. Toa taarifa, kama rushwa nenda takukuru maana unao ushahidi wote. Hapa FB leta hoja za msingi
Kwahiyo ndio inaondoa ukweli kuwa kanisa uchwara limejengwa katikati ya barabara ? Ndio inaondoa ukweli kuwa wanaiba maji kujiunganishia maji bila vibali vya mamlaka husika?
 
Kazi yako ni kuchunguza kanisa hili linafanya nini. Asante kwa ajira nzuri. Wewe unajua mamlaka zinazohusika na maji. Toa taarifa, kama rushwa nenda takukuru maana unao ushahidi wote. Hapa FB leta hoja za msingi
Kuiba maji sio hoja ya msingi ? Kujenga katikati ya barabara sio hoja ya msingi ? Kujiunganishia maji bila kibali na bila kufuata utaratibu sio hoja ya msingi ? Walokole gani mnakosa hata hela ya kulipia maji mpaka muibe ?
 
jamaa anaongea utafikiri yeye ndiye mtoa vibali, unajuaje kama hawajaruhusiwa? halafu, kitu kinachopiga kelele mitaani ni kanisa tu? baa na masinagogi mengine huko huwa hayatusumbui usingizi ule wa asubuhi? acha watu waabudu jombaaa.
 
Kazi yako ni kuchunguza kanisa hili linafanya nini. Asante kwa ajira nzuri. Wewe unajua mamlaka zinazohusika na maji. Toa taarifa, kama rushwa nenda takukuru maana unao ushahidi wote. Hapa FB leta hoja za msingi
Walokole wezi sijawahi kuwaona ? Mungu wenu wa kilokole anawatuma muibe maji , muibe mpaka mchanga wa majirani hata aibu hamna mnamsalua Mungu gani anayewaruhusu kuiba ?
 
jamaa anaongea utafikiri yeye ndiye mtoa vibali, unajuaje kama hawajaruhusiwa? halafu, kitu kinachopiga kelele mitaani ni kanisa tu? baa na masinagogi mengine huko huwa hayatusumbui usingizi ule wa asubuhi? acha watu waabudu jombaaa.
Utaratibu upo na unajulikana hakuna lililo la siri, hawana kibali kuanzia kibali cha ujenzi, hawana usajili wa kanisa, hawana kibali cha muda kuendesha ibada ni genge la wahuni nchi inaendeshwa kwa taratibu ndugu .
 
Utaratibu upo na unajulikana hakuna lililo la siri ,hawana kibali kuanzia kibali cha ujenzi , hawana usajili wa kanisa , hawana kibali cha muda kuendesha ibada ni genge la wahuni nchi inaendeshwa kwa taratibu ndugu .
si ukute wewe ndiye mhuni, kama hawana unafikiri wanapata wapi ujasiri wa kuendelea na ujenzi? wewe ndiye afisa ardhi mtoa vibali? kama ndiyo basi unatakiwa utumbuliwe kwa kutowachukulia hatua na kuja kulalamika hapa, kama sio basi hauna mandate ya kubeza kwasababu wewe sio mshika majalada ya vibali vya ardhi. tuliza mshono.
 
Kama mtakumbuka mwezi mmoja au miwili iliyopita nilileta taarifa ya kanisa lililojengwa katikati ya barabara na kupiga muziki mkubwa sana masaa 24 mtaa Kariakoo kata ya Kitete...
Wewe ni muumini wa hilo kanisa?Au una kanisa lako jirani?Hio unayoita njia imewekewa Beacon/mawe ya tanroads?Sasa hivi mnapita wapi baada ya njia kufungwa? Kuna mengi sana siyaelewi.
 
Wewe ni muumini wa hilo kanisa?Au una kanisa lako jirani?Hio unayoita njia imewekewa Beacon/mawe ya tanroads?Sasa hivi mnapita wapi baada ya njia kufungwa?Kuna mengi sana siyaelewi.
huyu ni mhuni fulani tu mbabe wa mtaani asiyependa makanisa wala kuheshimu imani za watu wengine, hana ushahidi wa uhalali wa kinachoendelea.

Hana mandate kupeleka lalamiko kwa ofisi ya serikali husika, amekuja hapa kuleta umbea tu, anatakiwa kupuuzwa. kama kweli umezibwa njia hakuna mtu ambaye angekuwa amebako home hadi sasaivi angeshaenda ofisi za ardhi kushitaki zamani sana na wangeshapigwa stop.

Ukiona anakuja huku anonymous kushambulia mtu jua ni mhuni na mbeya asiye na maana.
 
Back
Top Bottom