Mtuflani Official
JF-Expert Member
- Dec 31, 2019
- 1,936
- 4,347
Jenista Mhagama ni Waziri wa Sera, Bunge na Ajira. Ila naona kama anadhani yeye ni Waziri wa Bunge pekee. Anahakikisha posho, mikopo na mishahara wanapata kwa wakati labda ndo maana wanamshangilia sana akitajwa bungeni.
Hiki kipande cha Ajira naona amekikalia kimya kabisa. Watu wengi hasahasa vijana wamo kwenye maofisi lakini wanalipwa mishahara ya dharau kabisa.
Mtu ana Masters’ analipwa Tshs. 200000. Kwenye maofisi mikataba watu hawapewi kabisa. Pesa za mifuko ya jamii hazipelekwi. Watu wengi hawajui hata kama kuna Waziri anahusika na ajira.
Hiki kipande cha Ajira naona amekikalia kimya kabisa. Watu wengi hasahasa vijana wamo kwenye maofisi lakini wanalipwa mishahara ya dharau kabisa.
Mtu ana Masters’ analipwa Tshs. 200000. Kwenye maofisi mikataba watu hawapewi kabisa. Pesa za mifuko ya jamii hazipelekwi. Watu wengi hawajui hata kama kuna Waziri anahusika na ajira.