Waziri Jafo zuia Rais Magufuli asidhalilishwe na Uhuni huu wa CCM Iringa!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,113
33,621
Kama Waziri wa nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Waziri Suleiman Jafo unayo fursa pekee ya kuzuia Rais John Magufuli kudhalilishwa na Uhuni unaofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) dhidi ya wananchi wa Iringa.

Jafo wewe ni "Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais" au kwa maana nyingine ni Waziri mdogo wakati Waziri mwenyewe akiwa ni Rais Magufuli. Inaposemwa Waziri mwenye dhamana na serikali za mitaa, huwa inamaanishwa anayetajwa ni Rais na siyo wewe.

Kwa maana nyingine mambo ya kihuni kama kumuondoa Meya wa Iringa kama ilivyo kwa yule wa Darisalama yasipochukuliwa hatua, huwa inaonekana ni kama Rais Mwenyewe ndiyo anayafurahia wakati kumbe wewe ndiyo unayepaswa kufanya maamuzi kwa wakati ili Rais asiabishwe.

Hapa Iringa Manispaa baada ya Uchaguzi wa Mwaka 2015 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilipata viti 14 vya Udiwani dhidi ya viti 4 vya udiwani vya CCM. Kwa maana nyingine kwenye Kata 18 zilizopo CCM ilikataliwa kwenye Kata 14.

Lakini hapa kwa ufupi sana nitaelezea uhuni uliofanyika kuzuia Meya kuwa Meya kinyume cha sheria na ustaarabu!!

Meya wa Iringa ameondolewa bila ya kuwa na hoja za msingi za kuondolewa kwake wala ushahidi wa kuthibitisha tuhumu alizokuwa anatuhumiwa nazo. Kimsingi Alex Kimbe kisheria bado ndiyo Meya wa Iringa Manispaa.
 
Bado ni meya wa Iringa? Si kàkubali kutoka na ofisi kakabidhi? Katika hili utaabika bure kama utalalamikia ukweli, kwa sababu wanaopiga kura kumuondoa Meya ni madiwani na si wanaCCM au wanaCHADEMA
 
Bado ni meya wa Iringa? Si kàkubali kutoka na ofisi kakabidhi? Katika hili utaabika bure kama utalalamikia ukweli, kwa sababu wanaopiga kura kumuondoa Meya ni madiwani na si wanaCCM au wanaCHADEMA
Kanuni inasemaje kura zinatakiwa ziwe ngapi ili Meya aondolewe. Ulitaka asikabidhi ili milango ifungwe kama Dar? Ulisikia alisemaje wakati anakabidhi?
 
Naamini huu uhuni una baraka zote za rais.

Kama rais angekuwa ahusiki na haya mambo ile hama hama ya washenzi kutoka chadema hangeikemea ASAP
 
Maoni ya Kamati yalilkuwa haya:
Tume ya Uchunguzi inashauri yafuatayo:-

  • Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa anatakiwa wakati wote anapotekeleza majukumu yake kuzingatia sheria, kanuni, Taratibu na kuwa na kiwango cha juu kabisa cha uadilifu kama inavyosisitizwa kwenye Kanuni ya 8 (a) (b) na Kanuni ya 9 ya Kanuni za maadili ya madiwani (Mamlaka za miji) za mwaka 2000.
  • Kutokana na kuthitibitika kwa tuhuma nyingi zinazomkabili Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mheshimiwa Alex Kimbe, Timu ya Uchunguzi inapendekeza kuwa, Halmashauri iendelee na mchakato kama inavyoelezwa kwenye kanuni namba 5 (7) ya Kanuni za kudumu za Halmashauri.
  • Upo Umuhimu kwa vyombo vingine kama vile TAKUKURU kuchunguza kwa kina mwenendo wa Mstahiki Meya Alex Kimbe hususan mali zake na namna alivyozipata ili kubaini endapo mali hizo ni halali au la na kuchukua hatua stahiki.
Haya maelezo ndiyo yaliyosababisha kura ipigwe KARLO MWILAPWA
 
Tume wala haijulikani inahusisha kina nani na inaleta taarifa isiyo na viambatanisho hata kimoja!! Yaani Tume inadai eti Kimbe aliomba rushwa ya ngono kwa maelezo kuwa ilimhoji aliyetongozwa bila ya kuonesha kama kuna meseji ama sauti iliyorekodiwa.
 
Back
Top Bottom