Waziri Jafo: Wananchi nunueni Majokofu mapya yale ya mitumba yanachafua hali ya hewa!

Waziri wa mazingira mh Jaffo amewataka wananchi kuacha kutumia majokofu ya mitumba kwani yanachafua hali ya hewa na hivyo kuharibu mazingira.

Jaffo amesema ni vema wananchi wakanunua majokofu mapya kwa ajili ya usalama wa afya zao.

Source: Upendo tv
Na hela ya kutop up wanatuongezea kwa njia ipi mobile money au Bank?
 
Badala ya kuwaambia wananchi aongee na Taasisi husika ili kuzuia kupunguza uagizwaji wa majokofu hayo, na kupunguza kodi kwenye mapya..
 
Ukweli ni kuwa used friji zilizojaa Hapa nchini Ulaya azitakiwi tena 1.zinakula sana Umeme 2.Zina Gesi Hatarishi zinazoharibu Ozone Layer....so sisi ni damping site..mbali na hizo friji pia kuna taka nyingi za kielectronic ambazo zinajaza nchi yetu bila faida bali hasara kwa mazingira yetu.
Hajui huyo, msamehe. Gas hiyo haikai kwenye mazingira. Inapaa juu na kwenda kuitafuna ozone layer, inayokinga mionzi hatari toka kwenye jua (utraviolet rays) ambayo ikitufikia huleta hatari nyingi, ikiwemo kansa ya ngozi, kuzeeka ngozi mapema, na matatizo ya macho. R12 na 22 au Freone 12 na 22 Ulaya kwa sasa zipo ni kwenye makumbusho ya maabara. R134a ndio gas inayotumika kwa sasa.
 
Mi naomba kuuliza majokofu ndio kitu gani
Mafriji mkuu , nimenunua jipya zaidi ya 1m, haya yazamani yanamaliza sana umeme wa LUKU .
Lakini wangapi wanaweza kununua mpya.

Mwaka wa sita huu hawatoi ajira.

Mazingira hayawezi kutunzwa na yakapendeza kwenye ufukara na maisha duni kama Tanzania.

Tunaposema CCM wameshindwa wapishe hii ndio maana yake.
Huko vijijini watu wanakata tu miti hovyo kutengeza mikaa wanafukuza mvua, tafuteni mbadala wa mkaa. Hii nchi ipo kwenye hali mbaya kimazingira.
 
Ni kweli kabisa, lakini kosa si la wanunuzi kosa ni wale wanaoruhusu bidhaa zisizo na ubora kuingizwa nchini.
Hata hivyo Waziri wa Mazingira anao wajibu wa kusaidia walau kwa kupiga marufuku uingizwaji wa bidhaa zinazochafua mazingira.
 
Mafriji mkuu , nimenunua jipya zaidi ya 1m, haya yazamani yanamaliza sana umeme wa LUKU .
Lakini wangapi wanaweza kununua mpya.

Mwaka wa sita huu hawatoi ajira.

Mazingira hayawezi kutunzwa na yakapendeza kwenye ufukara na maisha duni kama Tanzania.

Tunaposema CCM wameshindwa wapishe hii ndio maana yake.
Huko vijijini watu wanakata tu miti hovyo kutengeza mikaa wanafukuza mvua, tafuteni mbadala wa mkaa. Hii nchi ipo kwenye hali mbaya kimazingira.
Kulea miti halihitaji utafiti. Kupika ni lazima. Serikali inakamata wauza mkaa bila kuweka mbadala ya nishati mbadala. Serikali ikiondoa kodi kwenye gas, majiko na vifaa vyake, ikashusha bei ya umeme majumbani, hakuna atakae pikia mkaa. Miaka 10 baadae mbao zitakosa wanunuzi na tuta export na kupata hela za kigeni. Serikali kubariki kuongeza bei ya gas na umeme ni uendawazimu.
 
Ni kweli kabisa, lakini kosa si la wanunuzi kosa ni wale wanaoruhusu bidhaa zisizo na ubora kuingizwa nchini.
Hata hivyo Waziri wa Mazingira anao wajibu wa kusaidia walau kwa kupiga marufuku uingizwaji wa bidhaa zinazochafua mazingira.
Waziri anakumbuka shula majogoo.
 
Huoni kama wewe ndo kilaza aisee,au hujui CFCs toka ktk mafridge/AC ndo zinachangia KWA kiasi kikubwa kuharbu ozone?

Hebu piga shule kwanza Kisha ndo ujibu thread za kitaaluma
Kinachowafanya wasikataze hizo friji za mtumba ni nini??? Tatizo umekurupuka kunijibu, lengo langu sio kukataa uhabiribifu unaotokana na hizo friji... Kwanini wao wasichukue hatua kama mamlaka??? Kwanini wasiongeze kodi kwenye za mtumba na waounguze kwenye friji mpya ili kutimiza hiyo azma yake badala ya kupayuka tu watu wasinunue kitu ambacho ni ngumu kutekelezeka???
 
Hajui huyo, msamehe. Gas hiyo haikai kwenye mazingira. Inapaa juu na kwenda kuitafuna ozone layer, inayokinga mionzi hatari toka kwenye jua (utraviolet rays) ambayo ikitufikia huleta hatari nyingi, ikiwemo kansa ya ngozi, kuzeeka ngozi mapema, na matatizo ya macho. R12 na 22 au Freone 12 na 22 Ulaya kwa sasa zipo ni kwenye makumbusho ya maabara. R134a ndio gas inayotumika kwa sasa.
R134 na yenyewe wameacha kuitumia kwenye latest fridge. Fridge latest ya mtumba inatumia R600 siku hizi

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Ukiangalia matatizo meengi wanayowatesa hawa viongozi yametokana na jamii kuwa masikini....Competancy huwezi kuipata kama watu wako wengi ni masikini, hivi vitu vibovu vinakuja kwa kuwa huku ndio dampo wanakoishi waokota makopo ndio sisi sasa...umasikini huleta incompetency maana mtu mwenye njaa hawezi kufikiri wala kusoma vizuri...Vijana wetu wengi vyuo vikuu wanasoma wakitokea kwenye umasiki na wanasoma pia wakiwa na njaa..unaanzaje kuelewa hapo?
Waambie wawaambie na wake zao wanaofanya biashara ya mitumba waache!
 
Waziri wa mazingira mh Jaffo amewataka wananchi kuacha kutumia majokofu ya mitumba kwani yanachafua hali ya hewa na hivyo kuharibu mazingira.

Jaffo amesema ni vema wananchi wakanunua majokofu mapya kwa ajili ya usalama wa afya zao.

Source: Upendo tv

======

Na Ramadhan Hassan, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Seleman Jafo amewataka watanzania kutunza mazingira ikiwa ni pamoja na kununua bidhaa rafiki wa Ozoni (Ozone friendly) ili kulinda tabaka la Ozoni dhidi ya uharibifu.

Waziri Jafo amesema hayo jijini Dodoma Septamba 16, 2021 alipofanya ziara kwenye maduka ya vifaa vya umeme pamoja na mafundi wanaojishughulisha na uuzaji na utengenezaji wa majokofu na viyoyozi katika maadhimisho yakupambana na kulilinda anga la hewa (Ozone layer).

Amesema ozoni ni tabaka la hewa ambalo liko katika anga la juu la pili lifahamikalo kitaalamu kama Stratosphere ambalo linaweka aina ya tabaka ama tambara angani ambalo linazuia mionzi mikali ya jua inayoweza kuleta athari katika afya za binadamu na viumbe hai kuja moja kwa moja duniani.

Amesema kuwa uharibifu wa tabaka la Ozoni unapelekea madhara mbalimbali duniani ikiwemo kuongezeka kwa kiwango cha joto duniani pamoja na kuleta mabadiliko ya tabia ya nchi jambo ambalo ni hatari kwa afya ya binadamu na viumbe hai.

Amewataka Wafanyabiashara kuacha kuuza Majokofu na Viyoyozi vya mtumba kwani vimeonekana kuleta athari kubwa katika vizazi vyetu vya sasa na vijavyo, wafanyabishara wengi wamekuwa wakiuza majokofu ya mtumba yalikuwa yakitumia gesi R 22 ambayo yalikuwa ikiharibu mazingira.

Jafo ametoa wito kwa vijana ambao wanaojishughulisha na masuala ya ufundi wa viyoyozi kwenye Majokofu ya mtumba kutumia aina ya gesi inayoruhusiwa na viwango vya kimataifa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Remidius Mwema ambaye alimwakilisha , Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amesema Dodoma inakuwa kwa kasi hivyo kuna haja ya kutengeneza jukwaa la pamoja litakalosaidia kutoa elimu kwa wananchi.

“Ni kweli wananchi wamekuwa wakinunua Majokofu ya mtumba ambayo yameonekana kuwa na madhara na hiyo yote inatokana na kutokuwa na uelewa juu ya madhara hayo lakini sasa kama tutakuwa na jukwaa la pamoja la kutoa elimu juu ya madhara ya bidhaa hizi za mtumba ninaimani bidhaa hizo za mtumba hazitanunuliwa,” amesema Mwema.

Naye, Fundi anayejishughulisha na Ufundi wa Viyoyozi Matukuta Juma amesema kutokana na ushauri huo watahamasisha wengine kutumia mitungi ya gesi inayokubalika huku akitumia fursa hiyo kuiomba Serikali kuwapunguzia gesi ambayo haiharibu mazingira kwani inauwza bei ya juu.

Chanzo: Mtanzania Digital
Vipi anasemaje kuhusu nguo za mitumba na magari ya mitumba kuhusu kuchafua mazingira na.hewa ya ukaa. Tuba.wanasiasa mamburulaz kweli kweli. Shibe mwanamalevya

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Mafriji mkuu , nimenunua jipya zaidi ya 1m, haya yazamani yanamaliza sana umeme wa LUKU .
Lakini wangapi wanaweza kununua mpya.

Mwaka wa sita huu hawatoi ajira.

Mazingira hayawezi kutunzwa na yakapendeza kwenye ufukara na maisha duni kama Tanzania.

Tunaposema CCM wameshindwa wapishe hii ndio maana yake.
Huko vijijini watu wanakata tu miti hovyo kutengeza mikaa wanafukuza mvua, tafuteni mbadala wa mkaa. Hii nchi ipo kwenye hali mbaya kimazingira.
Asante mkuu, mi ndio Mara ya kwanza kushika neno majokofu ila leo nimejifunza,Asante
 
Back
Top Bottom