Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Wakala wa Majengo Tanzania ( TBA) wametakiwa kurejesha Shilingi million 300 walizolipwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya Serikali katika Halmashauri ya Buchosa mkoani Mwanza, huku Halmashauri hiyo ikipigwa marufuku kuwapa kazi TBA.
Akizungumza wakati wa ziara yake wilayani humo juzi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI), Seleman Jafo alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuwaandikia barua ya kuwataka warejeshe fedha hizo ili zitumike kwenye majukumu mengine.
" Nilitamani ujenzi huu uwe umeisha lakini siyo sababu yenu ni sababu ya mtu mliyempa kazi msiwape tena kazi za huku ndani unapowalipa wanaenda kufanya kazi sehemu nyingine maeneo ya mjini wanafanya kazi sana ili kusifiwa na viongozi lakini huku ndani hawafanyi vizuri kabisa Mkurugenzi waandikie barua tena zile fedha zirudi zifanye mambo mengine" alieleza Jafo.
Akizungumzia suala la ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hiyo alisema hawafanyi vizuri hivyo waongeze juhudi katika kukusanya kwani mpaka sasa wanaokusanya kwa asilimia 29, ukusanyaji wa mapato ndio kipimo cha Wakurugenzi kwa watakaoshindwa hawatakuwa na sifa.
" Ofisa mipango ,idara ya fedha imani yangu mtafanya vizuri katika hili na ofisi ya Mkurugenzi ninachowaomba mdumishe mahusiano pia wakuu wa idara fanyeni kazi vizuri na watu wa chini na mfanye kwa mahusiano mazuri na mpendane ili mfanye kazi na kuacha maigizo nataka watu wafanyakazi kwa amani msiwaonee watu" alisema Jafo.
Pia Waziri alisifia ujenzi wa hospital na jengo la Halmashauri nakusema kuwa wanafanya vizuri na kuwa halmashauri inayokuja kwa kasi na kuzitaka halmashauri zote nchini kuiga mfano wake.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo hilo Erick Shigongo alisema matatizo yanayomkosesha usingizi ni ubovu wa barabara, huduma za afya na miundombinu ya madarasa hivyo aliiomba Waziri Jafo kuliangalia hilo
" Nafarijika umetusifia uliposema mmejitahidi roho yangu imefarijika, shida kubwa ni barabara siku ikiondolewa tutalala simu nyingi nazozipokea kwa wananchi wangu ni hiyo ombi langu kwa watumishi tuchape kazi kwa nguvu ili kuonyesha Buchosa tunania ya kuleta maendeleo na kuipeleka Buchosa mbele" alieleza Shigongo.
Akizungumza wakati wa ziara yake wilayani humo juzi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI), Seleman Jafo alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuwaandikia barua ya kuwataka warejeshe fedha hizo ili zitumike kwenye majukumu mengine.
" Nilitamani ujenzi huu uwe umeisha lakini siyo sababu yenu ni sababu ya mtu mliyempa kazi msiwape tena kazi za huku ndani unapowalipa wanaenda kufanya kazi sehemu nyingine maeneo ya mjini wanafanya kazi sana ili kusifiwa na viongozi lakini huku ndani hawafanyi vizuri kabisa Mkurugenzi waandikie barua tena zile fedha zirudi zifanye mambo mengine" alieleza Jafo.
Akizungumzia suala la ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hiyo alisema hawafanyi vizuri hivyo waongeze juhudi katika kukusanya kwani mpaka sasa wanaokusanya kwa asilimia 29, ukusanyaji wa mapato ndio kipimo cha Wakurugenzi kwa watakaoshindwa hawatakuwa na sifa.
" Ofisa mipango ,idara ya fedha imani yangu mtafanya vizuri katika hili na ofisi ya Mkurugenzi ninachowaomba mdumishe mahusiano pia wakuu wa idara fanyeni kazi vizuri na watu wa chini na mfanye kwa mahusiano mazuri na mpendane ili mfanye kazi na kuacha maigizo nataka watu wafanyakazi kwa amani msiwaonee watu" alisema Jafo.
Pia Waziri alisifia ujenzi wa hospital na jengo la Halmashauri nakusema kuwa wanafanya vizuri na kuwa halmashauri inayokuja kwa kasi na kuzitaka halmashauri zote nchini kuiga mfano wake.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo hilo Erick Shigongo alisema matatizo yanayomkosesha usingizi ni ubovu wa barabara, huduma za afya na miundombinu ya madarasa hivyo aliiomba Waziri Jafo kuliangalia hilo
" Nafarijika umetusifia uliposema mmejitahidi roho yangu imefarijika, shida kubwa ni barabara siku ikiondolewa tutalala simu nyingi nazozipokea kwa wananchi wangu ni hiyo ombi langu kwa watumishi tuchape kazi kwa nguvu ili kuonyesha Buchosa tunania ya kuleta maendeleo na kuipeleka Buchosa mbele" alieleza Shigongo.