Waziri Jafo umekosea kulazimisha watu wenye taaluma kufanya kazi za propaganda

seedfarm

JF-Expert Member
Feb 9, 2020
260
2,654
Members,

Siri aliyoitoa Selemani Jafo huko Arusha inafikirisha sana na kutoa picha halisi ya Chama cha Mapinduzi.

Mosi, kumbe watu wanakusanywa na kulazimishwa wajitokeze waonekane wengi wakati wa uzinduzi wa miradi na kampeni za CCM.

Hili jambo la kukusanya watu wasiojielewa kama mifugo ili waje kupiga makofi uzinduzi wa barabara ya lami halina afya hata kidogo kwa mustakabali wa taifa.

Leo hii watu wengi wanafahamu ni kazi ya serikali kuweka lami na kujenga miundombinu, hili sio ombi ni lazima kwa kuwa wanatuumiza kwenye kodi.

Jambo baya zaidi unalazimisha watumishi wenye taaluma zao wakakusanye watu ili waje kukushangilia wewe na barabara ya lami

Pili, watendaji wenye taaluma zao mfano engineers, waganga wakuu wa hospital za wilaya na afya na wengine wanalazimishwa kujiingiza kwenye siasa kwa nguvu ili kusifu na kupiga makofi. Nini kosa la yule mtendaji wa serikali?

Je, yule mtendaji anayelazimishwa kukusanya watu Arusha na Selemani Jafo alipewa pesa za mafuta na vipaza sauti ili ashawishi wananchi kuja kushangilia barabara ya lami.

Kwa hili Jafo kubali umekosea na omba msamaha watu watakusamehe, kubali umeteleza.

Yule mtumishi anayesimamia barabara Arusha hukutaka kumsikiliza uliona hoja zake zina mashiko. Ulikuwa na hasira na frustration zako na mihemko isiyokuwa na maana kama Waziri.

Selemani Jafo ukiwa na hasira jaribu kunywa maji mengi na kutulia kwanza. Ulevi wa madaraka ulioonyesha kwa mtumishi Arusha mwenye taaluma yake kumlazimisha akaswage watu kama mifugo halikubariki kabisa.

Propaganda fanyeni nyie wanasiasa. CCM Arusha ilikuwa wapi kukusanya hao watu waje kukushangilia wewe na barabara ya lami.

Je, Arusha hakuna katibu wa chama cha mapinduzi au Mwenyekiti wa CCM Arusha.

Umetumia madaraka yako vibaya sana. Watu walikuamini lakini sasa wanapata picha yako halisi kuwa wewe ni katili, mpenda sifa na usiyetaka kusikiliza hoja za watumishi wa umma.

Yule mtumishi aliyesimamia barabara Arusha kama engineer ulipasa kumsifu na kumpa hongera yake. Kitendo cha kumlazimisha engineer akatafute watu waje kukupigia makofi wewe na barabara ya lami ni aibu kubwa. Hata bosi wako hawezi kukubaliana na ulichokifanya Arusha kumuondoa mtumishi wa uma kisa hajatafuta watu wa kukupigia makofi wewe na kupigia makofi barabara ya lami.
 
Kabisa kwa uzoefu wangu wa kufanya kazi kwenye halmashauri wanaotakiwa kuhamasisha watu kuhudhuria maujinga kama anayotaka Jafo Ni Mwenyekiti wa Mtaa na mtendaji wake wa eneo husika, diwani na mtendaji wa kata, DED na DC wa eneo husika.

Meneja wa Tarura kwa namna yeyote hausiki kabisa na kuhamasisha wananchi. Jafo nimemuona kilaza sana kwenye hii ishu.

Kuna maeneo watu hawahamasiki DED analazimika kuwalazimisha watumishi, hususani walimu na manesi hata wanafunzi kuhudhuria tukio just kuonesha wananchi ni wengi kumbe ni magumashi.
 
Ndio maana mwana taaluma ukiomba kazi kwenye usaili watataka kuona how flexible you are! Hao kina Pompeo ni mabobezi kwenye taaluma zao,lakin inabidi waende sambamba na Trump.

Kama unaona huwezi fuata maelekezo ya mkubwa wa kazi, acha tu kazi. Tarura kazi kubwa ni kusimamia barabara za wilaya ambazo zinawagusa wananchi wapiga kura.

Kwa kipindi hiki cha uchaguzi. Hakuna serikali ilio tayari kuwakosa wapiga kura,kwenye eneo gumu kama Arusha,kisa tu wewe ni mwana taaluma.
 
Ndio maana mwana taaluma ukiomba kazi kwenye usaili watataka kuona how flexible you are! Hao kina Pompeo ni mabobezi kwenye taaluma zao,lakin inabidi waende sambamba na Trump.

Kama unaona huwezi fuata maelekezo ya mkubwa wa kazi,acha tu kazi. Tarura kazi kubwa ni kusimamia barabara za wilaya ambazo zinawagusa wananchi wapiga kura.

Kwa kipindi hiki cha uchaguzi,hakuna serikali ilio tayari kuwakosa wapiga kura,kwenye eneo gumu kama Arusha,kisa tu wewe ni mwana taaluma.
Ficha upumbavu wako ndugu? Ni wapi kwenye majukumu ya meneja wa tarula ameambiwa majukumu yake ni kukusanya wananchi kwenye uzinduzi?

Alafu barabara kuzinduliwa bila wananchi ndo subotage? Kwani wananchi Hawaioni? Hawaitumii?

Alafu pale kulikuwa na waandishi wa habari ambao jukumu Lao ni kuhabarisha umma tena kwa uwepo wao tu habari ya ile barabara imeenda mbali zaidi ya Arusha! Je ni sahihi kutumia sababu za kipumbavu namna ile kumuonea mtumishi yule? Au kwa kuwa hana mtetezi?

CCM mmezidi kuwa wajinga na primitive sana. Yaani mtakachokipata mwaka huu hamtasahau nawaambia
 
Ndio maana mwana taaluma ukiomba kazi kwenye usaili watataka kuona how flexible you are! Hao kina Pompeo ni mabobezi kwenye taaluma zao,lakin inabidi waende sambamba na Trump.

Kama unaona huwezi fuata maelekezo ya mkubwa wa kazi, acha tu kazi. Tarura kazi kubwa ni kusimamia barabara za wilaya ambazo zinawagusa wananchi wapiga kura.

Kwa kipindi hiki cha uchaguzi,hakuna serikali ilio tayari kuwakosa wapiga kura,kwenye eneo gumu kama Arusha,kisa tu wewe ni mwana taaluma.
Wewe Jafo, acha kutetea ujinga ulioufanya. Ona mfano wako wa Pompeo, kwani Pompeo cheo chake cha Sasa ni cha kisiasa ama Cha kitaaluma?
 
Ficha upumbavu wako ndugu? Ni wapi kwenye majukumu ya meneja wa tarula ameambiwa majukumu yake ni kukusanya wananchi kwenye uzinduzi?
Umeuona mkataba wake wa kazi? Umeomba kazi serikalini,na serikali yenyewe ni hii ya ccm unategemea nini?kama hawezi kuendana na kasi yetu ajiuzulu wapo vijana wengi sana wana elimu nzuri tu wanaweza kuchukua nafasi
 
Members, Siri aliyoitoa Selemani Jaffo huko Arusha inafikirisha sana na kutoa picha halisi ya chama cha mapinduzi
...
Hili jambo la kukusanya watu wasiojielewa kama mifugo ili waje kupiga makofi uzinduzi wa barabara ya lami halina afya hata kidogo kwa mustakabali wa Taifa.

Leo hii watu wengi wanafahamu ni kazi ya serikali kuweka lami na kujenga miundombinu, hili sio ombi ni lazima kwa kuwa wanatuumiza kwenye kodi
Kweli ni jambo la kufikirisha kwa wafuasi wa viongozi wa upinzani, hasa humu JF, kila kukicha huja na hoja zilezile za viongozi wao wanaotafuta umaarufu wa kisiasa kwa kuipinga Serikali pasipo kuwa na hoja.

Hoja ya kwamba ni kazi ya serikali kuweka lami na kujenga miundombinu ni ya kitoto kabisa.

Serikali ipingwe/ikosolowe pale inaposhindwa kutimiza wajibu wake huo na si vinginevyo. Viongozi wa upinzani wanapoipinga badala ya kuipongeza wanajiweka mbali na wananchi ambao hatimaye wanaona na kufaidi matunda ya kodi zao. Kuwaita watu wasiojielewa ni matusi ya nguoni yanayoweza kutolewa tu na Mpumbavu.
 
Umeuona mkataba wake wa kazi?
Umeomba kazi serikalini,na serikali yenyewe ni hii ya ccm unategemea nini?kama hawezi kuendana na kasi yetu ajiuzulu wapo vijana wengi sana wana elimu nzuri tu wanaweza kuchukua nafasi
Mikataba ya utumishi wa umma ni standard. Hakuna mtu mkataba wenye kipengele cha kukusanya wananchi kwenye uzinduzi.

Kwa iyo unamaanisha kasi ya CCM saivi ni kuonea watumishi wa umma??? Sawasawa mmesomeka vizuri, tunazidi kuweka kumbukumbu sawa. Sijui nani atawabeba mwaka huu.
 
Mikataba ya utumishi wa umma ni standard. Hakuna mtu mkataba wenye kipengele cha kukusanya wananchi kwenye uzinduzi.
Kuna kipengele kinasema utafanya na kazi ingine ambayo utapangiwa na mwajiri wako,hicho kipo mpaka China utakikuta
Waliokitunga si wajinga,ndio maana wengine tumeamua kujiajiri tu
 
Members,Siri aliyoitoa Selemani Jaffo huko Arusha inafikirisha sana na kutoa picha halisi ya chama cha mapinduzi

Mosi,Kumbe watu wanakusanywa na kulazimishwa wajitokeze waonekane wengi wakati wa uzinduzi wa miradi na kampeni za ccm
Hili jambo la kukusanya watu wasiojielewa kama mifugo ili waje kupiga makofi uzinduzi wa barabara ya lami halina afya hata kidogo kwa mustakabali wa Taifa
Leo hii watu wengi wanafahamu ni kazi ya serikali kuweka lami na kujenga miundombinu ,hili sio ombi ni lazima kwa kuwa wanatuumiza kwenye kodi
Jambo baya zaidi unalazimisha watumishi wenye taaluma zao wakakusanye watu ili waje kukushangilia wewe na barabara ya lami

Pili,Watendaji wenye taaluma zao mfano engineers,Waganga wakuu wa hospital za wilaya na afya na wengine wanalazimishwa kujiingiza kwenye siasa kwa nguvu ili kusifu na kupiga makofi,Nini kosa la yule mtendaji wa serikali
Je?Yule mtendaji anayelazimishwa kukusanya watu Arusha na Selemani Jaffo alipewa pesa za mafuta na vipaza sauti ili ashawishi wananchi kuja kushangilia barabara ya lami

Kwa hili Jaffo kubali umekosea na omba msamaha watu watakusamehe,Kubali umeteleza

Yule mtumishi anayesimamia barabara Arusha hukutaka kumsikiliza uliona hoja zake zina mashiko ,Ulikuwa na hasira na frustration zako na mihemko isiyokuwa na maana kama Waziri

Selemani Jaffo ukiwa na hasira jaribu kunywa maji mengi na kutulia kwanza ,Ulevi wa madaraka ulioonyesha kwa mtumishi Arusha mwenye taaluma yake kumlazimisha akaswage watu kama mifugo halikubariki kabisa

Propaganda fanyeni nyie wana siasa,ccm Arusha ilikuwa wapi kukusanya hao watu waje kukushangilia wewe na barabara ya lami

Je Arusha hakuna katibu wa chama cha mapinduzi au Mwenyekiti wa ccm Arusha

Umetumia madaraka yako vibaya sana ,Watu walikuamini lakini sasa wanapata picha yako halisi kuwa wewe ni katili ,mpenda sifa na usiyetaka kusikiliza hoja za watumishi wa uma

Yule mtumishi aliyesimamia barabara Arusha kama engineer ulipasa kumsifu na kumpa hongera yake,Kitendo cha kumlazimisha engineer akatafute watu waje kukupigia makofi wewe na barabara ya lami ni aibu kubwa,Hata bosi wako hawezi kukubaliana na ulichokifanya Arusha kumuondoa mtumishi wa uma kisa hajatafuta watu wa kukupigia makofi wewe na kupigia makofi barabara ya lami

Kuunga juhudi lazima uwe na akili kama za mwendawazimu.
 
Back
Top Bottom