Waziri Jaffo: Mwezi April 2020 nitamkabidhi Rais Magufuli orodha ya Wakurugenzi wavivu

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,550
Waziri wa nchi Tamisemi, Seleman Jafo amesema ana majina ya wakurugenzi wasiokwenda na kasi ya utendaji kazi wa Serikali ya Tanzania, atayakabidhi kwa Rais John Magufuli Aprili, 2020.

Jafo ameeleza hayo leo Jumatano Januari 22, 2020 mjini Dodoma wakati akikabidhi mashine 7227 za kukusanyia mapato kwa halmashauri zote. Mashine hizo imetolewa na balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen.

Waziri huyo amesema ameshindwa kuzivumilia baadhi ya halmashauri kwa kuwa zinatekeleza majukumu yake kinyume na miongozo ya Serikali, ikiwa ni pamoja na kutokusanya fedha ipasavyo.

"Wiki ijayo nitatoa taarifa ya makusanyo yote kwa halmashauri, lakini taarifa yangu ya mwezi Aprili nitaorodhesha majina na kumkabidhi mwenye mamlaka, nitatoa mapendekezo ikibidi wakurugenzi waachiwe maana hawatufai," amesema Jafo.

Amebainisha kuwa kuna halmashauri zinadaiwa madeni makubwa, zikiwemo posho za madiwani, “kuna halmashauri inadaiwa Sh758 bilioni ambazo ni malimbikizo ya posho za wabunge, mkurugenzi wake anapaswa kujitathimi.”

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri wa nchi Tamisemi, Seleman Jafo amesema ana majina ya wakurugenzi wasiokwenda na kasi ya utendaji kazi wa Serikali ya Tanzania, atayakabidhi kwa Rais John Magufuli Aprili, 2020.

Jafo ameeleza hayo leo Jumatano Januari 22, 2020 mjini Dodoma wakati akikabidhi mashine 7227 za kukusanyia mapato kwa halmashauri zote.

Mashine hizo imetolewa na balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen.

Waziri huyo amesema ameshindwa kuzivumilia baadhi ya halmashauri kwa kuwa zinatekeleza majukumu yake kinyume na miongozo ya Serikali, ikiwa ni pamoja na kutokusanya fedha ipasavyo.

"Wiki ijayo nitatoa taarifa ya makusanyo yote kwa halmashauri, lakini taarifa yangu ya mwezi Aprili nitaorodhesha majina na kumkabidhi mwenye mamlaka, nitatoa mapendekezo ikibidi wakurugenzi waachiwe maana hawatufai," amesema Jafo.

Amebainisha kuwa kuna halmashauri zinadaiwa madeni makubwa, zikiwemo posho za madiwani, “kuna halmashauri inadaiwa Sh758 bilioni ambazo ni malimbikizo ya posho za wabunge, mkurugenzi wake anapaswa kujitathimi.”


Chanzo: Mwananchi
 
Na wale wanaodaiwa madawai ya rikizo matibabu ha uhamisho wa walimu tunaweka kundi gani?
Watakuwa wakurugenzi goigoi
 
Waziri wa nchi Tamisemi, Seleman Jafo amesema ana majina ya wakurugenzi wasiokwenda na kasi ya utendaji kazi wa Serikali ya Tanzania, atayakabidhi kwa Rais John Magufuli Aprili, 2020.

Jafo ameeleza hayo leo Jumatano Januari 22, 2020 mjini Dodoma wakati akikabidhi mashine 7227 za kukusanyia mapato kwa halmashauri zote. Mashine hizo imetolewa na balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen.

Waziri huyo amesema ameshindwa kuzivumilia baadhi ya halmashauri kwa kuwa zinatekeleza majukumu yake kinyume na miongozo ya Serikali, ikiwa ni pamoja na kutokusanya fedha ipasavyo.

"Wiki ijayo nitatoa taarifa ya makusanyo yote kwa halmashauri, lakini taarifa yangu ya mwezi Aprili nitaorodhesha majina na kumkabidhi mwenye mamlaka, nitatoa mapendekezo ikibidi wakurugenzi waachiwe maana hawatufai," amesema Jafo.

Amebainisha kuwa kuna halmashauri zinadaiwa madeni makubwa, zikiwemo posho za madiwani, “kuna halmashauri inadaiwa Sh758 bilioni ambazo ni malimbikizo ya posho za wabunge, mkurugenzi wake anapaswa kujitathimi.”

Sent using Jamii Forums mobile app
Jaffo sijui anafeli wapi?.......kuna wanafunzi bado wanakaa chini katika karne hii!
 
Aanze na jina lake, kwani ni uvivu wa hali ya juu kwamba list anayotayari lakini itamfikia raisi mwezi wa nne, si watakua wameshatuhujumu vyakutosha ao wanaotumwa na mabeberu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom