Waziri huyu hafai

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,832
2,790
Bila shaka sasa kuna haja pamoja na mambo mengine ya kisiasa pia tuwawajibishe mawaziri wetu kupitia JF hasa katika Thread hii ya "Waziri huyu hafai" Nimebuni blog hii si kwa nia ya kuwakomoa mawaziri watakao chomoka kwa ajili ya kujadiliwa kuhusu kutokufaa kwao bali pia ni kuwakumbusha kwamba wamefikia mstari mwekundu kwa hiyo watahitaji kupata usimamizi maalumu na wahusika wao. Chukulia mathalani mtoto mchanga anatakiwa kuhudhuria kliniki kila mwezi ambapo hupimwa uzito na mambo mengine na huwekwa alama ya uzito wake yule atakaye over weight itaonyeshwa pia itafika mahali ikizidi mhusika ataelekezwa hatua za kuchukua na kama mtoto ata under weight vivyo hivyo. Mawaziri watachunguzwa mali zao bila kujua na jinsi walivyozipata na huku katika JF tutatoa tathmini kwamba hapa hii ni obesity anatakiwa kupunguza uzito ama la. Lakini pia kuna mawaziri wazuri sana ambao kweli wanaipenda nchi hii wao huenda hata majina yao yasionekane humu JF. Lengo kuu ni kuwasafisha ili tubaki na Tanzania yetu ikiwa safi.
 
Wa tano ni basil P. Mramba

Na wa sita ni Kingunge
Nasema kingunge kwa maana ya kwamba huyu jamaa amekuwa waziri toka enzi ya Nyerere, ni kikongwe pekee aliyebaki ndani ya Govt, ni heri basi angekuwa na Busara lakini hakuna ni politics tu.

Huyu jamaa hana msimamo kabisa, enzi za nyerere alisimamia siasa za ujamaa kumliko hata Mwalimu, tukajua huyu ni mjamaa kweli kweli, Akaja Mwinyi, hatukusikia hata siku moja akipingana na mwinyi kama ilivyokuwa kwa mwalimu JK Nyerere, akaja Mkapa na sera za ubinafsiji na uwazi na Ukweli,NBC, TCC etc wameuza, yeye kimya, Kaingia JK naye yu mstari wa mbele kwa usanii badala ya kukemea. Huyu mtu yupo kwa maslahi yake tu na ndiyo maana sasa hivi ni bepari mkubwa.

Salim, Ng'wandu, kahama wamestaafu yeye yumo tu, hata kama unateuliwa si useme mi basi. Huyu hatufai, hana msimamo ni BENDELA FUATA UPEPO, leo akija mwingine na hili na yeye yumo.
 
Mramba, Karamagi, Meghji, Peter Msola, Kingunge bin Kingwendu
 
mhe. hawa ghasia.
amekuwa ni mshauri mbovu kwa muungwana kuhusu maslahi ya wafanyakazi wa serikali,
 
Salim, Ng'wandu, kahama wamestaafu yeye yumo tu, hata kama unateuliwa si useme mi basi. Huyu hatufai, hana msimamo ni BENDELA FUATA UPEPO, leo akija mwingine na hili na yeye yumo.

..ukiona yeye bado yupo,ujue bado anahitajika!

..ingekuwa hana kazi,asingewekwa tena wakati mwingine kwa kupewa ofisi isiyo na majukumu maalum!

..kwa maana hiyo,jukumu lake ni maalum!ndo maana serikali zote hizo ame-serve!

..miye silijui hilo jukumu lake!ila nadhani ni maalum!
 
mawaziri wote wanaohusu ajira na vijana!
mhe nchimbi ni msanii tu
 
mungu anazidi kunipa majina ya mawaziri wanaotuibia..
mhe msabaha
anahusika moja kwa moja na dili la richmond,hata JK Anafahamu hili coz wakati muungwana anatembelea pale ubungo alimuulizia 'dk msabaha nasikia hii kampuni ni yako,lini mtamaliza kutoa umeme?
msabaha alishtuka na hakujibu..
mtu wa 14 ni mhe masha,
huyu amekuwa mtu wa kupenda kujipatia ukwasi wa haraka katika kipindi alipokuwa pale MINERAL,
ni watu ambao wanalindwa na ndanda kosovo
 
Meghji hana uwezo wa kusimamia hiyo ministry of finance,she doesnt have any dynamic monetary policy ya kutusukuma mbele,dont know hata kama anajua anachofanya zaidi ya kusoma libajeti fake bungeni kila mwaka...she should go
 
Andrea Chenge (kutumia ofisi vibaya, mikataba yote kipindi cha Mkapa ilipitia kwake kama mwanasheria mkuu)
 
Meghji hana uwezo wa kusimamia hiyo ministry of finance,she doesnt have any dynamic monetary policy ya kutusukuma mbele,dont know hata kama anajua anachofanya zaidi ya kusoma libajeti fake bungeni kila mwaka...she should go

Kila nikiangalia change iliyotokea kwenye bajeti ya mwaka huu nazidi kuwa convinced huyu mama anajua anachokifanya.
Leo $1 iko 1210 TShs
Nimejaribu kulinganisha bajeti ya mwaka jana na mwaka huu na nimeconclude kwamba we are on right track...
 
SAWA MNAPENDEKEZA HAO MLIOWATAJA WAONDOLEWE,SASA MNATAKA NANI AINGIZWE KUJAZA NAFASI ZAO?

Mimi waziri ambaye naona atoke ni wa usarama wa raia ,mwapachu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom