falcon mombasa
JF-Expert Member
- Mar 5, 2015
- 9,159
- 9,241
Mwaka jana akiwa Waziri wa Afya uliagiza James Delicious, Dani mtoto wa mama, Kaoge na kadhalika wakamatwe kwa kujihusisha na vitendo vya mapenzi ya jinsia moja.
Lakini imetushangaza wengi siku za karibuni Hamisi Kigwangalla huyohuyo akijikomba kwa mtangazaji wa kipindi cha The Ellen Show cha nchini Marekani ambaye amefunga ndoa na mwanamke mwenzie ambapo mtangazaji huyo aliambatana na mke wake kwenye ziara yao ya siri ya honeymoon waliyofanyia Tanzania.
Licha ya wao kutotaka kujulikana location waliyopo, Waziri Kigwangalla alionekana akiwa anachangia mara kwa mara kuwaomba wawili hao waweke hashtag yenye neno TANZANIA.
Sasa hoja na swali la msingi ni:- Je, msimamo wa Kigwangalla juu ya uwepo wa mashoga na wasagaji ni upi?
Lakini imetushangaza wengi siku za karibuni Hamisi Kigwangalla huyohuyo akijikomba kwa mtangazaji wa kipindi cha The Ellen Show cha nchini Marekani ambaye amefunga ndoa na mwanamke mwenzie ambapo mtangazaji huyo aliambatana na mke wake kwenye ziara yao ya siri ya honeymoon waliyofanyia Tanzania.
Licha ya wao kutotaka kujulikana location waliyopo, Waziri Kigwangalla alionekana akiwa anachangia mara kwa mara kuwaomba wawili hao waweke hashtag yenye neno TANZANIA.
Sasa hoja na swali la msingi ni:- Je, msimamo wa Kigwangalla juu ya uwepo wa mashoga na wasagaji ni upi?