Waziri Hamisi Kigwangalla amemsimamisha kazi mkuu wa kanda Pori la Akiba Rukwa, Emmanuel Barabara

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
pic%2Bmaliasili.jpg


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla amemsimamisha kazi mkuu wa kanda Pori la Akiba Rukwa lililopo wilayani Mlele mkoani Katavi kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.

Taarifa ya Kaimu Katibu Mkuu, Dk Aloyce Nzuki iliyotolewa jana Machi 10,2018 inasema waziri amemsimamisha kazi Emmanuel Barabara ambaye pia ni mhifadhi wanyamapori mkuu.

Dk Kigwangalla amefikia uamuzi huo kutokana na taarifa za raia wema kuwa Barabara amekuwa akishirikiana na majangili kuhujumu rasilimali za misitu nchini.

Waziri Kigwangalla katika taarifa hiyo ameagiza iundwe kamati ya uchunguzi kubaini ukweli wa tuhuma hizo.

Amesema iwapo mtuhumiwa atatiwa hatia, hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa umma ili iwe fundisho kwa wengine.

“Tunatoa onyo kali kwa watumishi wa wizara wanaojihusisha na vitendo vya uhujumu wa rasilimali za misitu, wanyamapori na mali kale. Tunawataka waache mara moja kwa kuwa hatutosita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo, ikiwemo kufukuzwa kazi,” amesema.

Amewataka watumishi wa wizara kuzingatia sheria, kanuni, utaratibu na miongozo iliyowekwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku ya uhifadhi wa rasilimali za nchi kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
kigwa.jpg
 
Back
Top Bottom