#COVID19 Waziri Gwajima: Viongozi wa Serikali wasiochanjwa waachie ngazi

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,312
24,171
Waziri wa Afya, Dorothy Gwajima karudi na rungu.

Ametoa rai kuwa viongozi ambao mpaka sasa hawajachanjwa, watatakiwa waachie ngazi kwani hawawezi kusimamia kampeni ya kusimamia uchanjwaji dhidi ya corona.

Waziri wa Afya amesema kama Rais kachanja ili iwe mfano, sasa hao viongozi hawatetei msimamo wa Serikali

Tulisha liona hili huko nyuma: #COVID19 - Kuchanja sasa kuwe lazima, hasa wafanyakazi serikalini. Chanja au achia ngazi

 
Waziri wa Afya Dr. Dorothy Gwajima amewataka viongozi mbali mbali wa serikali ambao hawajachanjwa dhidi ya ugonjwa wa COVID-19 kuachia nafasi zao kwani wameshindwa kuwahamasisha wananchi kupokea chanjo hiyo.

SOURCE: ITV Habari
 
Waziri wa afya Dr Dorothy Gwajima amewataka viongozi wite wa serikali ambao hawajachanjwa chanjo ya Corona waavhie ngazi mara moja.

Waziri Gwajima amesema kiongozi asiyechanja hawezi kuwa na hamasa ya kushswishi watu wengine Wachanjwe ndio maana mimi kama waziri natoa ushauri wajiuzulu nafasi zao mara moja.

Source: ITV habari
 
Back
Top Bottom