#COVID19 Waziri Gwajima: Tanzania maambukizi yafikia watu 47 toka 14 kwa siku

Zile tetesi kwamba chanjo ya J&J inasababisha kuganda kwa damu kwenye ubongo, serikali imetolea ufafanuzi? Ikumbukwe wananchi wengi walipatiwa hizo chanjo.



Acha story za vijiwe vya kahawa..
 
Atupe maelekezo tuliochanja J and J tunaweza kuchanjwa Moderna au Pfizer naona Israel wanachanja mpaka chanjo ya 4 wengine sio wafuasi wa tapeli Askofu Gwajima
[/QUOl duh ! Wasi Wasi ndo akili lkn , mpaka Dec 2022 tutakuwa na majiwimbi ya kutosha.. Mungu atusaidie
 
Nabii, Mtume, Askofu Daktari Rashid Gwajima alidai amepewa dhima ya kuilinda Tanzania dhidi ya Uviko sasa kulikoni?
 
Nimecheki kwenye ukurasa wa Wizara ya afya huko Twitter, naona waziri aliteleza labda...
View attachment 2054332
Pale wizarani Kuna watu wanna busara Sana,huwa wanamfunika nguo,Kuna siku tena alibwatuka viongozi ambao hawajachanjwa waachie ngazi, wizara tena ikadai watu wamemuelewa vibaya.
Hii tena ya watu kufa nilimuona ITV, tulikuwa na jamaa wengine tunacheki waanza kumrushia matusi🤣🤣🤣🤣.
 
Pale wizarani Kuna watu wanna busara Sana,huwa wanamfunika nguo,Kuna siku tena alibwatuka viongozi ambao hawajachanjwa waachie ngazi, wizara tena ikadai watu wamemuelewa vibaya.
Hii tena ya watu kufa nilimuona ITV, tulikuwa na jamaa wengine tunacheki waanza kumrushia matusi🤣🤣🤣🤣.
Dah! Kweli uwezo wa kuwasilisha ujumbe ni kipawa. Mama inabidi aidha afanye mazoezi kabla ya kuongea na umma, au aandikiwe asome au amuachie mtu mwenye uwezo wa kutoleta mkanganyiko. Sekta ya afya ni nyeti kuifanyia makosa ya mara kwa mara.
 
Aliteleza waziri,au aliyeandika aliyoyasema waziri ndo kateleza?
Au ni marekebisho mwandishi kafanya kutokana na kauli ya waziri
Maswali mazuri Mkuu. Kwa kuwa siko wizarani sielewi makosa yamefanyika wapi. Ila ni rahisi kuteleza ukiongea kuliko ukiandika.
 
WAZIRI DK DOROTHY GWAJIMA AZINDUA MPANGO WA JAMII HARAKISHI NA SHIRIKISHI WA CHANJO YA COVID -19 AWAMU YA PILI

===
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amezindua Kampeni Harakishi na Shirikishi kwa Jamii awamu ya pili na kusema, changamoto za uwepo wa UVIKO 19 ni changamoto kwa maendeleo ya dunia nzima ikiwemo na Tanzania.

Dkt. Gwajima, ameyasema hayo leo Desemba 22, 2021, mkoani Arusha, ambapo Hafla hiyo imefanyika na kuhudhuriwa na Viongozi wa Serikali, Dini pamoja na Jamii sambamba na Wananchi wa Arusha na Mikoa ya Jirani.

Akizindua Mpango huo, Dkt. Gwajima, amesema, katika kipindi cha kuanzia Mwezi Disemba, 2021 nchi yetu pia imeshuhudia kuendelea kuongezeka kwa maambukizi mapya ya UVIKO-19 kutoka maambukizi 14 kwa siku hadi 47 miongoni mwa wasafiri kwa takwimu za vipimo vya maabara kuu ya taifa.

"Mafanikio ya mapambano haya yanategemea zaidi jinsi gani Wakuu wa Mikoa na vyombo vyenu mmeendelea kujipanga kila siku, kwa kuboresha mikakati ya kuwafikia wananchi hadi ngazi ya mitaa, vijiji na vitongoji ili waelimike wajikinge na wapate huduma ya chanjo. Alisema Dkt. Gwajima.

Kampeni ya kaya kwa kaya ya kuwashirikisha viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji inadhamira ya kuona mikoa mingine inafanya na kupata mafanikio makubwa zaidi kama Mwanza, Kagera na Ruvuma ilivyofanikiwa.

Dkt. Gwajima ametumia fursa hiyo, kuwaomba, Viongozi wa Mikoa na Halmashauri wanakua bega kwa bega ili kufikia azma yakuchanja watu wapatao 4000 hadi 5000 kwa Mkoa na watu 80,000 hadi 100,000 kwa nchi nzima kila siku.

Akitoa taarifa wakati wa hafla hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi alisema, kwa sasa wameanza kufanya utafiti wa chanjo na wataendelea kutoa taarifa wapi tumefikia kwenye Chanjo hiyo, aidha "kwa sasa nchi ina mitambo ya kufua hewa ya Oksijeni kwenye hospitali zetu, hii itasaidia kuokoa maisha kwa wahitaji wa hewa kama watoto njiti na wagonjwa wengine mahututi" Prof.Makubi.

Akiongea kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa, Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa, nchini ambaye pia ni Mkuu wa Arusha, John Mongella, alisema, wamejipanga kutekeleza maelekezo ya Serikali.

"Mhe Waziri, sisi ni Wasaidizi wa Mhe. Rais, hii ajenda ameibeba mwenyewe Rais, kwa kuanza kuchanja, na sisi wengine baada yakuona amechanja, Wakuu wa Mikoa wote tukachanja, hii ni kuonesha kuunga mkono mapambano haya" alisema Mongela.

Naye Prof. Riziki Shemdoe, Katibu Mkuu Tamisemi, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ummy Mwalimu, alisema, Mpango Harakishi na Shirikishi ni Mpango unaosimamiwa na Wizara zote ndio maana katika Kampeni hiyo wanashirikiana pamoja hasa ikizingatiwa kuwa Wizara hiyo ndio iliyo karibu zaidi na Wananchi.

Akitoa Salaam za Kamati ya Bunge, Mwenyekiti, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi Mhe. Fatma Tofiq, amesema wanaihakikishia Serikali, kuwa bega kwa bega katika kusukuma ajenda ya Chanjo. Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Dkt. Stanslaus Nyongo amempongeza Wizara ya Afya kwa namna ilivyoweza kutekeleza Maekezo ya Serikali pamoja na yale ya Bunge

^Mhe. Waziri kwaniaba ya Kamati ya Bunge, niwapongeze sana kwa jinsi mnavyotekeleza Maelekezo ya Bunge, lakini pia ya Serikali, niahidi kwaniaba ya Kamati kuendelea kukupa Ushirikiano wakati wote na kuwashauri inavyopaswa" Alisema Mhe. Nyongo.

Katika Hafla.hiyo, Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima aliitaja Mikoa vinara kwa Chanjo yaani iliyofanya vizuri katika Chanjo mpaka sasa kuwa ni Ruvuma, Mwanza, Dodoma, Kagera na Mara. huku akiitaka Mikoa mingine kuongeza bidii

View attachment 2053776



View attachment 2053779

View attachment 2053780

View attachment 2053781

View attachment 2053783
Bado nahoji ukweli wa hizi takwimu. Hao watu 100,000 kwa siku Tanzania hii wako wapi?
 
Dah! Kweli uwezo wa kuwasilisha ujumbe ni kipawa. Mama inabidi aidha afanye mazoezi kabla ya kuongea na umma, au aandikiwe asome au amuachie mtu mwenye uwezo wa kutoleta mkanganyiko. Sekta ya afya ni nyeti kuifanyia makosa ya mara kwa mara.
Kweli kabisa.
Tatizo yeye anataka kumufurahisha Hangaya kwa gharama za maisha ya watu,na Hangaya anavyopambana kupata 50/50 ili asifiwe na wazungu,ni vigumu kutengua uteuzi wa mwanamke.
 
Team JF,


MERRY CHRISTMAS AND HAPPY NEW YEAR 2022.

#TUENDELEE KUMUUNGA MKONO RAIS WETU,
 
WAZIRI DK DOROTHY GWAJIMA AZINDUA MPANGO WA JAMII HARAKISHI NA SHIRIKISHI WA CHANJO YA COVID -19 AWAMU YA PILI

===
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amezindua Kampeni Harakishi na Shirikishi kwa Jamii awamu ya pili na kusema, changamoto za uwepo wa UVIKO 19 ni changamoto kwa maendeleo ya dunia nzima ikiwemo na Tanzania.

Dkt. Gwajima, ameyasema hayo leo Desemba 22, 2021, mkoani Arusha, ambapo Hafla hiyo imefanyika na kuhudhuriwa na Viongozi wa Serikali, Dini pamoja na Jamii sambamba na Wananchi wa Arusha na Mikoa ya Jirani.

Akizindua Mpango huo, Dkt. Gwajima, amesema, katika kipindi cha kuanzia Mwezi Disemba, 2021 nchi yetu pia imeshuhudia kuendelea kuongezeka kwa maambukizi mapya ya UVIKO-19 kutoka maambukizi 14 kwa siku hadi 47 miongoni mwa wasafiri kwa takwimu za vipimo vya maabara kuu ya taifa.

"Mafanikio ya mapambano haya yanategemea zaidi jinsi gani Wakuu wa Mikoa na vyombo vyenu mmeendelea kujipanga kila siku, kwa kuboresha mikakati ya kuwafikia wananchi hadi ngazi ya mitaa, vijiji na vitongoji ili waelimike wajikinge na wapate huduma ya chanjo. Alisema Dkt. Gwajima.

Kampeni ya kaya kwa kaya ya kuwashirikisha viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji inadhamira ya kuona mikoa mingine inafanya na kupata mafanikio makubwa zaidi kama Mwanza, Kagera na Ruvuma ilivyofanikiwa.

Dkt. Gwajima ametumia fursa hiyo, kuwaomba, Viongozi wa Mikoa na Halmashauri wanakua bega kwa bega ili kufikia azma yakuchanja watu wapatao 4000 hadi 5000 kwa Mkoa na watu 80,000 hadi 100,000 kwa nchi nzima kila siku.

Akitoa taarifa wakati wa hafla hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi alisema, kwa sasa wameanza kufanya utafiti wa chanjo na wataendelea kutoa taarifa wapi tumefikia kwenye Chanjo hiyo, aidha "kwa sasa nchi ina mitambo ya kufua hewa ya Oksijeni kwenye hospitali zetu, hii itasaidia kuokoa maisha kwa wahitaji wa hewa kama watoto njiti na wagonjwa wengine mahututi" Prof.Makubi.

Akiongea kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa, Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa, nchini ambaye pia ni Mkuu wa Arusha, John Mongella, alisema, wamejipanga kutekeleza maelekezo ya Serikali.

"Mhe Waziri, sisi ni Wasaidizi wa Mhe. Rais, hii ajenda ameibeba mwenyewe Rais, kwa kuanza kuchanja, na sisi wengine baada yakuona amechanja, Wakuu wa Mikoa wote tukachanja, hii ni kuonesha kuunga mkono mapambano haya" alisema Mongela.

Naye Prof. Riziki Shemdoe, Katibu Mkuu Tamisemi, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ummy Mwalimu, alisema, Mpango Harakishi na Shirikishi ni Mpango unaosimamiwa na Wizara zote ndio maana katika Kampeni hiyo wanashirikiana pamoja hasa ikizingatiwa kuwa Wizara hiyo ndio iliyo karibu zaidi na Wananchi.

Akitoa Salaam za Kamati ya Bunge, Mwenyekiti, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi Mhe. Fatma Tofiq, amesema wanaihakikishia Serikali, kuwa bega kwa bega katika kusukuma ajenda ya Chanjo. Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Dkt. Stanslaus Nyongo amempongeza Wizara ya Afya kwa namna ilivyoweza kutekeleza Maekezo ya Serikali pamoja na yale ya Bunge

^Mhe. Waziri kwaniaba ya Kamati ya Bunge, niwapongeze sana kwa jinsi mnavyotekeleza Maelekezo ya Bunge, lakini pia ya Serikali, niahidi kwaniaba ya Kamati kuendelea kukupa Ushirikiano wakati wote na kuwashauri inavyopaswa" Alisema Mhe. Nyongo.

Katika Hafla.hiyo, Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima aliitaja Mikoa vinara kwa Chanjo yaani iliyofanya vizuri katika Chanjo mpaka sasa kuwa ni Ruvuma, Mwanza, Dodoma, Kagera na Mara. huku akiitaka Mikoa mingine kuongeza bidii

View attachment 2053776



View attachment 2053779

View attachment 2053780

View attachment 2053781

View attachment 2053783
Tukachanje
 
Miradi yote iliyoachwa na Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli Rais Samia Suluhu Hassan anaitekeleza kwa 100%

Sihiyo tu tayari mingine mipya inaendelea na Ujenzi,

Tunawajibu wa kumwombea Mama huyu,
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom