Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 9,995
- 34,607
Huyu waziri hana Akili sawa sawa.Kwa mujibu wa Dkt. Gwajima, huku kumeathirika zaidi:
“Maeneo ya kanda ya ziwa pamoja na Kilimanjaro yameathirika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa huo, na ilihitajika mitungi ya ziada kutokana na eneo la kanda ya ziwa kuathirika zaidi na ugonjwa huo,” alisema Gwajima."
Mwenye masikio na asikie:
“Nataka hapo wananchi watuelewe, tuvae barakoa, tunawe mikono na maji tiririka pia tujiepushe na misongamano isiyo ya lazima. Katika wakati huu hakuna ulazima wa mtu kwenda katika miziki au kupanda katika gari lililojaza watu,” amesisitiza Dk Gwajima."
--------
My take:
Tahadhari zaidi maeneo hayo ikiwamo kupunguza safari zinazoweza kuepukika, kutoka au kwenda maeneo hayo ni jambo la busara zaidi.
Taarifa yake imekaa kisiasa badala ya kuakisi uhalisia.
Waziri anapaswa kuja na taarifa yenye takwimu kuhusu wagonjwa na vifo vinavyohusiana na Corona nchi nzima ili tujijue tuko kwenye hali gani.