sblandes
JF-Expert Member
- Apr 25, 2010
- 6,120
- 4,229
Kweli kabisa kumbe mkataba ulikuwa bado haujasainiwa yale yalikuwa mapendekezo.It was an intial agreement between the two parts. Baada ya makubaliano yale ndio usainishaji wa mkataba wenyewe ungefuata. Waziri yuko sahihi kuwa mkataba haukusainiwa na aliyeshindwa kutoa maelezo vizuri mbele ya wananchi ni Magufuli.
Nakumbuka Magufuli akisema tutaendelea kufanya majadiliano.
Na yule aliekuwa bosi wa Bandari alizungumzia mapungufu yaliyomo kwenye muswaada.
Magufuli alitafuta njia mbadala kwa kuzijengea bandari zote uwezo na kupuuza Bagamoyo project.
Na China ilivyogundua kuwa Magufuli hapendi kabisa mapendekezo ya mkataba, ndipo nao Wachina wakajiongeza kufanya lobbying kupitia watu mashuhuri mmojawapo ni Spika Ndugai alipoitembelea China.
Lakini asiyependa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo si Magufuli tu bali hata nchi jirani kama Kenya,Mozambique na hata South Africa,sababu ya maslahi kwa nchi zao.
Lakini kwa awamu ya uongozi wa SSH kuna uwezekano mkubwa Bandari ya Bagamoyo kujengwa baada ya kufikia makubaliano na wabia wa China.